MADINI CHUMA
Member
- Dec 25, 2013
- 29
- 9
Wadau, Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 23. Elimu yangu ni kidato cha sita na nimwanafunzi wachuo kikuu, ninamalengo ya kugombea ubunge jimbo la Mwibara. Sababu Zakugombea ni 1. Tunashida ya barabara tangu uhuru mpaka kesho kitu ambacho kimekuwa nikero kwa wananchi waliowengi 2. Elimu inadolola kila uchao lakini hakuna jitihada zozote za kuiweka sawa 3. Watu wamechoka na utawala dharimu wa ccm kwani hauna tija kwa wananchi waliowengi 4. Hakuna miradi yoyote ya maendeleo kama kilimo cha umwagiliaji kwani jimbo la mwibara limekuwa kinara wa kuomba misaada ya chakula kila kukicha Kulingana nahayo niliyo yasema hapo juu, nimeona ni vyema kugombea nafasi hiyo kupitia cdm ili tuasaidiane na wananchi wa mwibara kujikomboa katika lindi kubwa la umaskini. Nawaomba wananxhi wenzangu wa mwibara tushirikiane kuyafanikisha haya.