Nipe ramani ya wilaya za Kigamboni na Ubungo

N'yadikwa

JF-Expert Member
Aug 10, 2014
6,825
9,528
Nimekaa hapa nikawa natafuta details za hizo wilaya mpya mbili za Dar, hebu niambie/nichoree ramani ya hizo wilaya mbili mpya.Na je wilaya za zamani zinaishia wapi. Na wapi yaliko makao makuu ya wilaya hizo mpya mbili.

Karibu unisaidie kufahamu.
 
Wataangalia kata zilizo ndan ya wilaya hizo zinajulikana na kila mtendaji wa kata na madiwan wanajua mipaka yao hivyo kama madiwan wa kigambon wote wakikaa katika kata zao wata-shape hilo jimbo na raman itajulikana na the same apply kwa wilaya ya ubungo
 
Kwani mkuu unazihitaji za ninj, au wewe ni mwalimu wa tuition, u ataka wapa wanafunzi nondo. Hahaahaahah,
Ukipata na mm utanipasia kiasi.
Nimekaa hapa nikawa natafuta details za hizo wilaya Mpya mbili za Dar, hebu niambie/nichoree ramani ya hizo wilaya mbili mpya.
Na je wilaya za zamani zinaishia wapi. Na wapi yaliko makao makuu ya wilaya hizo mpya mbili. Karibu unisaidie kufahamu.
 
Kiswahili kigumu au mazoea, kule Kenya wanasema nipe ila Tanzania tunasema naomba au nisaidie. Usimlaumu inategemeana na makuzi, yeye alimaanisha naomba.

Nipe maneno haya chini kwa lugha ya wenzetu kwa mfano waingereza

Nipe ni ....
Nisaidie ni ....
Naomba ni ....
Tafadhali ....

Nitapenda kujifunza nami nielewe hiki kiswahili nacho kinaboa wakati mwingine kutumia.
 
Asante kwa kila aliechangia majibu kamili nishayapata japo sio ktk uzi huu.
 
Nipe ... Give me
Nisaidie ... Help me
Naomba... I beg you
Tafadhali ... Please
Nipe maneno haya chini kwa lugha ya wenzetu kwa mfano waingereza

Nipe ni ....
Nisaidie ni ....
Naomba ni ....
Tafadhali ....

Nitapenda kujifunza nami nielewe hiki kiswahili nacho kinaboa wakati mwingine kutumia.
 
So hiyo ya juu ni big NO kutumika kihivihivi ni kama mtu hana heshima.. kwangu mimi nionavyo.
Waswahili hupenda sana kutumia uungwana wakati wakitaka kitu. Uko sahihi ila lakini umri ndio hutumika kutofautisha ridhaa ya kupatiwa kitu. Kwa mfano naomba maji ya kunywa hutumika kwa watu wazima; na nipe maji ya kunywa hii ni kama amri na hutumika kwa watoto wanapoombwa maji ya kunywa. Hilo neno mtu asiye na heshima naogopa kulitumia kwa kuwa lina utata katika matumizi. Mtu asiye na heshima huchukuliwa mtu asiyethamini wenzake.
 
Waswahili hupenda sana kutumia uungwana wakati wakitaka kitu. Uko sahihi ila lakini umri ndio hutumika kutofautisha ridhaa ya kupatiwa kitu. Kwa mfano naomba maji ya kunywa hutumika kwa watu wazima; na nipe maji ya kunywa hii ni kama amri na hutumika kwa watoto wanapoombwa maji ya kunywa. Hilo neno mtu asiye na heshima naogopa kulitumia kwa kuwa lina utata katika matumizi. Mtu asiye na heshima huchukuliwa mtu asiyethamini wenzake.

Nimekupata, ndio maana mie nililelewa nafundishwa hilo neno na wazazi kwa wao kulitamka kwa watoto wao pia. So likanikaa, hata kusema shukurani hadi kwa vitu mtu huwezi fikiria katiks maisha tulisukumwa tuseme kwao kama kupanda gari wameendesha na kushuka lazima tunawashukuru n.k.

Ila watoto wadogo ni majukumu ya wazazi/ walezi kuwafunza, bila hivyo sijui nani tena atafanya.

Kama mimi nisipolisema nakuwa najijua nafanya makusudi kama nilitakiwa haswaaa kutilitamka au kuomba vizuri.

Ndugu naona upo vizuri pia kushikilia misimamo yako.
 
Nimekupata, ndio maana mie nililelewa nafundishwa hilo neno na wazazi kwa wao kulitamka kwa watoto wao pia. So likanikaa, hata kusema shukurani hadi kwa vitu mtu huwezi fikiria katiks maisha tulisukumwa tuseme kwao kama kupanda gari wameendesha na kushuka lazima tunawashukuru n.k.

Ila watoto wadogo ni majukumu ya wazazi/ walezi kuwafunza, bila hivyo sijui nani tena atafanya.

Kama mimi nisipolisema nakuwa najijua nafanya makusudi kama nilitakiwa haswaaa kutilitamka au kuomba vizuri.

Ndugu naona upo vizuri pia kushikilia misimamo yako.
Aksante kwa kunielewa.
 
Back
Top Bottom