Nini maana ya maneno haya ya mathayo 7: 13 - 23?

Nini maana ya maneno haya ya mathayo 7: 13 - 23?

The real Daniel

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2017
Posts
2,144
Reaction score
8,027
Mathayo 7:13-24
Biblia Habari Njema (BHN)

13. “Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kwenye maangamizi ni pana, na mlango wa kuingilia humo ni mpana; waendao njia hiyo ni wengi.

14. Lakini njia inayoongoza kwenye uhai ni nyembamba, na mlango wa kuingilia humo ni mwembamba; ni watu wachache tu wanaoweza kuigundua njia hiyo.

15. “Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali.

16. Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La!

17. Basi, mti mzuri huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.

18. Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.

19. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.

20. Kwa hiyo, mtawatambua kwa matendo yao.

21. “Si kila aniambiaye, ‘Bwana, Bwana’, ataingia katika ufalme wa mbinguni; ila ni yule tu anayetimiza matakwa ya Baba yangu aliye mbinguni.

22. Wengi wataniambia siku ile ya hukumu: ‘Bwana, Bwana! Kwa jina lako tulitangaza ujumbe wako, na kwa jina lako tuliwatoa pepo na kufanya miujiza mingi’.

23. Hapo nitawaambia: ‘Sikuwajua nyinyi kamwe; ondokeni mbele yangu, enyi watenda maovu.’
 
Matendo (si maneno pekee) yanadhihirisha wema ama uovu wetu.
 
Mbona ipo wazi sana mkuu.
IPO wazi Ila inahitaji kuelewa vizuri,
1. Njia ya kumpata kristo ni WACHACHE Sana wanaoigundua kuliko wanaodai kuwa wameipata. ( Inabidi uiangalie Sana sehemu uliyopo Kama IPO kwenye njia pana au mpo nyembamba)

2. Wengi wanoafanya miujiza katika jina la yesu; Yesu hawatambui( kazi kwako kujua ni akina Nani)

Wengi wanahitaji kuielewa hii mistari ili wampate kristo
 
Back
Top Bottom