Nini ushauri wako kwa anayetaka kuacha kazi ili amtumikie Mungu?

Genio the great

Senior Member
Aug 29, 2022
159
491
Habari Wana jamvi, naiheshimu sana JamiiForums kwani ni forum ambayo imekuwa ikifanya kazi kubwa ya kuielimisha jamii katika nyanja mbalimbali.

Na hii ni kwasababu imejawa na watu wengi wenye ufahamu mkubwa juu ya mambo mbalimbali na experience tofauti. Leo nmesukumwa tushirikishane juu ya mada niliyoweka hapo juu.

Viongozi wengi wa dini pamoja na watumishi wengi kwenye shuhuda zao mbalimbali hasa upande wa dini ya kikristo ambayo ninaufahamu nayo Kwa asilimia nyingi kidgo nikilinganisha na dini nyingine.

Huwa wanaongea kwamba waliacha hiki(kazi) wakaamua kufanya hiki(kutumikia Mungu ) Kwa kumaanisha yaani sio Kwa kudonoa donoa.

Nilishawahi kumsikia Mtumishi wa Mungu mwl Christopher Mwakasege akisema zamani alikuwa afisa ugavi selikarin lakini lilipokuja swala la kumtumikia Mungu akaamua kuachana na kazi akaamua kufanya Hilo.

Japo awali anasema alipitia changamoto nyingi sana kwakuwa alikuwa na familia na inategemea mahitaji kutoka kwake lakini Leo tunaona Ni miongoni mwa watumishi wa Mungu waliofanikiwa kihuduma na kiuchumi pia.

Mimi nmemtaja yeye yawezekana nawewe Kuna ushuhuda wa wengine wengi unaowajua wenye senario za Namna hiyo.

Wewe kupitia hili umejifunza nini au unashauri nini mtu ambaye yupo kazini lakini kazi imekuwa kama mzigo kwake na ndani mwake anaona anawito wa kumtumikia Mungu ambao yawezekana ukabadiri hatima yake ikawa Bora zaidi.

Na akiwa anafanya lolote linalomuhusu Mungu Kuna mwanga anauona ila ujasiri wa kufanya maamuzi ya kuacha kazi ndio unakosekana Kwani familia inategemea.

Karibu sana Kwa mawazo na Mungu akubariki.

Na Mwl Kazidi "The code breaker"
 
Wewe kupitia hili umejifunza nini au unashauri nini mtu ambaye yupo kazini lakini kazi imekuwa kama mzigo kwake na ndani mwake anaona anawito wa kumtumikia Mungu ambao yawezekana ukabadiri hatima yake ikawa Bora zaidi
Ni hivi;
Kumtumikia Mungu ni wito. Watu wanaoitwa na Mungu kwa ajili ya kumtumikia huwa hawaombi ushauri kwa watu. Wanatoa taarifa za kufuata taratibu za wito wao.

Ukiona mtu anataka ashauriwe juu ya kuacha kazi yake (kama anayo) au asiache, ujue huyo hana wito. Huenda anafikiria zaidi kuanzisha kanisa na kunufaika na matoleo yeye binafsi.
 
Mambo ya kumtumikia Mungu ni ya kiroho sana. Kama wewe ni mtu wa rohoni na ukaambiwa uache kazi utumike na Mungu its okay. LAKINI kama wewe ni wa mwilini.... macho yako yanangalia kimwili na umetamani faida za kumtumikia Mungu ukaamua kuacha kazi ili utumike ule sadaka na vya madhabahuni HUTAFANIKIWA, utaishia kutafuta nguvu za miujiza na utamtumikia shetani badala ya Mungu.
 
Kuacha kazi sio tatizo,jambo muhimu ni wewe kumwomba Mungu akujalie kujua wakati sahihi wa wewe kufanya maamuzi hayo.
 
Waulize kama wanaweza kuifanya hiyo kazi bila zile sadaka, kisha urudi na majibu hapa.

Mtu anaacha kazi anayosubiria mshahara kwa kila mwezi, kisha anaenda kupokea sadaka kila weekend. Bila sadaka hawezi kuacha kazi, na hiyo point ya kumtumikia Mungu hauwezi kuisikia.

Kiuhalisia kinachofanyika sio kuacha kazi, ni kubadilisha tu kazi, hivi mtaibiwa mpaka lini.?
 
hio kazi inalipa sana mkuu.
nenda kawaongoze kondoo umiliki renji
Sio wote wanapata neema hiyo, makanisa yapo mengi, mengine hayana watu Kama vile ya kina mwamposa watu kufulika vile, wengine watu kumi hawafiki ndani na sio watoa sadaka wazuri.
 
Kama Mungu kweli ndio kakuita na umeisikia sauti yake dhahiri na ukaijaribu kwamba ni yeye kweli unaacha na inatumia!!

Lakini kama unajisikia jisikia tu kama wengi wafanyavyo eti najisikia sikia kumtumikia Mungu !!!!usije jaribu utajuta!!

Halafu sio Kila mtumishi unaemwona anamtumikia Mungu, wengine hudhani hivyo kumbe wanatumikia taaisisi ambayo wanadhani ni ya Mungu kumbe sio,na wengine ni wajasiria Mali wa kiroho!!
 
Habari Wana jamvi, naiheshimu sana JamiiForums kwani ni forum ambayo imekuwa ikifanya kazi kubwa ya kuielimisha jamii katika nyanja mbalimbali.

Na hii ni kwasababu imejawa na watu wengi wenye ufahamu mkubwa juu ya mambo mbalimbali na experience tofauti. Leo nmesukumwa tushirikishane juu ya mada niliyoweka hapo juu.

Viongozi wengi wa dini pamoja na watumishi wengi kwenye shuhuda zao mbalimbali hasa upande wa dini ya kikristo ambayo ninaufahamu nayo Kwa asilimia nyingi kidgo nikilinganisha na dini nyingine.

Huwa wanaongea kwamba waliacha hiki(kazi) wakaamua kufanya hiki(kutumikia Mungu ) Kwa kumaanisha yaani sio Kwa kudonoa donoa.

Nilishawahi kumsikia Mtumishi wa Mungu mwl Christopher Mwakasege akisema zamani alikuwa afisa ugavi selikarin lakini lilipokuja swala la kumtumikia Mungu akaamua kuachana na kazi akaamua kufanya Hilo.

Japo awali anasema alipitia changamoto nyingi sana kwakuwa alikuwa na familia na inategemea mahitaji kutoka kwake lakini Leo tunaona Ni miongoni mwa watumishi wa Mungu waliofanikiwa kihuduma na kiuchumi pia.

Mimi nmemtaja yeye yawezekana nawewe Kuna ushuhuda wa wengine wengi unaowajua wenye senario za Namna hiyo.

Wewe kupitia hili umejifunza nini au unashauri nini mtu ambaye yupo kazini lakini kazi imekuwa kama mzigo kwake na ndani mwake anaona anawito wa kumtumikia Mungu ambao yawezekana ukabadiri hatima yake ikawa Bora zaidi.

Na akiwa anafanya lolote linalomuhusu Mungu Kuna mwanga anauona ila ujasiri wa kufanya maamuzi ya kuacha kazi ndio unakosekana Kwani familia inategemea.

Karibu sana Kwa mawazo na Mungu akubariki.

Na Mwl Kazidi "The code breaker"
Ni kusonga mbele wala hakuna kusita wala kuuliza...manake sisi wanadamu hatuna uwezo wa kuzijua njia za Mungu.
 
Back
Top Bottom