picha ya kwanza ianonyesha matabaka mawili tofauti katika maisha maskini na matajiri
maskini wanaangaika shambani kulima na kuvuna wakati matajiri wanatumia mavuno hayo katika matumizi ambayo si msingi(?)(kwaida jamii nyingi hata za kiafrika hutumia nafaka kuwamwagia wali au maarusi).Watu waliopo hapo wanaweza kuwa watu wa dunia ya tatu hasa Asia (Vietnam/China) na wale wa nchi za magharibi
picha ya pili kuna mwili wa mwanaume mwenye kichwa mithili ya ATM kadi (Visa card) na mwili wa mwanamke mwenye kichwa cha mashine ya kutolea fedha(ATM machine) hiyo ni ishara simple kwamba akili ya mwanamke iko katika fedha za mwanaume na mwanaume ndiye mmilki na mtoahi wa fedha kwa mwanamke.
ya tatu ni mtu aliye na ufukara ambaye anawaza juu ya misha yake yalijaa ufukura(yanwakilshwa na panya,nguo zilizochakaa) wakati huo huo anatamani utajiri(Unawakilishwa na vipande/mirabaha ya dhahabu)
Picha ya nne kuna bunduki,mkono na maua.Bunduki imefichwa nyuma ya maua.Bunduki inawakilisha uadui,chuki na unafiki wakati maua yanawakilisha upendo,amani na furaha na mkono unawakilisha mtoaji.Tafsiri yake ni kwamba mtoaji anaonyesha upendo wa kinafiki ulioja chuki na uadui nyuma yake.Kwa methali ya kiswahili tungesema chui aliyevaa ngozi ya kondoo.