Ninunue lori ya kichina 0 KM au Scania used from Saab Scania

Mleta mada Leo umenifurahisha Sana kwa Uzi huu
Kwanza umenikumbusha mbali mno
Niliishi kwenye fleet na kuipenda hyo Kaz Sana

Ili fika mahali milio ya Malory ya kuchina na ya kizungu ubongo ukazoe hata nikiwa mbali nikisikia lorry linanguruma nitajuw. Tu Ni howo au scania r420 -480

Safi Sana ukinunua tafdhali tupe mrejesho

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Km mzunguko wa biashara ni mzuri chukua mchina kwanza for at least 2yrs then anza kuchanganya na scania ilimchina akianza choka scania anakubeba mzigo unakua na kitu kinaitwa business continuity
Bonge moja la comment.. shukrani sana mdau
 
Kachumbari ya magari haitakiwi hasa kwa mazingira yetu ya bongo ambapo kupata spare part original au best aftermarket ni mtihani,
Lakini tatizo kubwa kwa wasafirishaji wa Tanzania ni kuwa hawajui jinsi ya kuspecify gari kutokana na kazi walizo nazo mkononi, Naona mtoa mada pia anastruggle na tatizo hilo, kazi aliyonayo mkononi ni Congo migodini, kule kunahitaji gari heavy duty, yenye retarder , sio lazima iwe double diff , a tag unit with high range hub reduction diff ipo vizuri na ni nyepesi kuliko double diff .p 360 kama unaipeleka kolwezi basi angalau iwe ya south Africa , sio Uk.
Tatizo pia lipo kwa wanaouza hayo magari , hapa naongelea saab scania, wao gari mpya zao zipo well speced kwa mazingira yetu, ila mitumba wanaleta pusher trucks (mid lift), pusher trucks by default ni gari za kazi laini laini, ukishaanza kuipeleka kolwezi R450 pusher , unachezea pesa yako tu maana gharama lazima ziwe juu, kuanzia brake maintanace hadi drive train.
Kwa hiyo kiongozi katika hili naomba ushauri wa best truck na best trailer..
 
Habari natumaini wakongwe mko vizuri


Nina mpango wa kuanzisha kampuni ya usafirishaji nikiwa na mpango wa kusafirisha mizigo kutoka nchini kwenda nchi jirani kwa maana DRC, Zambia, Burundi, Rwanda n.k
(Transit)

Katika kuuliza uliza nimekutana na mawazo makuu mawili ambayo yamekuwa yakinipa mawazo nikaona ni vyema niilete kwenu kwa majadiliano wakongwe

WAZO LA KWANZA

Wazo la kwanza ni kuchukua lori 0 Km kutoka kwa wachina aidha Howo au Faw

WAZO LA PILI

Wazo la pili ni kichukua scania used kutoka saab scania ambapo pale naweza kupata P360 iliyosimama

Trip ni kusafirisha makontena kuelekea maeneo kama vile Congo Kolwezi, Likasi, Lubumbash, Kasumbalesa, Lusaka, Rwanda, Burudi na Malawi

Hivyo basi nataka kujua gari sahihi ambalo wakongwe mtanishauri ninunue kutokana na aina ya safari zangu hizo

Tayari Agent yupo ambaye uhakika wa kutupa tenda za kusafirisha ni uhakika

Kwa kuanza tuna mpango wa kuanza na magari sita (06) lakini upo uwezekano wa kununua mpaka kumi na mbili (12)

UTAFITI WANGU WA AWALI

Gharama za mchina na Scania hazitofautiani sana mathalan kwa mfano ukienda kwa Dr Howo pale kurasini gari N7 na tella lake ambazo ni 0 Km ni $81,000 wakati saab scania used p 360 ni Tsh 150M , ukichukua na tella la superdol na bima na kila kitu ni kama 250M ambayo ni $106,000

MANUNUZI

Mchina:Truck and trailer (both brand new) $81,000
Scania : Used and trailer (brand new) $106,000

MAFUTA

Kwa upande wa mafuta wachina kwenye mafuta wako vizuri kwa maana trip ambayo scania atatumia lita 1900 mchina anaweza kutumia lita 1700 hiyo lita 200 unakuwa umeokoa ambayo ni takribani laki sita (600,000)

Kwa maana mchina gharama za ununuzi ziko chini, uendeshaji ziko chini ila hazidumu sana kwa maana baada ya miaka yako mitano gari kwisha kazi

Ila scania gharama za ununuzi ziko juu, uendeshaji, iko juu ila zinadumu hadi miaka saba hadi nane..

Naileta hii mada kwenu kwamba je niingie kwa mchina au niingie kwa msweeden?

WHY SAAB SCANIA NA SIO KUAGIZA SCANIA KUTOKA UINGEREZA


Watu wamenishauri kuagiza scania gharama haitofautiani iwapo ukaenda kununua saab scania lakini haina guarantee unaweza agiza gari kutoka UK used limetembea km 400,000 ukaanza safari kufika chalinze tu ngoma imesizi, hapo uneshapokea mzigo wa mtu ni lazima ufanye engine overhaul na mambo mengine mengi

Hapo unakuta unapoteza mpaka 9 M kwa engine na fundi etc

Lakini pia kwa upande wa kichina ni kwamba madereva wazuri wanazikimbia sababu ya aina ya magari kiafya sio rafiki kwao hivyo ukiwa na scania kama p360 ni rahisi kupata madereva wazuri kwani talent pool ya madereva wanaotaka kuendesha hizo p360 ni kubwa pia

Hivyo basi naomba kuuliza kwa gari 6 mpaka 12, agent tayari kashakuwa spotted anaweza kutupa kazi trip ni za kwenda Congo Kolwezi, Likasi, Lubumbash, Kasumbalesa, Lusaka, Rwanda, Burudi na Malawi je nishukue mchina au niingie kwa m sweeden naomba kujua sana sana technical know hows za hizi chuma mbili

Maana kuna watu wanashauri kuwa ni bora mchina na wengine wanashauri ni bora m sweeden used

Tayari eneo ambalo nitalifanya kama yard nimesha li spot ambapo ni Kibaha kwa mathias itakapokuwa makao makuu na main yard ya chuma kwa maana agent akikamilisha kila kitu chuma zinaamsha toka kibaha kwenda bandarini kupakia kisha kuamsha...

Natanguliza shukrani

C.T.UView attachment 2566531View attachment 2566532
Nimefurahi kusikia kuhusu mpango wako wa kuanzisha kampuni ya usafirishaji wa mizigo kwenda nchi jirani kama DRC, Zambia, Burundi, Rwanda, na kadhalika. Kwa upande wa gari, nashauri kuwa ununue Scania badala ya Howo au Faw, kwa sababu kwa mujibu wa utafiti wako wa awali, Scania inadumu kwa miaka saba hadi nane wakati Howo inadumu kwa miaka mitano tu. Ingawa gharama ya ununuzi wa Scania ni kubwa, inaweza kuokoa gharama ya mafuta, ambayo ni karibu Tsh 600,000 ($200), kutokana na ufanisi wake wa matumizi ya mafuta.

Kwa kuwa umeshaelezea kuwa una mpango wa kuanza na magari sita hadi kumi na mbili, ni vizuri kuchagua gari ambalo linaweza kudumu kwa muda mrefu na kuwa na dereva mzuri. Kwa upande wa yard yako, kuna mambo kadhaa ya kuzingatia, kama vile nafasi ya kutosha, upatikanaji wa huduma za ujenzi, na kadhalika. Kwa ujumla, nashauri uwe makini na uzingatie gharama na ufanisi wa gari, na uangalie pia upatikanaji wa huduma za matengenezo na vipuri kwa gari unalotaka kununua. Mafanikio mema katika biashara yako ya usafirishaji!
 
Chukuwa scania mkuu utaleta mrejesho hapa parts zake zipo rundo na zina mafundi wazoefu sana, pia nakupa ujanja mara ununuapo gari za kichina badili sit ya dereva ndiyo inayoumiza kwa kweli.
Wanasema hizi howo N7 siti zimeboreshwa ila ngoja nitafuatilia zaodi
 
Mkuu ushauri wangu kwa structure ya kazi zako na huko unakokwenda , nakushauri gari ya kichina,
Sipendi gari ya kichina na kupata madereva ni ngumu sana kwa sasa , kwa sababu as they become popular nowadays watu wanafahamu mengi kuhusu hizo gari , kiukweli sio rafiki wa afya kwa dereva , na zinachosha sana, yes zinatumia.mafuta vizuri lakini zikiwa mpya tu, zikichoka zipo vibaya ,
Kwa nini sikushauri scania japo naipenda sana , !!, sababu nimeona unafocus kwenye mtumba wa Uk, kama unaweza nenda botswana ,namibia au south africa huko utapata scania za kwenda nazo kolwezi.
R450 mtumba wa uk inakuja na diff yenye ration 2.92, hii ni diff ya mbio sio kupanda milima , R460 ya south ni euro 3 na inakuja na diff yenye ratio 3.08.hii ni diff ya milima sio.mbio, ndio maana ukiilazimisha r450 ya mtumbaipande milima kwa uwezo wa engine lazima utaoverhaul engine mapema
Shukrani sana Mkuu kwa hiyo ni focus sana sana na euro 3 si ndio eeeh
 
Kwa sababu wewe ni mgeni wa biashara.

Kaa kwenye zero km.

Fuel Consumption itakubeba.

Spare parts nazo haitakugharimu sana

Mengine utajifunzia ukiwa field
Shukrani sana kamanda
 
Kwa hiyo kiongozi katika hili naomba ushauri wa best truck na best trailer..
Best trailer tafuta double tires on air suspension , preferably with bendix or wabco Abs system
Best truck kwa nature ya huko unakotaka kwenda tafuta gari ya kichina ambazo kwa kawaida ni 6x4, kama mfuko unaruhusu zama south kachukue R460 duoble diff mtumba wa south au namibia , hii unaweza kuja nishukuru baadaye , ni very best option kwa kazi na barabara zetu.
Kwa kazi zako kama ulivyoelezea mwanzo , kaa mbali sana na gari za mtumba wa uingereza , hasa euro 5 na 6.
 
Shukrani sana Mkuu kwa hiyo ni focus sana sana na euro 3 si ndio eeeh
Tafuta Euro 3 ! Kwa kuwa mafuta tunayotumia bado yana sulpbur content kubwa , Trucks za euro 5 na6 zinatumia ultra low sulphur diesel, huku hatuna hiyo , ndio sababu cha kwanza huwa zinazingua sensors ni nyingi na ukishawekandiesel yetu matatizo yanaanza , wich is the reason why hata ukiwa na pwaa yako scania Tanzania hawezi kukuagizia gari mpya yoyote ya euro 6, maana anajua hataweza kukupa warranty na litakusumbua .
kuna option kama mbili tatu,
1 ,brand new kutoka vingunguti
2 mtumba kutoka scandinavians, huko hawa kurush kwenye emmission control.kama Uk.
3 .mtumba kutoka south africa , namibia ,botswana au brazil .
 
Najaribu kuchambua comment.

Kuna maswala ya msingi sana technically kuna swala la diff ratio kwenye scania... nimeona zipo R450 ya UK ina diff ya 2.92 ambayo mdau kasema inaweza mbio na si heavy duty haipandi milima mikali HAIFAI. Ushauri wake kwa kuzingatia target ya route zako ni R460 ya S.A yenye diff ratio ya 3.08 inanguvu ya kupanda milima ila haina mbio na hii ndio itafaa uendako.

Kwa mchina Howo nimeona Imekuwa recommended kutokana na uhimilivu wake na configaration ya 6 by 4 yaani ni double diff pia fuel consumption iko vizuri [hapa navyo kumbuka huwa ku formula ya fuel consumption Hii inatofautiana gari na gari (Total Km (one way) x 0.3 empty plus Total Km (one way) x 0.5 loaded)x fuel price... kujua gharama za mafuta. HOWO inachangamoto za cabin suspension system na inner body design haitoi starehe kwa dereva wa long route. Pia life span yake ni 5years haina engine rebuild kit (overhaul) pia haiuziki kirahisi ikiwa used.

HOWO straingth ni 0 km, low maintanance cost, low fuel consumption, low buying price, cheap spare, easy spare availability and technicians (mafundi wapo)

Why Scania and not Scania...
Used Most is above 400,000km, high buying price, kodi kubwa, inategea hali ya hewa ya nchi ilikokusudiwa, inachagua barabara, spare ni aghali, fuel consumption is high ukilinganisha na HOWO, haina uhakika wa uzima wake baada ya kuinunua, ukiilazisha ni rahisi kuharibika, service ni aghali, wauzaji wake hawaaminiki kwenye taarifa za gari...kuna kupigwa!

Straingth ni imara ukibahatisha, inadumu muda mrefu, suspension system yake is superb very confortable , madereva wanaipenda, ukipata ya S.A R460 Euro3 yenye diff ratio ya 3.08 unauhakika wa kupasua milima

Matatizo ya kibiashara na uendeshaji, kuna utapeli kwa madalali, wizi wa mizigo hasa Congo, ubovu wa barabara Congo, kodi za gari, upandaji wa bei ya mafuta na vipuri, uaminifu kwa madereva na ujuzi wao wa kazi, ajali, changamoto za urejeshaji wa mkopo (ikiwa ulikopa) uharaka na uhakika wa upatikanaji wa mizigo.

Faida na hasara
Ni biashara yenye 50% risk
Ukipata mizigo kwa bei nzuri bila changamoto inalipa haraka sana. Na hasara ni haraka mfano kuungua kwa gari na mzigo, ajari kubwa, bima na nk

Hitimisho; chambua maoni fanya maamuzi.
 
KUlima ni Rukwa mzee, Ruvuma kanunue vitalu vya makaa ya mawe ndo habari ya mjini.
cheza bingo hiyo ukibutua ni mpunga wa kula hadi unaiaga dunia .ukifeli unalima mahindi.
Nipe ABC mzee..ni kule Kitai?
 
Back
Top Bottom