Njaa isitufanye kujivunjia heshima

Njaa isitufanye kujivunjia heshima

Incredible

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
1,031
Reaction score
1,603
Leo nimesoma kwenye gazeti la Nipashe Kitila Mkumbo akitetea rais alivyoingiza msimamo wa CCM siku alipozindua Bunge La Katiba. Nipashe limeandika hivi:

Dk. Mkumbo alisema anaunga mkono hatua ya Rais KIkwete kubainisha bungeni msimamo wake juu ya mchakato huo, hasa katika suala la aina ya mfumo wa muungano wa serikali mbili au tatu.

Alisema Kikwete angekuwa Rais wa kwanza wa ajabu duniani kama asingeonyesha msimamo wake na kwamba, pamoja na masuala mengine, huo ndiyo unaotakiwa kujadiliwa na kutumia nguvu za hoja kuonyesha udhaifu wake.

"Wamkosoe au wamuunge mkono kwa hoja, Bunge liendelee lakini kwa sasa wengi wana mihemuko ya uchaguzi mkuu ujao, Bunge hili liahirishwe ili Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania liendelee na lifanyie marekebisho Sheria ya Mabadiliko ya Katiba," alisema Dk. Mkumbo.

Sasa hawa wasomi wetu wanaelekea wapi? JK mwenyewe alijua na anajua kwamba amekosea. Sasa huyu msomi wetu anataka apate utajiri kwa kulamba watu miguu, atafanikiwa kweli?
 
Incredible;
Kitila ni haki yake amsifie JK. Huko kwetu tunasema ni kurudisha fadhila. Si ajabu hata JK atakapo endelea tena miaka 2. (Kwani kila dalili inaonesha) ataweza kumpa hata ukatibu mkuu wa sheria. Kwa JK yoote yawezekana.
Lakini, kuliko kujitia ujuha ili upate kukumbukwa na mkuu ni aheri kufa maskini. Mwl. aliwahi kusema; Heri tulale njaa kuliko kujikomba kwa hao wanaosema wanacho.
Maskini Kitila, umekumbwa na nini?? Mbona ulikuwa shpavu saana?
 
Never trust politicians they are unpredictable!! They don't mean what they say and they say what they don't mean
 
Never trust politicians they are unpredictable!! They don't mean what they say and they say what they don't mean

uko sawa lakini mimi nitakua na yeyote anaesema yuko CDM na akitoka mi nitabaki mpaka mwisho
 
Dr Kitila yuko sahihi kwa mtazamo wake wa sasa wenye mawazo yasiyo ganda na wakati. Kinachogomba si kile alichokisema yeye bali ni Kuwa kasema kinyume na kile ambacho ulitaka na kutazamia aseme ulivyotaka wewe aseme. Na huo ndio uhuru wa mawazo. Cha msingi ni kuchambua uzito wa hoja yake kwa sasa na si tuhuma ambazo ni vigumu kuzithibitisha. Kinyume na hapo utakuwa mvunja demokrasia mkubwa. Kumbuka kuna WATU waliuliwa kwa kauli tu Kuwa DUNiA inazunguka Jua na baada kumuua wote waligeuka na kukubali Kuwa DUNiA inazunguka JUA. Ni vizuri Kabla ya kujenga msimamo tukapima hoja.
 
Kitila na mwigulu wanatoka sehemu moja na wanafikiri namna moja na kusema mambo yanayofanana. What a coincidence. Kweli mkumbo alikuwa msaliti.
 
Back
Top Bottom