Kimilidzo
JF-Expert Member
- Jan 3, 2011
- 1,346
- 627
Jumamosi asubuhi nilihamisha hela kwa NMB Mobile toka account yangu ya benki kuja kwenye namba ya simu kwa njia ya MPesa jumla ya shilingi laki mbili. Toka hiyo Jumamosi hadi Leo Jumatatu hela yangu haijafika, nimepiga simu zaidi ya mara 60 kwenye customer service yao sijafanikiwa kuzungumza na mtoa huduma licha ya kwamba kuna wakati nimekaa hewani dakika 18 wananiimbia nyimbo Tu huku namaliza charge kwenye simu yangu.
Nilikuwa naihitaji hiyo hela Jumamosi nimekwamishwa, nimeulizia watu wengine wameniambia imeishawatokea kusubiri hadi wiki nzima ndio hela ikahama.
Wito wangu kwa BOT, haya makampuni ambayo kutoa huduma za hovyo ndio sera zao msiwape leseni ya kutoa huduma sensitive kama za mobile money, wanatutesa na kutunyanyasa wateja na hatuna mtetezi. Hapa nilipo hela haipo kwenye account na haipo kwenye simu kwa siku mbili, nini haki yangu. NMB Ni janga la kitaifa, ingawa tumejiunga kwa sababu za ukabwela wetu, tunaomba mtuthamini walau kidogo.
Nilikuwa naihitaji hiyo hela Jumamosi nimekwamishwa, nimeulizia watu wengine wameniambia imeishawatokea kusubiri hadi wiki nzima ndio hela ikahama.
Wito wangu kwa BOT, haya makampuni ambayo kutoa huduma za hovyo ndio sera zao msiwape leseni ya kutoa huduma sensitive kama za mobile money, wanatutesa na kutunyanyasa wateja na hatuna mtetezi. Hapa nilipo hela haipo kwenye account na haipo kwenye simu kwa siku mbili, nini haki yangu. NMB Ni janga la kitaifa, ingawa tumejiunga kwa sababu za ukabwela wetu, tunaomba mtuthamini walau kidogo.