Njia gani nitumie kudai deni?

kindaboyi

Member
Joined
Apr 5, 2018
Posts
23
Reaction score
23
Nimemfuata kiustarabu imeshindikana, nimemfuata kiukali lkn wap, nimeongea na watu wake wa karibu pamoja na familiya yake nimeambulia patupu, nikamtishia kumpeleka mahakamani akasema hatukuandikishiana popote hamna shahidi, sasa jamani nitumie njia gan nyingine nilipwe deni langu? Naombeni ushauri
 
Kudai Deni ni mtihani mkubwa sanaa...
Kuna Watu itokee tu ila hana njia utatumia kukunjua moyo wake.

Utumie lugha ya busara olaa..
Utumie mlango wa dini olaaa,
Utumie biti olaaa,
Umtishie kipira olaaa,
Utumie ubabe olaaa...

Na usiombee Mdeni wako ajue kama huna pa kushikiaaa...

Kurudisha Deni ni busara na shukrani za mtu, kitu ambacho wengi tumekosa.
 
Ungekua na ushahidi ningekushauri uende mahakamani hutapata hela yako yote kwa pamoja ila utalipwa.
 
Zipo njia mbili na ngumu kidogo mie niliona zimefanikisha kwangu,nenda kwake kakae sebulen usindoke hd amekupa chako kaa hapo,kula hapo mda wote mkewe akuone upo ht km ni wiki mbili kaa hapo,pili fanya upelelezi ujue siku yupo nyumban esp jumapili asbh ya saa nne anzia mtaa pili vua nguo watu wakianza kukufuata kwa wingi tembea hadi kwake zama ndani hutoki humo hadi ulipwe,km utaweza fanya hivo
 
For sure [emoji817]
 
Reactions: Lis

Hana mali huyo mtu unayemdai?
 
Hii njia ya kwanza lazima ntaitumia
 
Mpeleke kwa mjumbe au serikali za mtaa, au mahakamani kama ulivyosema awali. Akikubali unamdai mnnaandikishana namna ya kukulipa.

Akikukataa hujamkopesha muulize mara mbilimbili akizidi kukataa nawa/futa mikono angalia juu sema maneno muachie Mungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…