Njia haramu za kuingia Ulaya zaongezeka

Njia haramu za kuingia Ulaya zaongezeka

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,361
Reaction score
4,816
Takwimu mpya zinaonesha idadi ya wakimbizi wanaoingia katika mataifa ya Umoja wa Ulaya kwa njia haramu mwaka huu zimeongezeka kwa asilimia 46 ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Hayo yameibuliwa katika ripoti ya Halmashauri ya Umoja wa Ulaya. Njia nyingi haramu ziliundwa kwa kuingilia Ugiriki na makundi makubwa ya wakimbizi yalikuwa kutoka Afghanistan.

Katika makubaliano ya Umoja wa Ulaya na Uturuki ya mwaka 2016, Uturuki ilipaswa kuimarisha ulinzi wa mipaka yake, katika namna ya kudhibiti wahamiaji wasiweze kuingia tena kinyume cha sheria. Kwa zingatio la makubaliano hayo Uturuki ilipaswa kupewa kiasi cha euro bilioni sita ili kuwa na uangalizi wa karibu kwa wakimbizi.
 
Sijui kwanini Sina hata chembe ya mshituko wa kwenda huko
sio wewe tu watanzania wengi hatuwazagi kutafuta nje ya wilaya/mkoa/kanda/nchi yetu.

yaani ni waoga wa changamoto si kdg,tunawaza kula ugali hadi kufa.kuna mtu wa mkoa hata umpe m.5 ahamie dar hawez kubali
 
sio wewe tu watanzania wengi hatuwazagi kutafuta nje ya wilaya/mkoa/kanda/nchi yetu.

yaani ni waoga wa changamoto si kdg,tunawaza kula ugali hadi kufa.kuna mtu wa mkoa hata umpe m.5 ahamie dar hawez kubali
Kweli kabisa,niliona taarifa moja wakongo kibao wameweka kambi mexico wakisubiri kuingia US,cha ajabu mexico inawabembeleza waishi pale lakini hawataki,angalia umbali Wa kutoka Congo mpaka mexico lakini watu wanajitoa kwa gharama zozote wafike wanapotaka hafu ni watu Wa kawaida kama sisi.
 
Sijui kwanini Sina hata chembe ya mshituko wa kwenda huko
Ujamaa bado upo ndani yetu na maisha ya Bongo ukujishughulisha kidogo tu hukosi pesa ya kupata msosi. Huwa na amini Tanzania ingekuwa na viongozi wazuri na nchi ingestawi, ingekuwa kimbilio la Waafrika wengi sana.
 
Back
Top Bottom