Ndugu wana ARUSHA!
Natangaza rasmi kuwa nitagombea ubunge wa jimbo la ARUSHA MJINI 2015 kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA),
huu ni uamuzi wangu binafsi na wa kidemokrasia kwa kuzingatia misingi ya sheria na katiba ya nchi pamoja na ya chama changu,
ninaamini ninazo hoja za msingi, uwezo na kipaji cha kipekee katika kutimiza azma yangu ya kuwatumikia wana Arusha na Taifa kwa ujumla.
Ninaamini ya kuwa, yapo mambo ya msingi sana ambayo yanahitaji uwepo wangu wa moja kwa moja katika kuyafanya na kuyasimamia mwenyewe kwani mtu mwingine hawezi kufanya kwa weledi kama nilivyokusudia mimi.
Natambua mengi mema aliyoyafaya na anayoyafanya Mhe LEMA, lakini pia ikumbukwe uwezo wetu wa kufikiri ni tofauti, anayoyafikiri Mhe LEMA inaweza isiwe ndivyo ninayofikiri mimi,
*NATAMANI KUONA MATUMAINI MAPYA KATIKA ARUSHA NA TAIFA LANGU,
*NATAMANI KUONA FIKRA MPYA NA ZENYE UHAI KATIKA NCHI,
*NATAMANI KIZAZI CHENYE MITAZAMO CHANYA KWA KUMAANISHA,
*NATAMANI KUONA MATOKEO MAPYA NA MATUNDA MEMA KATIKA VIWANGO VYA JUU ZAIDI KWA MAENDELEO YA ARUSHA NA TAIFA ZIMA,
NB: CHANGAMOTO HAI NA ZENYE MANUFAA HULETWA NA KIZAZI KINACHOFIKIRI SAWASAWA, mimi ni mmoja wapo.
Natambua ugumu uliopo katika safari hii hasa ikizingatiwa kuwa Mhe Lema ana wafuasi wengi, jambo hili ninanipa fursa nzuri ya kujiandaa vyema kama ilivyosemwa "BELIEF CREATES THE ACTUAL FACT" ALBERT EINSTEIN.
wenu
MWANAWAVITTO
Acha usngizi wa maluelue kwani wakufanya waota ndoto za alinacha,ndoto za maruerue ambazo ni heri ya ndoto za mchana.Mara hii ushasahau kipigo cha 4-bila???Mwee!!!Hilo jimbo litarudi ccm, piga ua garagaza. Hutaki unaacha
Kama una nia ya dhati si ungetaja jina lako na kuwela picha kabisa nashangaa unatoa tamko huku ukiwa umejificha ni nini hasa unaogopa?
View attachment 109250
Mbona uliamua kujibinua mimi nimekuweka sawa.
"unity?"
sidhani kama unatambua vema ni nini maana ya neno unity. Hapa hakuna confusion kwani confusion inakuja pale tunapoacha kuteteana na kukipigania chama! Hapo ndipo unity ina disappear,
Wanaarusha saivi wanajuta kwann walichagua mhuni
Lema kapambana na arusha imemkubali nakuomba utupe ata nafasi uliyowahi kushika katika huongozi wowote
Kwi kwi kwiiiiiiiii! Nilifikiri mtoa mada unatania kumbe umepania hahahahahaaaaaaaaaah! Yani hauna tofauti na mtu anayefikiri kuwa HILUX (pick up) ikikua inazuka FUSO.Mimi ndg yako labda nikusaidie tu maana usije ukapoteza muda na nguvu nyingi kutetea hoja yako hii,Kwa jinsi Lema alivyokubalika kwa wapiga kura wake wa Arusha mjini hadi kufikia hivi sasa hana mpinzani iwe ndani au nje ya CDM.Pamoja na kuwa hadi kufikia hapa ushajivua sifa ya kuwa mwanachama mtiifu kwa kukiuka taratibu za ndani za chama lkn bila kupepesa macho na kutafuna maneno nikuonye tu kuwa LEMA si size yako na kikubwa hapa nakushauri ukajifunze HADABU.
Kwanza tumpongeze kwa kuonyesha nia ya kupambana na jabali! Lema kabla alishika wadhifa gani tusipende kuuliza mtu alichofanya wakati lema anakubalika wakati kabla hakuwa historia kubwa
Muacheni atumie haki yake kikatiba apate uzoefu wa kupambana na jabali japo nina uhakika hakuna wakumtoa Lema Arusha si nje wala ndani ya CHADEMA.
Jimbo linaongozwa na mgonjwa kajitokeza mwendawazimu sijui nani atashinda kazi kwenu arusha.
Ndugu wana ARUSHA!
Natangaza rasmi kuwa nitagombea ubunge wa jimbo la ARUSHA MJINI 2015 kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA),
huu ni uamuzi wangu binafsi na wa kidemokrasia kwa kuzingatia misingi ya sheria na katiba ya nchi pamoja na ya chama changu,
ninaamini ninazo hoja za msingi, uwezo na kipaji cha kipekee katika kutimiza azma yangu ya kuwatumikia wana Arusha na Taifa kwa ujumla.
Ninaamini ya kuwa, yapo mambo ya msingi sana ambayo yanahitaji uwepo wangu wa moja kwa moja katika kuyafanya na kuyasimamia mwenyewe kwani mtu mwingine hawezi kufanya kwa weledi kama nilivyokusudia mimi.
Natambua mengi mema aliyoyafaya na anayoyafanya Mhe LEMA, lakini pia ikumbukwe uwezo wetu wa kufikiri ni tofauti, anayoyafikiri Mhe LEMA inaweza isiwe ndivyo ninayofikiri mimi,
*NATAMANI KUONA MATUMAINI MAPYA KATIKA ARUSHA NA TAIFA LANGU,
*NATAMANI KUONA FIKRA MPYA NA ZENYE UHAI KATIKA NCHI,
*NATAMANI KIZAZI CHENYE MITAZAMO CHANYA KWA KUMAANISHA,
*NATAMANI KUONA MATOKEO MAPYA NA MATUNDA MEMA KATIKA VIWANGO VYA JUU ZAIDI KWA MAENDELEO YA ARUSHA NA TAIFA ZIMA,
NB: CHANGAMOTO HAI NA ZENYE MANUFAA HULETWA NA KIZAZI KINACHOFIKIRI SAWASAWA, mimi ni mmoja wapo.
Natambua ugumu uliopo katika safari hii hasa ikizingatiwa kuwa Mhe Lema ana wafuasi wengi, jambo hili ninanipa fursa nzuri ya kujiandaa vyema kama ilivyosemwa "BELIEF CREATES THE ACTUAL FACT" ALBERT EINSTEIN.
wenu
MWANAWAVITTO