ungonella wa ukweli
JF-Expert Member
- Mar 27, 2012
- 4,210
- 555
Wana jamvi habarini, ni hivi nimemtongoza msichana ambaye kwa namna moja ama nyingine ambaye nimempenda kiukweli, tatizo ni kwamba ameathirika kisaikolojia kwa kuwachukia wanaume kwa sababu siku za nyumwa alitendwa na boy friend wake, hata hivyo mpaka sasa mambo bado hajaeleweka, yeye anadai kwamba kila akikumbuka maumivu aliyoyapata anakosa amani, na anasema bado hajawa tayari. Ndugu wana jamvi nifanyeje au mambo gani niyafanye kwa mrembo huyo ili niweze kuwa naye? Karibuni kwa ushauri wenu maana nimetokea kumpenda sana huyu binti!