mmmuhumba
JF-Expert Member
- Nov 8, 2017
- 491
- 476
1. Msimamo
Kuonyesha upo naye kwenye wakati wote iwe kwenye shida na raha, kwenye changamoto zake na zako. Kuacha ile tabia ya pale unapokuwa unahitaji kitu toka kwake unakuwa mpole ila ukishapata basi umemaliza mjuaji ni wewe.
Kuonyesha huna tamaa za kutaka kila mwanaume na kila kitu uwe wewe tu. Onyesha umetulia ushtushi na mbwembwe za watu na maisha.
2. Onyesha kuwa na nia na unachokusudia
Iwe ni biashara, ndoa, kuwa na maisha bora, kuleta faida ama kusaidia. Basi onyesha unajitenga na matumizi ya ovyo, mawazo povu ya maisha, vitabia vya kukera nk. Mfanye aone ni sifa na hadhi kuwa nawe kwa kuonyesha kweli umekusudia kitu chema. Jitenhe na vyote vitavyokuonyesha wewe huna nia kama kujichanganya na watu asiopenda, kufanya asiyoyataka na kuwa mtu wa hasara kwake.
3. Usiwe mchoyo
Anapohitaji kutetewa basi mtetee, kitu, ushauri, msaada, penzi, nk. kama vipo kwenye uwezo wako fanya. Unaposema unampenda na uwezi kumpa atakacho nalo ni tatizo, siyo wanaume wote ni wavumilivu wa kusubiria au kufumbia macho baadhi ya mambo. Wanaume wanatabia ya kupenda na kushindwa kulazimisha mwanamke wake afanye atakacho badala yake uanzisha mahusiano mapya pembeni ambapo atapata atakavyo.
4. Onyesha una muda naye
Usimtenge, usijifanye uko bize, kujiweka mbali nae nk. Hata kama unamtambua hulka zake, unapohitaji kitu ziweke pembeni ufanikiwe malengo aliyokupa.
5. Mheshimu na mheshimishe
Mkweze aone yeye amefika sehemu sahihi, usimchunge kwa uwazi, muweke wazi kuwa ni shemeji kwa rafikizo na nduguzo, penda kuzungumza naye pale penye gumu katika faragha. Unapofanya haya ni rahisi yeye kuona hekima yako, kukua kwako, uhuru kuwa nawe hivyo ufanya akuamini.
6. Onyesha chochote unachofanya/ utachofanya kina maslahi ya kwake/wote
Kumjali yeye, kumlinda yeye, maendeleo yenu ya baadae, kuogopa kumkosa maishani, kumpa faida, kuwa muwazi katika ndoto zako na unachowaza kukifanya. Mwanaume ni rahisi kutoa nguvu zake na mawazo yake kwenye jambo au kitu chenye kumpa faida.
7. Kuonyesha kupenda waliokaribu naye
Muonyesha mapenzi, jali familia yake kama amekuonyesha, watu wake na kile anachokifanya. Wanaume wengi uolea familia na siyo wao. Sifa zinazotoka huku uzidi kupanda thamani kwake. Mwanaume anaposifiwa alichokichagua moyo wake huwa mwepesi na ukitunza.
8. Jiongeze kimapenzi na kimaisha
Cheza na hisia zake na mitazamo yake ya maisha. Kama hana kitu basi onyesha wewe siyo muoga wa maisha, mpe faraja, mnogeshe kwa mahaba, kuwa mtundu, pendeza, mtege, mvuruge akili kimahaba, onyesha kujali kilichopo, usiwe na papara, tambua muda sahihi wa kukumbushia ahadi ama kuomba kitu. Hii itamfanya aamini wewe ni wake.
9. Kuwa na nadhimu
Iwe fedha, mali, mawazo, vitu,utiifu,maelekezo akupayo yazingatie, utunzaji, ukumbushaji, weka umbali na mambo asiyopenda na usimpande.
10. Kuwa mlezi
Onyesha unajali, unapenda kuwa mke, kuwa mama, mwenye mambo machache, toa bila kuombwa, hata kama huna mtoto, au huna ndoto za kupata mtoto au una tatizo lipo nje ya uwezo wako. Ulezi ni kuweza kuishi na mtu wako.
Kuonyesha upo naye kwenye wakati wote iwe kwenye shida na raha, kwenye changamoto zake na zako. Kuacha ile tabia ya pale unapokuwa unahitaji kitu toka kwake unakuwa mpole ila ukishapata basi umemaliza mjuaji ni wewe.
Kuonyesha huna tamaa za kutaka kila mwanaume na kila kitu uwe wewe tu. Onyesha umetulia ushtushi na mbwembwe za watu na maisha.
2. Onyesha kuwa na nia na unachokusudia
Iwe ni biashara, ndoa, kuwa na maisha bora, kuleta faida ama kusaidia. Basi onyesha unajitenga na matumizi ya ovyo, mawazo povu ya maisha, vitabia vya kukera nk. Mfanye aone ni sifa na hadhi kuwa nawe kwa kuonyesha kweli umekusudia kitu chema. Jitenhe na vyote vitavyokuonyesha wewe huna nia kama kujichanganya na watu asiopenda, kufanya asiyoyataka na kuwa mtu wa hasara kwake.
3. Usiwe mchoyo
Anapohitaji kutetewa basi mtetee, kitu, ushauri, msaada, penzi, nk. kama vipo kwenye uwezo wako fanya. Unaposema unampenda na uwezi kumpa atakacho nalo ni tatizo, siyo wanaume wote ni wavumilivu wa kusubiria au kufumbia macho baadhi ya mambo. Wanaume wanatabia ya kupenda na kushindwa kulazimisha mwanamke wake afanye atakacho badala yake uanzisha mahusiano mapya pembeni ambapo atapata atakavyo.
4. Onyesha una muda naye
Usimtenge, usijifanye uko bize, kujiweka mbali nae nk. Hata kama unamtambua hulka zake, unapohitaji kitu ziweke pembeni ufanikiwe malengo aliyokupa.
5. Mheshimu na mheshimishe
Mkweze aone yeye amefika sehemu sahihi, usimchunge kwa uwazi, muweke wazi kuwa ni shemeji kwa rafikizo na nduguzo, penda kuzungumza naye pale penye gumu katika faragha. Unapofanya haya ni rahisi yeye kuona hekima yako, kukua kwako, uhuru kuwa nawe hivyo ufanya akuamini.
6. Onyesha chochote unachofanya/ utachofanya kina maslahi ya kwake/wote
Kumjali yeye, kumlinda yeye, maendeleo yenu ya baadae, kuogopa kumkosa maishani, kumpa faida, kuwa muwazi katika ndoto zako na unachowaza kukifanya. Mwanaume ni rahisi kutoa nguvu zake na mawazo yake kwenye jambo au kitu chenye kumpa faida.
7. Kuonyesha kupenda waliokaribu naye
Muonyesha mapenzi, jali familia yake kama amekuonyesha, watu wake na kile anachokifanya. Wanaume wengi uolea familia na siyo wao. Sifa zinazotoka huku uzidi kupanda thamani kwake. Mwanaume anaposifiwa alichokichagua moyo wake huwa mwepesi na ukitunza.
8. Jiongeze kimapenzi na kimaisha
Cheza na hisia zake na mitazamo yake ya maisha. Kama hana kitu basi onyesha wewe siyo muoga wa maisha, mpe faraja, mnogeshe kwa mahaba, kuwa mtundu, pendeza, mtege, mvuruge akili kimahaba, onyesha kujali kilichopo, usiwe na papara, tambua muda sahihi wa kukumbushia ahadi ama kuomba kitu. Hii itamfanya aamini wewe ni wake.
9. Kuwa na nadhimu
Iwe fedha, mali, mawazo, vitu,utiifu,maelekezo akupayo yazingatie, utunzaji, ukumbushaji, weka umbali na mambo asiyopenda na usimpande.
10. Kuwa mlezi
Onyesha unajali, unapenda kuwa mke, kuwa mama, mwenye mambo machache, toa bila kuombwa, hata kama huna mtoto, au huna ndoto za kupata mtoto au una tatizo lipo nje ya uwezo wako. Ulezi ni kuweza kuishi na mtu wako.