Nipo njia panda, nichague mke au mzazi?

navin bobby

Member
Feb 17, 2016
21
39
Wadau,

Ukoo upo kwenye vikao na maandalizi ya mwisho kabisa ya kumsafirisha baba yangu mkubwa kuja Dar kwa matibabu zaidi baada ya ugonjwa wake kushindikana katika hospital ya mkoa.

Ukoo wamepanga afikie kwangu na mimi ndie nishughulike na masuala ya Muhimbili na hiyo rufaa kwa ujumla, baba amenipigia simu kunijulisha kuhusu mgonjwa kufikia kwangu, hakutaka majadiliano, ni kama amri vile, mzee wangu ni mkoloni hakuna mfano.

Kinachotutisha ni hali ya mgonjwa ilivyo, chances za kupona ni very slim, watotoa taarifa wameniambia kwanza akifika hai Dar basi mungu mkubwa, hivyo nikamgomea mzee kuwa haiwezekani hatuna nafasi.

Mzee akasema tutaona, kwamba anajua ni mke wangu ndio kakataa, sababu anawajua wanawake, hivyo akadai atamsafirisha mgonjwa hivyo hivyo tupende tusipende, akampigia na wife simu akamfokea sana.

Wadau, tunalikataa suala hili kwa sababu wote mnajua hali ilivyo kwa sasa, posho za vikao zimefutwa, mianya yote ya deals imefungwa hapo kazini, naishi kwa mshahara tu ambao nao nilishaukopea hivyo hauji kama ulivyo, sasa kwa hali hii nije nipate msiba hapa which is more likely, maana mgonjwa sasa amevelop kwiki kwiki isiyokatika muda wote.

Gharama za kusafirisha msiba kwenda mkoa wetu kwa coaster ni karibu 4 million, na mimi sina watu kihivyo hapa mjini, haya, bado gharama za hospital, tuseme Mungu ametenda muujiza akafika akalazwa najua gharama zote za hospital wataniachia mimi, maana wanaendelea kufikiria nina hela kama zamani

Wanampigia mke wangu simu na kumtisha kuwa watamtoa kwenye hii ndoa kama mgonjwa akifa, baba kila saa ananipigia simu nitume hiyo nauli ya ndege mgonjwa asafirishwe haraka mimi nakua namchenga.Sasa jambo hili limekua kubwa katika familia na limeleta mzozo mkubwa.

Msaada wenu wa mawazo unahitajika haraka sana.
 
Kuna vitu vinatokea kama lesson katika maisha.

Suala la ugonjwa hakuna mtu anayepanga, vivyo hivyo suala la kupona.

Zamani walikuwa wanaamini kila mtoto anazaliwa na riziki yake. Yawezekana msemo huu ni kweli kwasababu hakuna anayeweza kubashiri kwamba huyu ndie president ajaye.

Point yangu ni kwamba; ongea na mzee wako nafasi uliyonayo kwa kumwelewesha kuwa, kama mgonjwa wanataka aje, basi ukoo uchange pesa hata kwa kuuza mashamba ili nauli na pesa ya matibabu ipatikane.

Suala la kufa au kutokufa sio kazi yako. Ikitokea amekufa mikononi mwako basi Mungu atakuwa ameamua kukupa somo, na nakuhakikishia hautakosa msaada au namna ya kuhandle hilo jambo. Ila kukataa kwamba asiletwe kisa huna nafasi sio busara na hakuna jamii itakuelewa.
 
Mkuu pole katika hili,waingereza husema "everything happen for a reasons" kama cjakosea... anyway point yangu ni hii;ww fanya kwa kadiri Mungu atakavyokuongoza hujui kwann unalengwa ww na sio mwingine kwenye family, usilalamike usitake kumtafuta mchawi kwa jambo kama hili,ni jaribu na utaliweza nna hakika,Mungu humpa mtu jaribu ambalo halishindwi Fanya kwa uwezo ulionao

Kingine huyo ni babako mkubwa ndio Maana yamekutoka maneno yote hayo,swali je,angekuwa baba yako mzazi ungesema hivo na ungekuja hapa kuomba ushauri juu ya nn cha kufanya!?? Fanya kwa moyo hujui Mungu anataka kukuonesha kitu gani ktk njia zako,.mtegemee yy pekee.

NB:Mwenyezi Mungu akuongoze,Amen.
 
Wadau,

Ukoo upo kwenye vikao na maandalizi ya mwisho kabisa ya kumsafirisha baba yangu mkubwa kuja Dar kwa matibabu zaidi baada ya ugonjwa wake kushindikana katika hospital ya mkoa.

Ukoo wamepanga afikie kwangu na mimi ndie nishughulike na masuala ya Muhimbili na hiyo rufaa kwa ujumla, baba amenipigia simu kunijulisha kuhusu mgonjwa kufikia kwangu, hakutaka majadiliano, ni kama amri vile, mzee wangu ni mkoloni hakuna mfano.

Kinachotutisha ni hali ya mgonjwa ilivyo, chances za kupona ni very slim, watotoa taarifa wameniambia kwanza akifika hai Dar basi mungu mkubwa, hivyo nikamgomea mzee kuwa haiwezekani hatuna nafasi.

Mzee akasema tutaona, kwamba anajua ni mke wangu ndio kakataa, sababu anawajua wanawake, hivyo akadai atamsafirisha mgonjwa hivyo hivyo tupende tusipende, akampigia na wife simu akamfokea sana.

Wadau, tunalikataa suala hili kwa sababu wote mnajua hali ilivyo kwa sasa, posho za vikao zimefutwa, mianya yote ya deals imefungwa hapo kazini, naishi kwa mshahara tu ambao nao nilishaukopea hivyo hauji kama ulivyo, sasa kwa hali hii nije nipate msiba hapa which is more likely, maana mgonjwa sasa amevelop kwiki kwiki isiyokatika muda wote.

Gharama za kusafirisha msiba kwenda mkoa wetu kwa coaster ni karibu 4 million, na mimi sina watu kihivyo hapa mjini, haya, bado gharama za hospital, tuseme Mungu ametenda muujiza akafika akalazwa najua gharama zote za hospital wataniachia mimi, maana wanaendelea kufikiria nina hela kama zamani

Wanampigia mke wangu simu na kumtisha kuwa watamtoa kwenye hii ndoa kama mgonjwa akifa, baba kila saa ananipigia simu nitume hiyo nauli ya ndege mgonjwa asafirishwe haraka mimi nakua namchenga.Sasa jambo hili limekua kubwa katika familia na limeleta mzozo mkubwa.

Msaada wenu wa mawazo unahitajika haraka sana.
Kwanza nakupa pole kwa huu mvutano. Ndugu yangu, kila jambo huwa ni la mpito. Kwanza kabisa mwache mgonjwa aje na utampa accommodation na kutoa services kwa chochote kile ulichonacho. Swala lako la kiuchumi, mi nafikiri umshirikishe Baba yako mzazi na kimweleza kila kitu ili na wao wajipange ni jinsi gani wataweza toa support. Pia mweleze mkeo ili na yeye pia ajiandae kisaikolojia wakati mgonjwa atakapo fika hapo kwako; ataoe full support pale atakapo weza kwani hili ni swala la mpito.
 
Ndo matatizo ya kulelewa na ukoo mzima, ukiwa na familia kila mwana ukoo anakuwa na sauti juu yako. Pole na fanya unachotaka kufanya, hayo ni maisha yako
 
Wadau,

Ukoo upo kwenye vikao na maandalizi ya mwisho kabisa ya kumsafirisha baba yangu mkubwa kuja Dar kwa matibabu zaidi baada ya ugonjwa wake kushindikana katika hospital ya mkoa.

Ukoo wamepanga afikie kwangu na mimi ndie nishughulike na masuala ya Muhimbili na hiyo rufaa kwa ujumla, baba amenipigia simu kunijulisha kuhusu mgonjwa kufikia kwangu, hakutaka majadiliano, ni kama amri vile, mzee wangu ni mkoloni hakuna mfano.

Kinachotutisha ni hali ya mgonjwa ilivyo, chances za kupona ni very slim, watotoa taarifa wameniambia kwanza akifika hai Dar basi mungu mkubwa, hivyo nikamgomea mzee kuwa haiwezekani hatuna nafasi.

Mzee akasema tutaona, kwamba anajua ni mke wangu ndio kakataa, sababu anawajua wanawake, hivyo akadai atamsafirisha mgonjwa hivyo hivyo tupende tusipende, akampigia na wife simu akamfokea sana.

Wadau, tunalikataa suala hili kwa sababu wote mnajua hali ilivyo kwa sasa, posho za vikao zimefutwa, mianya yote ya deals imefungwa hapo kazini, naishi kwa mshahara tu ambao nao nilishaukopea hivyo hauji kama ulivyo, sasa kwa hali hii nije nipate msiba hapa which is more likely, maana mgonjwa sasa amevelop kwiki kwiki isiyokatika muda wote.

Gharama za kusafirisha msiba kwenda mkoa wetu kwa coaster ni karibu 4 million, na mimi sina watu kihivyo hapa mjini, haya, bado gharama za hospital, tuseme Mungu ametenda muujiza akafika akalazwa najua gharama zote za hospital wataniachia mimi, maana wanaendelea kufikiria nina hela kama zamani

Wanampigia mke wangu simu na kumtisha kuwa watamtoa kwenye hii ndoa kama mgonjwa akifa, baba kila saa ananipigia simu nitume hiyo nauli ya ndege mgonjwa asafirishwe haraka mimi nakua namchenga.Sasa jambo hili limekua kubwa katika familia na limeleta mzozo mkubwa.

Msaada wenu wa mawazo unahitajika haraka sana.

Jibu mawsali haya kwanza,

Je ni kweli mkeo alikusawishi msimpokee huyo mgonjwa na ukakubaliana naye?
Kwanini uliamini taarifa za watu wa nje kuwa atakufaa kuliko wanaukoo ambao wamejitolea kuokoa maisha ya ndugu yenu?
we Ni Mungu hata kuhalalisha kifo cha Mtu?

Nawashukuru walioshauri kabla yangu, usijitengee na ukoo wako, unajuaje kama mgongjwa hatapata nafuu mikononi mwako, unaogopa akifaa kwani wewe ndiye uayeuwaa. mpokee upesi na kama ni kweli mkeo umekushauri hivyo basi hafai, tena muonye kwa ukali mkuu lakini mwenye hekima ndani yake.

swala la gharama ni swala la ukoo, waambia mapema hali yako, kuwa utajitolea muda wa kuzunguka ghara mchangiane, kula atakula mnacho kula na kunywa pia, kama unahitaji usaidizi wa kuuguza omba mwanaukoo moja au wawili wambatane naye kadiri utakavyo ona inafaa.
Muombe nsamaha baba yako na endelea mbele na maisha muulize kama aliwambia wanaukoo, juu ya katazo lako na waombe msamaha pia.

Kumbu wema ni tunda la Mungu na linadhawabu yake. mpokee upesi huwezi jua anaweza kuishi kwa sababu ya familia yako.
 
Wadau,

Ukoo upo kwenye vikao na maandalizi ya mwisho kabisa ya kumsafirisha baba yangu mkubwa kuja Dar kwa matibabu zaidi baada ya ugonjwa wake kushindikana katika hospital ya mkoa.

Ukoo wamepanga afikie kwangu na mimi ndie nishughulike na masuala ya Muhimbili na hiyo rufaa kwa ujumla, baba amenipigia simu kunijulisha kuhusu mgonjwa kufikia kwangu, hakutaka majadiliano, ni kama amri vile, mzee wangu ni mkoloni hakuna mfano.

Kinachotutisha ni hali ya mgonjwa ilivyo, chances za kupona ni very slim, watotoa taarifa wameniambia kwanza akifika hai Dar basi mungu mkubwa, hivyo nikamgomea mzee kuwa haiwezekani hatuna nafasi.

Mzee akasema tutaona, kwamba anajua ni mke wangu ndio kakataa, sababu anawajua wanawake, hivyo akadai atamsafirisha mgonjwa hivyo hivyo tupende tusipende, akampigia na wife simu akamfokea sana.

Wadau, tunalikataa suala hili kwa sababu wote mnajua hali ilivyo kwa sasa, posho za vikao zimefutwa, mianya yote ya deals imefungwa hapo kazini, naishi kwa mshahara tu ambao nao nilishaukopea hivyo hauji kama ulivyo, sasa kwa hali hii nije nipate msiba hapa which is more likely, maana mgonjwa sasa amevelop kwiki kwiki isiyokatika muda wote.

Gharama za kusafirisha msiba kwenda mkoa wetu kwa coaster ni karibu 4 million, na mimi sina watu kihivyo hapa mjini, haya, bado gharama za hospital, tuseme Mungu ametenda muujiza akafika akalazwa najua gharama zote za hospital wataniachia mimi, maana wanaendelea kufikiria nina hela kama zamani

Wanampigia mke wangu simu na kumtisha kuwa watamtoa kwenye hii ndoa kama mgonjwa akifa, baba kila saa ananipigia simu nitume hiyo nauli ya ndege mgonjwa asafirishwe haraka mimi nakua namchenga.Sasa jambo hili limekua kubwa katika familia na limeleta mzozo mkubwa.

Msaada wenu wa mawazo unahitajika haraka sana.
@Gojaganize kamaliza
 
Ni ngumu kiasi gani kuwaambia ukweli kuhusu hali yako ya kifedha??
 
Ni jinsi vile ulivyojiweka kabla ya kufilisika... Hiyo jeuri yote kutoka kwa wazazi ni kwa sababu kipindi ulivyokuwa nazo ulikuwa unakumbatia kila kitu, sasa huna wanahisi hutaki makusudi...
 
Back
Top Bottom