MOJAWAPO ya matukio ya kisiasa yaliyotawala vyombo vya habari, mazungumzo ya kawaida na mitandao ya kijamii mwezi Machi mwaka huu ni kuzinduliwa rasmi kwa Chama cha ACT-Wazalendo. Uzinduzi wa chama hiki ulifanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam Machi 29, 2015.
Mambo mawili muhimu yametawala mjadala kuhusu kuzinduliwa kwa chama hiki. Jambo la kwanza ni kuhusu itikadi ya chama, ambayo ni ujamaa wa kidemokrasia. Baadhi ya wachambuzi wa mambo ya kisiasa wamehoji uhalali na uhalisia wa chama hiki katika kuhuisha na kutekeleza siasa ya ujamaa katika mazingira ya dunia ya leo ambapo siasa za ubwanyenye zimetawala.
Jambo la pili ni muundo wa uongozi unaotumiwa na chama hiki. Tofauti na utaratibu uliozoeleka katika miundo ya uongozi ya vyama hapa nchini, ACT-Wazalendo kimekuja na muundo wenye Kiongozi wa Chama sambamba na Mwenyekiti wa Chama.
Katika makala ya leo ninajadili na kufafanua kuhusu dhana na msingi wa muundo wa uongozi wa ACT-Wazelendo. Nikipata fursa huko mbele nitajitahidi kufafanua dhana na msingi wa itikadi ya Demokrasia ya ujamaa kama inavyotumiwa na ACT-Wazalendo hasa katika mazingira ya Tanzania ya leo.
Jambo moja jema katika mjadala unaoendelea kuhusu ACT-Wazalendo ni kwamba angalau tumeanza kujadili kuhusu itikadi na mifumo ya uendeshaji wa vyama vya siasa, badala ya kila siku kujadili matukio ya kisiasa yanayotokea.
Mfumo wa uongozi wa ACT-Wazalendo unajumuisha Kiongozi wa Chama sambamba na Mwenyekiti wa Chama. Kimsingi huu ndio mfumo wa uongozi unaotumiwa na vyama vya siasa katika nchi nyingi zilizomo katika Jumuiya ya Madola.
Kwa mfano, nchini Uingereza mfumo wa uongozi wa chama cha Conservatives unajumuisha Kiongozi wa Chama na Wenyeviti wawili. Kiongozi wa Chama cha Conservatives ni Waziri Mkuu wa sasa David Cameron wakati Grant Shapps na Lord Feldman ni wenyeviti wa chama hicho. Kiongozi wa Chama cha Liberal Democrats ni Nick Clegg wakati mwenyekiti wa chama (wanamuita Rais) ni Sal Brinton.
Mifano pia ipo mingi katika Bara la Afrika. Kwa mfano, Raila Odinga ni Kiongozi wa ODM nchini Kenya wakati Mwenyekiti wa Chama hicho ni Henry Kosgey. Nchini Afrika Kusini, Kiongozi wa Chama tawala cha ANC ni Jacob Zuma wakati Mwenyekiti wa chama hicho ni mwana mama Baleka Mbete, ambaye pia ni Spika wa Bunge la Afrika Kusini.
Sababu ya msingi ya kuwa na mfumo wa uongozi wa chama tofauti na mwenyekiti ni kuepuka kutengeneza chama dola. Moja ya matatizo yanayoikumba demokrasia barani Afrika ni ukweli kwamba mfumo wa uongozi wa vyama vya siasa ni wa kidola.
Hapa kwetu, kwa mfano, CCM ni chama dola kwa maana kwamba kimejipenyeza serikalini kutokana na muundo wake ambapo mwenyekiti wake ndiyo huyohuyo anakuwa kiongozi wa serikali. Huyu akimaliza kuendesha vikao vya Baraza la Mawaziri anahamia kuendesha vikao vya chama. Ni kwa sababu hii chama kinakuwa hakina uwezo wala mamlaka ya kuhoji utendaji wa serikali yake.
Matokeo ya muundo huo ndio yanayomfanya sasa Katibu Mkuu wa CCM kufanya kazi ya vyama vya upinzani ya kulalamika na kuikemea serikali yake barabarani kwa sababu anajua kwamba hawezi kuwa na nafasi hiyo ndani ya vikao vya chama kwa sababu huko serikali ndiyo inayoendesha chama.
Mfumo wa chama dola wa CCM hauna tofauti na vyama vingine. Ndiyo kusema vyama hivi navyo vitalazimika kuwa vyama dola mara vitakapoingia madarakani. Mfumo wa chama dola ni hatari kwa demokrasia kwa sababu hulazimisha watumishi wa umma kufanya kazi ya chama tawala badala ya kutumikia serikali kwa mujibu wa taaluma zao.
Kwa hiyo, msingi wa kuwa na mfumo wa uongozi wa chama sambamba na uenyekiti ni kuondoa udola katika chama cha siasa. Mfumo huu unatoa nafasi kwa chama kuweza kuhoji na kusimamia utendaji wa serikali yake bila chenyewe kujigeuza kuwa serikali. Hiki ndicho kilichofanyika Afrika Kusini ambapo baada ya kuona Rais Thabo Mbeki ameshindwa kusimamia sera za ANC katika serikali chama kiliamua kumuweka pembeni na hatimaye kumchagua Jacob Zuma kuwa Kiongozi wa Chama na baadaye Rais wa Afrika Kusini. Jambo hili lisingewezekana katika mfumo wa chama dola.
Kwa hiyo msingi wa ACT-Wazalendo kuwa na mfumo wa Kiongozi wa Chama sambamba na Mwenyekiti ni kugawanya majukumu ya kuendesha mfumo wa chama na kueneza itikadi na sera za chama kwa umma. Kwa mujibu wa Katiba ya ACT-Wazalendo, jukumu la msingi la Kiongozi wa Chama nje ya serikali ni kueneza itikadi, falsafa, misingi na sera za chama kwa umma. Ndiyo kusema kazi kubwa ya Kiongozi wa Chama itakuwa ni kuongoza jahazi la kuzunguka nchini katika kusaka kuungwa mkono na wananchi.
Jukumu la msingi la Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo ni kusimamia uendeshaji wa chama na taasisi zake. Yeye ndiye atakuwa mwenyekiti wa vikao vyote vya maamuzi ndani ya chama ikiwemo Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu.
Siku ACT-Wazalendo ikichaguliwa na kuunda serikali jukumu la Kiongozi wa Chama litakuwa ni kusimamia uendeshaji wa serikali na kuhakikisha kwamba serikali inatekeleza sera za chama kikamilifu na atatoa taarifa ya utekelezaji wa sera katika vikao vya chama vitakavyoendeshwa na Mwenyekiti wa chama.
Mgawanyo wa majukumu ya Kiongozi Mkuu na Mwenyekiti wa Chama yanajitokeza pia katika mamlaka za uteuzi. Kwa mfano, Kiongozi Mkuu wa Chama ana mamlaka ya kupendekeza uteuzi wa wenyeviti wa kamati za kisera na washauri wa chama. Mwenyekiti kwa upande wake ana mamlaka ya kupendekeza uteuzi wa watendaji wa chama kama vile manaibu katibu wakuu.
Kwa hiyo, pamoja na kwamba kimuundo Kiongozi wa Chama ndiye mwenye mamlaka zaidi ya kiuongozi ndani ya ACT-Wazalendo, mgawanyo wa nafasi mbili za Kiongozi wa Chama na Mwenyekiti ni wa kimajukumu zaidi kuliko kimamlaka.
Tunaamini kwamba kwa kuwa na mfumo wa uongozi huu ni hatua muhimu ya kujenga chama cha siasa kisicho chama dola. Aidha mfumo huu utahakikisha kwamba Mwenyekiti wa chama anakuwa na nafasi ya kutosha ya kujenga na kusisimamia uendeshaji wa mifumo ya chama.
Chanzo:Raia mwema
Mambo mawili muhimu yametawala mjadala kuhusu kuzinduliwa kwa chama hiki. Jambo la kwanza ni kuhusu itikadi ya chama, ambayo ni ujamaa wa kidemokrasia. Baadhi ya wachambuzi wa mambo ya kisiasa wamehoji uhalali na uhalisia wa chama hiki katika kuhuisha na kutekeleza siasa ya ujamaa katika mazingira ya dunia ya leo ambapo siasa za ubwanyenye zimetawala.
Jambo la pili ni muundo wa uongozi unaotumiwa na chama hiki. Tofauti na utaratibu uliozoeleka katika miundo ya uongozi ya vyama hapa nchini, ACT-Wazalendo kimekuja na muundo wenye Kiongozi wa Chama sambamba na Mwenyekiti wa Chama.
Katika makala ya leo ninajadili na kufafanua kuhusu dhana na msingi wa muundo wa uongozi wa ACT-Wazelendo. Nikipata fursa huko mbele nitajitahidi kufafanua dhana na msingi wa itikadi ya Demokrasia ya ujamaa kama inavyotumiwa na ACT-Wazalendo hasa katika mazingira ya Tanzania ya leo.
Jambo moja jema katika mjadala unaoendelea kuhusu ACT-Wazalendo ni kwamba angalau tumeanza kujadili kuhusu itikadi na mifumo ya uendeshaji wa vyama vya siasa, badala ya kila siku kujadili matukio ya kisiasa yanayotokea.
Mfumo wa uongozi wa ACT-Wazalendo unajumuisha Kiongozi wa Chama sambamba na Mwenyekiti wa Chama. Kimsingi huu ndio mfumo wa uongozi unaotumiwa na vyama vya siasa katika nchi nyingi zilizomo katika Jumuiya ya Madola.
Kwa mfano, nchini Uingereza mfumo wa uongozi wa chama cha Conservatives unajumuisha Kiongozi wa Chama na Wenyeviti wawili. Kiongozi wa Chama cha Conservatives ni Waziri Mkuu wa sasa David Cameron wakati Grant Shapps na Lord Feldman ni wenyeviti wa chama hicho. Kiongozi wa Chama cha Liberal Democrats ni Nick Clegg wakati mwenyekiti wa chama (wanamuita Rais) ni Sal Brinton.
Mifano pia ipo mingi katika Bara la Afrika. Kwa mfano, Raila Odinga ni Kiongozi wa ODM nchini Kenya wakati Mwenyekiti wa Chama hicho ni Henry Kosgey. Nchini Afrika Kusini, Kiongozi wa Chama tawala cha ANC ni Jacob Zuma wakati Mwenyekiti wa chama hicho ni mwana mama Baleka Mbete, ambaye pia ni Spika wa Bunge la Afrika Kusini.
Sababu ya msingi ya kuwa na mfumo wa uongozi wa chama tofauti na mwenyekiti ni kuepuka kutengeneza chama dola. Moja ya matatizo yanayoikumba demokrasia barani Afrika ni ukweli kwamba mfumo wa uongozi wa vyama vya siasa ni wa kidola.
Hapa kwetu, kwa mfano, CCM ni chama dola kwa maana kwamba kimejipenyeza serikalini kutokana na muundo wake ambapo mwenyekiti wake ndiyo huyohuyo anakuwa kiongozi wa serikali. Huyu akimaliza kuendesha vikao vya Baraza la Mawaziri anahamia kuendesha vikao vya chama. Ni kwa sababu hii chama kinakuwa hakina uwezo wala mamlaka ya kuhoji utendaji wa serikali yake.
Matokeo ya muundo huo ndio yanayomfanya sasa Katibu Mkuu wa CCM kufanya kazi ya vyama vya upinzani ya kulalamika na kuikemea serikali yake barabarani kwa sababu anajua kwamba hawezi kuwa na nafasi hiyo ndani ya vikao vya chama kwa sababu huko serikali ndiyo inayoendesha chama.
Mfumo wa chama dola wa CCM hauna tofauti na vyama vingine. Ndiyo kusema vyama hivi navyo vitalazimika kuwa vyama dola mara vitakapoingia madarakani. Mfumo wa chama dola ni hatari kwa demokrasia kwa sababu hulazimisha watumishi wa umma kufanya kazi ya chama tawala badala ya kutumikia serikali kwa mujibu wa taaluma zao.
Kwa hiyo, msingi wa kuwa na mfumo wa uongozi wa chama sambamba na uenyekiti ni kuondoa udola katika chama cha siasa. Mfumo huu unatoa nafasi kwa chama kuweza kuhoji na kusimamia utendaji wa serikali yake bila chenyewe kujigeuza kuwa serikali. Hiki ndicho kilichofanyika Afrika Kusini ambapo baada ya kuona Rais Thabo Mbeki ameshindwa kusimamia sera za ANC katika serikali chama kiliamua kumuweka pembeni na hatimaye kumchagua Jacob Zuma kuwa Kiongozi wa Chama na baadaye Rais wa Afrika Kusini. Jambo hili lisingewezekana katika mfumo wa chama dola.
Kwa hiyo msingi wa ACT-Wazalendo kuwa na mfumo wa Kiongozi wa Chama sambamba na Mwenyekiti ni kugawanya majukumu ya kuendesha mfumo wa chama na kueneza itikadi na sera za chama kwa umma. Kwa mujibu wa Katiba ya ACT-Wazalendo, jukumu la msingi la Kiongozi wa Chama nje ya serikali ni kueneza itikadi, falsafa, misingi na sera za chama kwa umma. Ndiyo kusema kazi kubwa ya Kiongozi wa Chama itakuwa ni kuongoza jahazi la kuzunguka nchini katika kusaka kuungwa mkono na wananchi.
Jukumu la msingi la Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo ni kusimamia uendeshaji wa chama na taasisi zake. Yeye ndiye atakuwa mwenyekiti wa vikao vyote vya maamuzi ndani ya chama ikiwemo Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu.
Siku ACT-Wazalendo ikichaguliwa na kuunda serikali jukumu la Kiongozi wa Chama litakuwa ni kusimamia uendeshaji wa serikali na kuhakikisha kwamba serikali inatekeleza sera za chama kikamilifu na atatoa taarifa ya utekelezaji wa sera katika vikao vya chama vitakavyoendeshwa na Mwenyekiti wa chama.
Mgawanyo wa majukumu ya Kiongozi Mkuu na Mwenyekiti wa Chama yanajitokeza pia katika mamlaka za uteuzi. Kwa mfano, Kiongozi Mkuu wa Chama ana mamlaka ya kupendekeza uteuzi wa wenyeviti wa kamati za kisera na washauri wa chama. Mwenyekiti kwa upande wake ana mamlaka ya kupendekeza uteuzi wa watendaji wa chama kama vile manaibu katibu wakuu.
Kwa hiyo, pamoja na kwamba kimuundo Kiongozi wa Chama ndiye mwenye mamlaka zaidi ya kiuongozi ndani ya ACT-Wazalendo, mgawanyo wa nafasi mbili za Kiongozi wa Chama na Mwenyekiti ni wa kimajukumu zaidi kuliko kimamlaka.
Tunaamini kwamba kwa kuwa na mfumo wa uongozi huu ni hatua muhimu ya kujenga chama cha siasa kisicho chama dola. Aidha mfumo huu utahakikisha kwamba Mwenyekiti wa chama anakuwa na nafasi ya kutosha ya kujenga na kusisimamia uendeshaji wa mifumo ya chama.
Chanzo:Raia mwema