Nini maana ya "Wakili msomi"?

Wanacheza na logic tu
 
Unajua hata Yesu ni wakili wa Wakristo, Hata Mama yako ni wakili wa familia yenu, hata wewe ni wakili wa hisia zako. Sasa kuna wale uwakili waneufuata shule ndio hujiita Wakili Msomi🤣
 
Hata mie hili limekuwa linanitatanisha sana na kutaka kujua kwa nini inatumika kwa mawakili pekee? Kwa nini daktari haitwi daktari msomi? au mwalimu msomi?
 
Wameanzisha miaka kama kumi iliyopita. Toka dunia imeumbwa hakukuwa na huu uhuni.

Ni uhuni wa kuchukua pesa zako haupo sehemu nyingine yoyote duniani.

UK, EU , USA hakuna huo ujinga. Wamesoma zaidi ya hawa Watanzania wachache wahuni.
 
Wewe ni ndugai au umetumwa na ndugai
 
Pia mtu kuitwa wakili msomi kwako inakupa shida gani?
Ni nani aliye kuponzwa ukaenda kusomea ualimu harafu leo unaona gele kwa walio somea "usomi"
Infact, tumekubaliana taaluma yetu ni ya wasomi (learned prominent lawyer) na tulio wakaribisha kujiita wasomi ni madaktari wengine wote makida makida.
Tena uwe unawaita "mwanasheria msomi sana, wakili wa mahakama kuu, muheshimiwa mwabukusi
 
Mtu asiyesommea sheria pia anaweza kuwa wakili.
Ndiyo maana Learned counsel anatofautishwa na Layman kwa kuitwa wakili msomi.
Yaani siyo wakili ambae hajasomea sheria, ingawa unaweza kusomea sheria na ukachagua kutokuwa wakili.
 
Elimu ya Tanzania ni ya maonesho, sahivi kuna CPA Rama, n.k. Mhandishi Asha ishazoeleka, bado watu wa IT, Pharmacy na wanaofanana na hao hawajapata Prefix za kuattach. Kuna Architect John and so on. Siyo elimu ya kutatua changamoto za jamii bali ya kujitambulisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…