Nitoke nje ya ndoa?


Mmmhhhhhh... Lait huyo mkeo tungempa nafasi na yey ajielezee nahis angesema meng sana unayomfanyia, wanawake tuna huruma sana na mpaka mtu akifikia hatua anakuonaona tu kam mtu na viugomvi bas ujue na wew unatatizo sema ndo hvyo wanaume mnapenda ubabe na kuonekana hamtendewi haki
 
25 years ndoani tayari...
duh ndoa ina miaka mingapi hiyo?
 
Huku nje unakotaka kuja unajua kukoje,kumbuka huo MOTO unaowaka ndani kwako ulitoka nje hukuhuku,nafasi zenyewe huku nje zimejaa sisi wenyewe tunataka ingia huko ndani ulipo mchungaji.
 
Kisa cha kuoa mapema nn.?? Pole wee..uliingia akili ikiwa haijakomaa c bure...wenzio wanaoa wakiwa 30 akili zishakomaaa

akili itakomaa hukohuko kwenye ndoa! bila ndoa pengine angekuwa anaendelea kumkosea muumba wake kwa kula tunda la mti wa kati!!!
 

mwache aoe...maisha mafupi sana siku hizi!!! maana kwa vijana wenye miaka 20-25 kufika miaka 40 au 50 ni ndoto, lifespan imepungua sana!!! muda haumsubiri mtu...
 

Source ya tatizo hasa ni nini!? maana ka alikupenda na umaskini wako ndo akubadilikie ghafla baada ya kuoa!? au mlipitia stage ya uchumba wiki 1?
 
Ok pole. Ukiona maombi yako yanakosa majibu washirikishe na wenzio. Nenda hapo kkkt kwa maksai atakuombea....................................... Kibongo bongo hakuna mwanamke atakayetaka kupokea mastress yako labda naye awe na shida ya vijisenti vyako.
 

Tatizo lako wewe ni mbishi... Unapoambiwa wewe ni mdogo kuingia kwenye ndoa kubali. Yes una busara, lakini hazitoshi kuhimili mikiki mikiki ya ndoa. Mfano mdogo ndio kama yanayokukumba sasa. Ungekuwa na busara za kutosha wala yasingekuumiza kichwa na akili kama yanavyokuumiza sasa.
Kwa umri ulionao huo ukienda nje ya ndoa ndio unaenda kujichimbia kaburi.

Mimi nakushauri kitu kimoja. Kuanzia sasa anza kuishi kama vile hujaoa. Usimuache mkeo, lakini pia usimchukulie kama mke. Mchukulie kama rafiki tu anayeishi katika nyumba yako. Kama mna mtoto/watoto we peleka care kwa watoto. Akinuna, akigomba, akilia, akicheka, usijali. Jali maisha yako mengine, but usiwaze tena kuhusu ndoa yako. Kama ni kulala, akikataa usilale kitandani, kalale chumba kingine au sebuleni. Usijaribu kabisa kumuomba au kutaka kufanya naye mapenzi. Kama ni chakula akipikupa kula, asipokupa kale kwa mama ntilie.

AMUA kuishi maisha kama hayo kwa muda utakaojipangia ama MIEZI 3 au 6. Strickly that way, yaani usimjali kwa lolote. Kwa kifupi chukulia kama hayupo humo ndani. Ni ushauri mgumu mgumu kidogo but matatizo magumu yanahusu maamuzi magumu, maana usipochukua hatua, ama utaua au utajiua au utakufa...
 
Reactions: Luv
Kumuulza mwenyewe haitosh shrkisha na watu wengne

ndoa na maelewano ni ya watu wawili akidhirikisha wengine ni kujichoresha tu. nao wana matatizo yao tena makubwa zaidi. wakae waelewane
 
mie nashindwa hata kujilazimisha kuamini..naona ni hadithi tu..maana majaribu hutoa hadithi za aina hii hii.pengine kuna mtu anamsemea
 

mpaka 40 papuchi imegegedwa mpaka basi loh
 
akili itakomaa hukohuko kwenye ndoa! bila ndoa pengine angekuwa anaendelea kumkosea muumba wake kwa kula tunda la mti wa kati!!!

dah wee umenena...wengibe wote wameleta porojo
 

...si kweli imekula kwake,, usimtishe....kwa umri wake ataishi maisha ya namna gani? Mungu hakutuumba tuishi bila amani au furaha, fuata taratibu mwaga kuleeee,,, rudi kwa Mungu omba msamaha utasamehewa.......jipange upya...
 

......yep maamuzi magumu.....sio miezi tuu,,, forever.....ila chakula pia asile....hawaeleweki hao,, akikutana na walimu huko nje atalishwa vipande vya uchafu ambavyo haviwezi kubalisha chochote .....uchafu tuu...
 

nyie ni wachokozi sana......wengi mko kwa kutaka kukopi kopi tuu....
 

Huyo mwanamke sio jini mkuu.. kuna uwezekano hakukupendia tangu mwanzo.Nakushauri ufanye uchunguzi kuna sababu ilimlazimisha
 
ndugu, umeacha kazi kwa sababu ya matatizo ya ndoa? unaishije sasa? huoni kuwa hilo linachangia hali ya sintofahamu kati yako na my wife wako? sasa unataka maza wa 35 hivi akutunze na kukufariji, mmmmh, ok. unadhani hilo ndiyo suluhisho? unapaswa kukaa chini na mwenzi wako, ikiwezekana washirikisheni watu wenu wa karibu, wazazi pande zote, viongozi wa dini, walezi wenu wa ndoa (if any), counselors watawasaidia kuwarudisha kwenye mstari, maisha ya ndoa/mahusiano yana mapito yake, usiyakimbie, bali kabiliana nayo kwa hekima na kwa akili nyingi...
 
dont do it
ongeza upendo kwake zawadi na vijisenti kibao na uoneshe upendo wa dhati msaidie kazi za home as well
na wakati wa ku do onesha unafanya kwa upendo sio dumbukiza tu!!!
 
Mtoto anapomuoa mtoto mwenzie na kukutana na majukumu huku akiwa hana Kazi, ww ulidhani kitakachofuata nn?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…