Daniel Adrian
JF-Expert Member
- Jan 1, 2019
- 311
- 335
Kwa ambao ntawaudhi kwa hili ntakalolisema mtanisamehe lakini nahisi hapa JF naweza pata ushauri au msaada wa nini cha kufanya kwa hii hali yangu.
Mimi ni kijana, umri wagu ni miaka 28 nimetimiza tu mwezi wa tisa mwaka huu. Naishi gongo la mboto, Dar es salaam. Changamoto yangu kubwa ni unene. Unene huu unanipa muonekano wa kibaba, yaani naonekana kama 'mbaba' hivi. Kuhusu mazoezi ya kukimbia nimefanya sana lakini unene haunitoki, hata mpira nacheza sana katika timu yetu ya mtaani lakini hainisaidii kupunguza unene angalau na mimi niondoe ule mwonekano wa 'kibaba'.
Muonekano huu unanipa changamoto sana kwani mpaka sasa sina mahusiano ya kueleweka. Wanawake (wa umri wangu) karibia wote wananikataa wanahisi mimi sio umri wao, wengine wananiamkia. Yaani mwanamke nikishamwita tu anaanza kuniamkia. Mwingine anaweza akaja akaniambia ukweli kabisa kuwa "mimi sio umri wako".
Hapa nimeshadangwa sana, mpaka nafikia hatua naogopa KABISA wanawake. Wakiniona tu wananiona 'danga material' yaani baba fualni hivi (mwenye mke na watoto) anapenda watoto wadogo. Ikitokea mwanamke akanipa namba basi kinachofuata ni mizinga MIZITO akihisi kalipata danga la kumhudumia. Rafiki zangu wawili wamepata wanawake na wameshaoa lakini changamoto ipo kwangu kutokana na huu muonekano wangu. Nifanye nini mimi nisionekana 'mbaba', mazoezi ya kukimbia nayafanya kila siku asubuhi na jioni lakini nipo vile vile nakula kidogo sana na sometimes hata usiku nalala bila kula ili nipungue lakini wapi.
Nimeajiriwa, hapa ninapofanyia kazi vijana wenzangu hata hawapendi kushirikiana na mimi, wanahisi sio mwenzio, wanaweza kuamua kukutana kula bata jumamosi lakini mimi hawatoniambia wanaona kama huyu mbaba akija hapa "atatunyima uhuru". Naweza sema labda wananiheshimu maana hata nikiwepo hawaongei stori zao za kiujana lakini kuniweka mbali nao inanipa maswali sana.
Nipeni ushauri jamani nifanyeje ? Maana hapa nilipo kwenye ujana sipo na kwenye uzee sipo.
Mimi ni kijana, umri wagu ni miaka 28 nimetimiza tu mwezi wa tisa mwaka huu. Naishi gongo la mboto, Dar es salaam. Changamoto yangu kubwa ni unene. Unene huu unanipa muonekano wa kibaba, yaani naonekana kama 'mbaba' hivi. Kuhusu mazoezi ya kukimbia nimefanya sana lakini unene haunitoki, hata mpira nacheza sana katika timu yetu ya mtaani lakini hainisaidii kupunguza unene angalau na mimi niondoe ule mwonekano wa 'kibaba'.
Muonekano huu unanipa changamoto sana kwani mpaka sasa sina mahusiano ya kueleweka. Wanawake (wa umri wangu) karibia wote wananikataa wanahisi mimi sio umri wao, wengine wananiamkia. Yaani mwanamke nikishamwita tu anaanza kuniamkia. Mwingine anaweza akaja akaniambia ukweli kabisa kuwa "mimi sio umri wako".
Hapa nimeshadangwa sana, mpaka nafikia hatua naogopa KABISA wanawake. Wakiniona tu wananiona 'danga material' yaani baba fualni hivi (mwenye mke na watoto) anapenda watoto wadogo. Ikitokea mwanamke akanipa namba basi kinachofuata ni mizinga MIZITO akihisi kalipata danga la kumhudumia. Rafiki zangu wawili wamepata wanawake na wameshaoa lakini changamoto ipo kwangu kutokana na huu muonekano wangu. Nifanye nini mimi nisionekana 'mbaba', mazoezi ya kukimbia nayafanya kila siku asubuhi na jioni lakini nipo vile vile nakula kidogo sana na sometimes hata usiku nalala bila kula ili nipungue lakini wapi.
Nimeajiriwa, hapa ninapofanyia kazi vijana wenzangu hata hawapendi kushirikiana na mimi, wanahisi sio mwenzio, wanaweza kuamua kukutana kula bata jumamosi lakini mimi hawatoniambia wanaona kama huyu mbaba akija hapa "atatunyima uhuru". Naweza sema labda wananiheshimu maana hata nikiwepo hawaongei stori zao za kiujana lakini kuniweka mbali nao inanipa maswali sana.
Nipeni ushauri jamani nifanyeje ? Maana hapa nilipo kwenye ujana sipo na kwenye uzee sipo.