X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,809
Ukiyaonja mapenzi utaujuwa utamu
Ndipo utapoyaenzi ukayaona adhimu
Nakupenda Mwenye enzi Ilahi Mola Karimu
Nisikupende kwa nini Nawe Umenikirimu
Nisikupende kwa nini Ya Ilahi ya Karimu
Nawe umenithamini kuniumba mwanadamu
Ukaniongeza shani Kwa dini ya Isilamu
Nisikupende kwa nini Nawe Umenikirimu
Meniumba insani Mwanadamu alo huru
Ukanipa Qur ani Ili iwe yangu nuru
Sasa nina kheri gani Kama sijakushukuru
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Rasuli ukamtuma Ili aje nifundisha
Kila jambo lilo jema Yote kanifahamisha
Akafanya kila hima Risala kukamilisha
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Akujuwaye yakini Hawezi kuwa mjinga
Akamfata shetani Na Wewe akakutenga
Kwani vyote ardhini Asili yake mchanga
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Umetuletea maji Twanywa tukiona raha
Hujayafanya ujaji Machungu yenye karaha
Ya Rabi ewe Mpaji Tuzidishie furaha
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Na mbingu ukaziumba Kwa nyota ukazipamba
Na kisha ukaziremba Zikapangika sambamba
Kama zimefungwa kamba Hapana kinachoyumba
Nisikupende kwa nini Nawe Umenikirimu
Wallahi tukiperemba Kutizama utukufu
Tunaelewa ya kwamba Ni kazi yako Latifu
Ni kazi yako Muumba Ilo timu kamilifu
Nisikupende kwa nini Nawe Umenikirimu
Neema zako ni nyingi Ya Rabbi L arbabu
Umetupa mambo mengi Hayana hata hesabu
Ewe Mpaji kwa wingi Ewe wangu Mahabubu
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Hewa hii tuvutayo Moja ya Zako neema
Neema ambayo kwayo Kukupenda ni lazima
Lau kama hatunayo Uhai ungeyoyoma
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Vyote ulitayarisha Hata bado kutuumba
Mahitaji ya maisha Bila hata kukuomba
Ukarimu usokwisha Kutoka kwako Muumba
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Ninakupenda Wallahi Na Wewe Ndiye Shahidi
Pendo kwako likisihi Ndipo nitapofaidi
Ninakupenda Ilahi Na Mtume Muhamadi
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
M. F. S. Al Saaiy
Ndipo utapoyaenzi ukayaona adhimu
Nakupenda Mwenye enzi Ilahi Mola Karimu
Nisikupende kwa nini Nawe Umenikirimu
Nisikupende kwa nini Ya Ilahi ya Karimu
Nawe umenithamini kuniumba mwanadamu
Ukaniongeza shani Kwa dini ya Isilamu
Nisikupende kwa nini Nawe Umenikirimu
Meniumba insani Mwanadamu alo huru
Ukanipa Qur ani Ili iwe yangu nuru
Sasa nina kheri gani Kama sijakushukuru
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Rasuli ukamtuma Ili aje nifundisha
Kila jambo lilo jema Yote kanifahamisha
Akafanya kila hima Risala kukamilisha
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Akujuwaye yakini Hawezi kuwa mjinga
Akamfata shetani Na Wewe akakutenga
Kwani vyote ardhini Asili yake mchanga
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Umetuletea maji Twanywa tukiona raha
Hujayafanya ujaji Machungu yenye karaha
Ya Rabi ewe Mpaji Tuzidishie furaha
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Na mbingu ukaziumba Kwa nyota ukazipamba
Na kisha ukaziremba Zikapangika sambamba
Kama zimefungwa kamba Hapana kinachoyumba
Nisikupende kwa nini Nawe Umenikirimu
Wallahi tukiperemba Kutizama utukufu
Tunaelewa ya kwamba Ni kazi yako Latifu
Ni kazi yako Muumba Ilo timu kamilifu
Nisikupende kwa nini Nawe Umenikirimu
Neema zako ni nyingi Ya Rabbi L arbabu
Umetupa mambo mengi Hayana hata hesabu
Ewe Mpaji kwa wingi Ewe wangu Mahabubu
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Hewa hii tuvutayo Moja ya Zako neema
Neema ambayo kwayo Kukupenda ni lazima
Lau kama hatunayo Uhai ungeyoyoma
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Vyote ulitayarisha Hata bado kutuumba
Mahitaji ya maisha Bila hata kukuomba
Ukarimu usokwisha Kutoka kwako Muumba
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
Ninakupenda Wallahi Na Wewe Ndiye Shahidi
Pendo kwako likisihi Ndipo nitapofaidi
Ninakupenda Ilahi Na Mtume Muhamadi
Kwa nini nisikupende Nawe Umenikirimu
M. F. S. Al Saaiy