Njia ya kimila ya kuwakomoa walafi

Njia ya kimila ya kuwakomoa walafi

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
12,212
Reaction score
23,258
kutokana na baadhi ya watu kutokua wasitaarabu wakati wa kula, mababu zetu walitumia njia mbalimbali kuwakomesha walafi.

kuna uchawi wa zongo huu upo sana maeneo ya Tanga, ukifika tanga kama usipokuwa mstaarabu unapigwa ZONGO (zongo ni uchawi Wa kuvimbisha tumbo) tumbo linavimba kama kama mama mjamzito, ukionekana kutoacha ulafi


Usipo acha ulafi wanakutupia kajini kadogodogo wakati Wa kula (hakaonekani kwa wote bali kwako tu) kanakuwa kana kupiga makofi wakati wa kula, ukiwa bado mvumilivu kwa umahili Wa kukwepa hayo makofi;

Basi utaongezewa kajini kengine kabaunsa, haka kajini kazi yake ni kukushikilia mikono wakati Wa kula hadi wenyeji washibe; (Hakaonekani kwa wote Bali kwako tu) baada ya chakula kinakuachia....Utasonya utavimba lakini potelea mbali hutasema kilichokutokea.

Tukiachana na uchawi Wa Tanga,Twende Huko morogoro kuna kabila la wadamba, kiboko ya roho mbaya, ukijitia mlafi wakati wa kula kuna style yao ya kimila yaani wanakunja vidole Vitatu vya mwisho kwa ustadi,baada ya hapo kitakachokupata wewe Mgeni unakuwa kama umekabwa kooni- unapaliwa chakula utakohoa mishipa yote itakusimama. huwezi tena thubutu kuendelea kula chakula kwa kabali zile,
Hivi ndivyo walafi wanashughulikiwa.
 
Sio kuwakomesha walafi huo unakuwa ni uchoyo tu, acheni watu wale.

Kuna Dogo alifariki baada ya kukabwa na nyama na alikuwa anakula na Mzee , Dogo alitangulia kuchukua nyama kabla ya wakubwa.
kuna miiko ya kula na wakubwa! dogo alichemka ,watu wakakunja vidole nahisi
 
Sio kuwakomesha walafi huo unakuwa ni uchoyo tu, acheni watu wale.

Kuna Dogo alifariki baada ya kukabwa na nyama na alikuwa anakula na Mzee , Dogo alitangulia kuchukua nyama kabla ya wakubwa.
hata vitabu vitakatifu vinaonya juu ya ulafi
 
Ukiwa Mgeni wa maeneo hayo jiongeze wakati mwingine kale hotelini ,kiosk,au hata kwa mama Lishe Sasa tabu yoote hadi vijinibaunsa ya Nini TUUWANE BURE SABABU YA TONGE!
 
Ukiwa Mgeni wa maeneo hayo jiongeze wakati mwingine kale hotelini ,kiosk,au hata kwa mama Lishe Sasa tabu yoote hadi vijinibaunsa ya Nini TUUWANE BURE SABABU YA TONGE!
ni kwa walafi tu hufanyiwa hivo
 
Back
Top Bottom