Nipeni ushauri nifanyeje juu ya hili?

Nipeni ushauri nifanyeje juu ya hili?

Daniel Adrian

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2019
Posts
311
Reaction score
335
Kwa ambao ntawaudhi kwa hili ntakalolisema mtanisamehe lakini nahisi hapa JF naweza pata ushauri au msaada wa nini cha kufanya kwa hii hali yangu.

Mimi ni kijana, umri wagu ni miaka 28 nimetimiza tu mwezi wa tisa mwaka huu. Naishi gongo la mboto, Dar es salaam. Changamoto yangu kubwa ni unene. Unene huu unanipa muonekano wa kibaba, yaani naonekana kama 'mbaba' hivi. Kuhusu mazoezi ya kukimbia nimefanya sana lakini unene haunitoki, hata mpira nacheza sana katika timu yetu ya mtaani lakini hainisaidii kupunguza unene angalau na mimi niondoe ule mwonekano wa 'kibaba'.

Muonekano huu unanipa changamoto sana kwani mpaka sasa sina mahusiano ya kueleweka. Wanawake (wa umri wangu) karibia wote wananikataa wanahisi mimi sio umri wao, wengine wananiamkia. Yaani mwanamke nikishamwita tu anaanza kuniamkia. Mwingine anaweza akaja akaniambia ukweli kabisa kuwa "mimi sio umri wako".

Hapa nimeshadangwa sana, mpaka nafikia hatua naogopa KABISA wanawake. Wakiniona tu wananiona 'danga material' yaani baba fualni hivi (mwenye mke na watoto) anapenda watoto wadogo. Ikitokea mwanamke akanipa namba basi kinachofuata ni mizinga MIZITO akihisi kalipata danga la kumhudumia. Rafiki zangu wawili wamepata wanawake na wameshaoa lakini changamoto ipo kwangu kutokana na huu muonekano wangu. Nifanye nini mimi nisionekana 'mbaba', mazoezi ya kukimbia nayafanya kila siku asubuhi na jioni lakini nipo vile vile nakula kidogo sana na sometimes hata usiku nalala bila kula ili nipungue lakini wapi.

Nimeajiriwa, hapa ninapofanyia kazi vijana wenzangu hata hawapendi kushirikiana na mimi, wanahisi sio mwenzio, wanaweza kuamua kukutana kula bata jumamosi lakini mimi hawatoniambia wanaona kama huyu mbaba akija hapa "atatunyima uhuru". Naweza sema labda wananiheshimu maana hata nikiwepo hawaongei stori zao za kiujana lakini kuniweka mbali nao inanipa maswali sana.

Nipeni ushauri jamani nifanyeje ? Maana hapa nilipo kwenye ujana sipo na kwenye uzee sipo.
 
Aiseee pole mkuu! Ila utakua na unene wa asili hivyo option labda uwe unakula milo miwili au mmoja tena ya vyakula chukuchuku tu.
 
Tafuta hela sasa 😅

Enewei jiamini tu mwaya , jikubali kwanza ndo wengine watakukubali
 
Tafuta hela sasa 😅

Enewei jiamini tu mwaya , jikubali kwanza ndo wengine watakukubali
Asante kwa ushauri lakini mimi sina tatizo la kujiamini. Na suala la kujiamini halihusiani na kesi yangu. Asnate lakini!
 
Aiseee pole mkuu! ila utakua na unene wa asili hivyo option labda uwe unakula milo miwili au mmoja tena ya vyakula chukuchuku tu.
Asante kwa ushauri kaka. Ntajaribu kufuata ratiba ya mlo mmoja!
 
Tafuta ela mzee baba , madem wote watakuona kijana mwenzao
 
Nenda Kwa wataalam wa lishe Yani kila mlo upangiwe kulingana na calories zilizopo kwenye chakula, kula kidogo sio kula healthy unaweza kula kidogo kumbe unakula calories nyingi na utakua hufanyi kitu pia jitahidi kutembea angalau nusu saa kwa siku
 
Kwa ambao ntawaudhi kwa hili ntakalolisema mtanisamehe lakini nahisi hapa JF naweza pata ushauri au msaada wa nini cha kufanya kwa hii hali yangu.

Mimi ni kijana, umri wagu ni miaka 28 nimetimiza tu mwezi wa tisa mwaka huu. Naishi gongo la mboto, Dar es salaam. Changamoto yangu kubwa ni unene. Unene huu unanipa muonekano wa kibaba, yaani naonekana kama 'mbaba' hivi. Kuhusu mazoezi ya kukimbia nimefanya sana lakini unene haunitoki, hata mpira nacheza sana katika timu yetu ya mtaani lakini hainisaidii kupunguza unene angalau na mimi niondoe ule mwonekano wa 'kibaba'.

Muonekano huu unanipa changamoto sana kwani mpaka sasa sina mahusiano ya kueleweka. Wanawake (wa umri wangu) karibia wote wananikataa wanahisi mimi sio umri wao, wengine wananiamkia. Yaani mwanamke nikishamwita tu anaanza kuniamkia. Mwingine anaweza akaja akaniambia ukweli kabisa kuwa "mimi sio umri wako".

Hapa nimeshadangwa sana, mpaka nafikia hatua naogopa KABISA wanawake. Wakiniona tu wananiona 'danga material' yaani baba fualni hivi (mwenye mke na watoto) anapenda watoto wadogo. Ikitokea mwanamke akanipa namba basi kinachofuata ni mizinga MIZITO akihisi kalipata danga la kumhudumia. Rafiki zangu wawili wamepata wanawake na wameshaoa lakini changamoto ipo kwangu kutokana na huu muonekano wangu. Nifanye nini mimi nisionekana 'mbaba', mazoezi ya kukimbia nayafanya kila siku asubuhi na jioni lakini nipo vile vile nakula kidogo sana na sometimes hata usiku nalala bila kula ili nipungue lakini wapi.

Nimeajiriwa, hapa ninapofanyia kazi vijana wenzangu hata hawapendi kushirikiana na mimi, wanahisi sio mwenzio, wanaweza kuamua kukutana kula bata jumamosi lakini mimi hawatoniambia wanaona kama huyu mbaba akija hapa "atatunyima uhuru". Naweza sema labda wananiheshimu maana hata nikiwepo hawaongei stori zao za kiujana lakini kuniweka mbali nao inanipa maswali sana.

Nipeni ushauri jamani nifanyeje ? Maana hapa nilipo kwenye ujana sipo na kwenye uzee sipo.
Nakushauri kunywa juice ya ndimu au limao weka kwenye chupa ya lita moja na nusu uwe unakunywa asubuhi na endelea kucheza mpira na punguza kula vyakula vya wanga ususani chips, pendelea kula matunda usiku, Mimi nimekuzid miaka mingi kidogo lakini muonekano wangu ni kama kijana wa miaka 25, na ninaweza kutogoza msichana wa kuanzia miaka 17 na nisipate changamoto yoyote kwasababu muonekano wangu siyo wa kibaba, mwili wangu ni mwembamba siyo bonge.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Nipeni ushauri jamani nifanyeje ? Maana hapa nilipo kwenye ujana sipo na kwenye uzee sipo

Mtafute BAGHDAD atakuelekeza DAWA YA KUONDOA MAFUTA MWILINI, KUTOKA 150KG MPAKA 80 KG

Screenshot_20221108-210251.png
 
Usijali yupo atakaekupenda jinsi ulivyo...cha msingi ni kujikubali na kupungua iwe ni matokeo ya muda mrf na isiwe kama ni jambo la haraka sana.. kitu chochote ukikifanya kwa stress and tension kubwa hakina matokeo bora. So just relaax na ishi maisha yako
 
Back
Top Bottom