Hakuna ubishi kuwa kama Tanzania ingekuwa na upinzani unaodhamiria kuchukua madaraka bila kungoja uchaguzi,mgomo wa sasa wa madaktari unaoathiri walalahoi wengi ulifaa kutumiwa kama kifyatulio (Trigger). Ni bahati mbaya sana kuwa CHADEMA wameshindwa kutumia fursa hii. Je wewe kama mkereketwa na muathirika wa hali hii ungeshauri nini kifanyike wakati huu? Je hapa tatizo ni wapinzani au watanzania kwa ujumla kungoja mjomba fulani aje kuwapigania?
Mapinduzi yoyote hayapangwi mezani, bali hutokea mara watu wanapokosa uvumilivu wa mateso na maonevu yanayotendwa na watawala. Ipo siku yaweza kutokea nawe ukawa shuhuda, ccm dharau yao na aibu itakuwa yao pia.