Heshima zenu wapendwa!
Hili nalo linanichanganya mwenzenu sijui kama mwenye kuweza kunisaidia.
Kwa mtazamo wangu mimi nadhani wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni wengi kuliko kazi wanayofanya. Wanasema 'two heads are better than one' lakini kusema kweli bunge letu halina tija na ni mzigo mkubwa sana kwa nchi.
Jambo linalonikera zaidi ni pale baadhi ya watu wanapoitetea serikali kana kwamba hawaoni uozo uliopo. Napata shida sana kuamini kama ni watanzania au ni mawazo mgando ndiyo unaowasumbua.
Jamani tushirikiane kuikomboa nchi yetu. Sioni sababu ya kuwa na wabunge wengi wanaokwenda kulala bungeni au hata kutetea uchafu unaofanywa na viongozi wetu.
Sitaki kuamini kwamba nchi hii haina tena watu wenye hekima kwamba wote ni mbumbu. Sipendi kuamini pia kwamba hakuna hata mtu mmoja mwenye uchungu na nchi hii ambayo wananchi wake walio wengi wanaishi katika umaskini japo kuna rasilimali nyingi zinazowanufaisha wachache.
Nawakilisha kwa mjadala, idadi ya wabunge katika bunge la JMT inaendana na utendaji wake?
Hili nalo linanichanganya mwenzenu sijui kama mwenye kuweza kunisaidia.
Kwa mtazamo wangu mimi nadhani wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni wengi kuliko kazi wanayofanya. Wanasema 'two heads are better than one' lakini kusema kweli bunge letu halina tija na ni mzigo mkubwa sana kwa nchi.
Jambo linalonikera zaidi ni pale baadhi ya watu wanapoitetea serikali kana kwamba hawaoni uozo uliopo. Napata shida sana kuamini kama ni watanzania au ni mawazo mgando ndiyo unaowasumbua.
Jamani tushirikiane kuikomboa nchi yetu. Sioni sababu ya kuwa na wabunge wengi wanaokwenda kulala bungeni au hata kutetea uchafu unaofanywa na viongozi wetu.
Sitaki kuamini kwamba nchi hii haina tena watu wenye hekima kwamba wote ni mbumbu. Sipendi kuamini pia kwamba hakuna hata mtu mmoja mwenye uchungu na nchi hii ambayo wananchi wake walio wengi wanaishi katika umaskini japo kuna rasilimali nyingi zinazowanufaisha wachache.
Nawakilisha kwa mjadala, idadi ya wabunge katika bunge la JMT inaendana na utendaji wake?