- Thread starter
- #21
Nakushukuru Padri mtarajiwa kwa ufafanuzi/mchango wako mzuri,lakini pamoja na maelezo yako mazuri, ningependa ufafanue zaidi pointi yako ya pili kwani katika utafiti wangu nimegundua kuwa wanandoa wengi waliooana kwa muda mrefu bila kupata watoto, ndoa zao huwa zinayumba sana hata wakati mwingine kupelekea kutengana.Mara nyingi vijana wanapooana matazamio yao hasa ya awali huwa ni kujiepusha na tamaa za mwili kama mtume Paulo alivyowambia Wakorintho , nanukuu "Ni bora kuoa kuliko kuwaka tamaa" Lakini baada ya kukaa Mwaka Wa 1, Wa 2 Wa 3 Wa 4 n.k bila kupata watoto malalamiko huanza mara oooh nataka mtoto mara ooh wewe hunifai hali ambayo hupelekea msongo mkubwa wa mawazo kwa wanandoa na hata amani kukosekana ndani ya ndoa! Je,nini ushauri wako kwa wanandoa inapotokea incidence kama hii,itapendeza zaidi pia kama utatoa reference kutoka kwenye Maandiko matakatifu ya Biblia!Mimi kama Padri wenu mtarajiwa nawaleteeni mafundisho haya kuntu ili yawafae na Mungu awabariki.
1. Kwa manufaa yenu ninyi mnaooana kusudi kuepuka vishawishi na tamaa mbalimbali. Kimsingi, kila mmoja anaoa ili amfae mwenzake na kujitoa kikamilifu kwa ajili ya mwenzake. Mnaoana kwa sababu mnajotoa kimasomaso kwa ajili yenu. Waweza hapa kurejea maandiko Matakatifu kidogo Mwanzo 2:23.
2. Kuzaa na kulea watoto. Walioamua kuoana huishi pamoja wakitarajia kupokea zawadi ya watoto kama baraka kutoka kwa Mungu. Kukosa watoto hakufanyi mapendo yenu kuwa batili au pungufu. Mnapata watoto ili mshirikiane na Mungu kuendeleza kazi yake ya uumbaji.
Karibu Paroko mtarajiwa!