Ashura9
JF-Expert Member
- Oct 21, 2012
- 740
- 485
Kushindwa kwa uume kusimama pia hutambulika kama kuishiwa nguvu za kiume. Ni kitendo cha mtu kushindwa kusimamisha uume au kudumisha usimamaji wa uume kwa muda wa kutosha kufanya tendo la tendo na mwenzake. Lakini wakati hii inaweza kumfikisha mwanaume katika upeo wa raha (orgasm), hali hii yaweza kumuacha mwanamke akiwa hakutosheka.
Kushindwa kwa uume kusimama kunaweza kutokea kwasababu ambazo ni pamoja na;
Kushindwa kwa uume kusimama kunaweza kutokea kwasababu ambazo ni pamoja na;
- Umri mkubwa zaidi
- Kisukari
- Kujichua/Punyeto
- Uzinzi
- Kukosa Elimu ya vyakula
- Kutokujishughulisha na mazoezi
- Shinikizo la juu la damu
- Maradhi ya moyo
- Uvutaji sigara/tumbaku
- Utumiaji uliozidi wa kafeina.
- Na kama hujuwi kafeina ni;
- Kafeina ni nini?
Kafeina ni madawa ya kulevya kundi la ‘Stimulants drugs’.
Utashangaa. Habari ndiyo hiyo. Hii ndiyo sababu kwa mtu aliyezoea kunywa chai hii kila siku au kahawa, siku asipokunywa kichwa humuuma, ni kwasababu amekuwa mtegemezi au teja wa kafeina.
Kafeina ni kiungo mhimu karibu katika soda zote zenye rangi nyeusi; Coca-cola, Pepsi, Sayona nyeusi, Azam cola na kadharika. Kafeina huongezwa pia katika Red bull, Malta na katika baadhi ya dawa za kupunguza maumivu mwilini.
Kwahiyo Kafeina ambayo hupatikana katika chai na kahawa ni aina mojawapo ya madawa ya kulevya.
- Kudhurika kwa neva au uti wa mgongo
- Madawa ya kulevya kama vile bangi, heroini, kokeini, na pombe
- Kiwango kidogo cha homoni ya testerone
- Athari kutoka kwa baadhi ya dawa