Nini kinacho-define mafanikio katika maisha ya mwanadamu?

Ubumuntu

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
14,316
10,782
Salaam wana JF!

Kama wasafiri hapa duniani, binadamu tumekuwa tukipigana na kujitahidi kwamba tunapata mafanikio ili siku pale parapanda litakapolia, basi mtu aweze kuondoka na kuacha alama, kwamba jamaa alikuwa amefanikiwa au hajafanikiwa kimaisha n.k.

Je, mafanikio katika maisha ya binadamu ni nini?
Yanakuwa defined vipi?
Ni yapi yanayotufanye tuseme fulani kafanikiwa kimaisha?


Je, kuwa na mali nyingi - magari, nyumba, pesa n.k. ni mafanikio katika maisha?
Je, kusafiri na kutembelea nchi na sehemu mbalimbali duniani (hata nje ya dunia, mwezini, angani n.k.), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na kazi nzuri (yenye mshahara mnono au kazi unayoipenda), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na watoto wengi, ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na marafiki wengi (kuishi vizuri na binadamu wenzako), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na machapisho mengi (vitabu, articles n.k.), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na wake/waume au wapenzi wengi ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na mume au mke, ni mafanikio katika maisha?
Je, kushika neno la Mungu na kumwamini Yeye, ni mafanikio katika maisha?


Je, kuna universal meaning ya mafanikio ya maisha?

Hakika ninapata ugumu katika kudefine mafanikio katika maisha!

NB: Mtanisamehe sana kama mada kama hii imeshawahi kujadiliwa; kama ndiyo, basi ifutwe.
 
Mafanikio kwangu yalipatikana kipindi nilipompokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yangu.
 
Mafanikio ni kuwa na taaluma/kipaji, Afya njema,fedha au kipato cha uhakika na Familia bora kama huna baadhi au vyote kati ya hivyo hapo juu haujafanikiwa.Kwa hiyo endelea kuvisaka.
 
Hiyo ni relative terminology!

binafsi nikipata wake wanne ni mafanikio makubwa kweli kweli......

mwingine akipata baiskeli mbili ni mafanikio ya ajabu kweli kweli!
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Mafanikio ni kuwa na pesa mingi bwana!!

Pesa nyingi tu?! Hujali binadamu wenzako wanaokuzunguka? Ukifa, pesa zitakuzika?!
Ukifa, nani atakusifia kwamba una mafanikio ukifa kama wewe mafanikio kwako ni kuwa na pesa mingi?!?
 
Mafanikio ni kuwa na taaluma/kipaji, Afya njema,fedha au kipato cha uhakika na Familia bora kama huna baadhi au vyote kati ya hivyo hapo juu haujafanikiwa.Kwa hiyo endelea kuvisaka.

Kwa hiyo ipi ndio maana halisi? Kuwa na hivyo vyote au kuwa na kimoja kati hivyo?
Je, nikiwa na afya njema, nakuwa nimefanikiwa kimaisha?
Je, nikiwa na taaluma/kipaji, nakuwa nimefanikiwa kimaisha?
Je, nikiwa na fedha au kipato cha uhakika, nakuwa nimefanikiwa kimaisha?
Je, nikiwa na familia bora, nakuwa nimefanikiwa kimaisha?
 
Hiyo ni relative terminology!

binafsi nikipata wake wanne ni mafanikio makubwa kweli kweli......

mwingine akipata baiskeli mbili ni mafanikio ya ajabu kweli kweli!

Angalau umenipa mwanga kidogo. Lakini:
Kwa hiyo hakuna universal meaning?
Kwa hiyo unataka kumainisha hakuna binadamu aliye na mafanikio katika maisha kwa sababu maana ya mafanikio inatofautiana baina ya wanadamu au?
 
Mafaniko kwangu ni kuweza kutimiza njozi nilizonazo.

Kuna vitu fulani natamani kuvifanya au kuvifikia, nitajiona nimefanikiwa siku nikivimaliza.

Mtizamo wangu wa maisha ni kama movie, unaletwa duniani kucheza part fulani, ukiimaliza lazima uondoke.

Cha kujiuliza, ulikuja hapa duniani ili ukamilishe nini? Ukishajua umekuja ili ufanye nini, basi kamilisha kusudio hilo.
 
Mafaniko kwangu ni kuweza kutimiza njozi nilizonazo. Kuna vitu fulani natamani kuvifanya au kuvifikia, nitajiona nimefanikiwa siku nikivimaliza. Mtizamo wangu wa maisha ni kama movie, unaletwa duniani kucheza part fulani, ukiimaliza lazima uondoke. Cha kujiuliza, ulikuja hapa duniani ili ukamilishe nini? Ukishajua umekuja ili ufanye nini, basi kamilisha kusudio hilo.
Asante kwa maelezo. Ila hivyo vitu unavyotamani kuvifanya au kuvifikia ni vipi? Swali lako la mwisho, limebeba ujumbe mzito na wa maana sana. Kwa hiyo ukishafahamu wewe umeletwa duniani kucheza role gani (kusudio fulani), hiyo ndiyo inakuwa njia na mwanga katika kupata mafanikio? Hivyo unataka kusema ili kuweza kufanikiwa katika maisha, binadamu anapaswa ajitambue kwanza?
 
mafanikio kwangu ni kwa namna gani uwepo wangu duniani utaweza kuwafikia watu wengi, tena kwa jinsi nzuri na kwa namna moja au nyingine kuwawezesha kubadili maisha au hata muonekano wa mitazamo yao kwa namna bora zaidi ya walivyokuwa kabla ya uwepo wangu. Hayo kwangu mimi ndio mafanikio ya ziara yangu fupi hapa duniani!
 
"Success should be measured not so much by the position that one has reached in life... but by obstacles which he/she has overcome while trying to succeed."

Mkuu inategemea kama mimi nimejitahidi bila elimu wala bila mtaji wowote nikijitahidi na kuweza kufungua kibanda cha nyanya nitakuwa-more successfully kuliko yule aliyeweza kujenga hoteli kwa kutumia mikopo au urithi na support ya wazazi.

Nikiwa siwezi kuongea vizuri nikajitahidi kutoa single moja nitakuwa more successfully huenda kuliko hata Whitney au Michael ambao walikuwa na vipaji
 
Watu wanaweza kuwa na definitions mbalimbali za mafaninikio.Lakini wengi hasa wasio mjua Mungu, wanadhani mafanikio ni yale yanayohusiana na kuustarehesha mwili.Kama unavyosema, kuwa na magari,nyumba nzuri nk.But that is nonsense, kwakuwa maisha ya duniani ni mafupi na safari towards a more permanent life ya umilele.Sio vibaya kuwa na nyumba na magari,lakini la msingi ni kuwa na uhusiano mzuri na Mungu wa kweli.Remember there are so many gods,hata Maitreya ni mungu kwa wengine,but he is not a true God.So mafanikio ya kweli duniani ni kuwa na uhusiano mzuri na Mungu wa kweli.Mengine yafuate baada ya hapo.
Salaam wana JF!

Kama wasafiri hapa duniani, binadamu tumekuwa tukipigana na kujitahidi kwamba tunapata mafanikio ili siku pale parapanda litakapolia, basi mtu aweze kuondoka na kuacha alama, kwamba jamaa alikuwa amefanikiwa au hajafanikiwa kimaisha n.k.

Je, mafanikio katika maisha ya binadamu ni nini?
Yanakuwa defined vipi?
Ni yapi yanayotufanye tuseme fulani kafanikiwa kimaisha?


Je, kuwa na mali nyingi - magari, nyumba, pesa n.k. ni mafanikio katika maisha?
Je, kusafiri na kutembelea nchi na sehemu mbalimbali duniani (hata nje ya dunia, mwezini, angani n.k.), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na kazi nzuri (yenye mshahara mnono au kazi unayoipenda), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na watoto wengi, ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na marafiki wengi (kuishi vizuri na binadamu wenzako), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na machapisho mengi (vitabu, articles n.k.), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na wake/waume au wapenzi wengi ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na mume au mke, ni mafanikio katika maisha?
Je, kushika neno la Mungu na kumwamini Yeye, ni mafanikio katika maisha?


Je, kuna universal meaning ya mafanikio ya maisha?

Hakika ninapata ugumu katika kudefine mafanikio katika maisha!

NB: Mtanisamehe sana kama mada kama hii imeshawahi kujadiliwa; kama ndiyo, basi ifutwe.
 
Asante kwa maelezo. Ila hivyo vitu unavyotamani kuvifanya au kuvifikia ni vipi? Swali lako la mwisho, limebeba ujumbe mzito na wa maana sana. Kwa hiyo ukishafahamu wewe umeletwa duniani kucheza role gani (kusudio fulani), hiyo ndiyo inakuwa njia na mwanga katika kupata mafanikio? Hivyo unataka kusema ili kuweza kufanikiwa katika maisha, binadamu anapaswa ajitambue kwanza?[/QUOTE]

Kwa mtazamo wangu hiii ni MUHIMU KULIKO VITU VYOTE KATIKA KUSAKA MAFANIKIO; usipojua UNACHOTAKA kufanya katika maisha yako si utajikuta unaishi kama testa ya umeme?? Unaingia katika kila soketi-yote wayajaribu wakati hakuna hata moja ulipalo uzito wa ktoka moyoni mwako
 
Asante kwa maelezo. Ila hivyo vitu unavyotamani kuvifanya au kuvifikia ni vipi? Swali lako la mwisho, limebeba ujumbe mzito na wa maana sana. Kwa hiyo ukishafahamu wewe umeletwa duniani kucheza role gani (kusudio fulani), hiyo ndiyo inakuwa njia na mwanga katika kupata mafanikio? Hivyo unataka kusema ili kuweza kufanikiwa katika maisha, binadamu anapaswa ajitambue kwanza?[/QUOTE]

Kwa mtazamo wangu hiii ni MUHIMU KULIKO VITU VYOTE KATIKA KUSAKA MAFANIKIO; usipojua UNACHOTAKA kufanya katika maisha yako si utajikuta unaishi kama testa ya umeme?? Unaingia katika kila soketi-yote wayajaribu wakati hakuna hata moja ulipalo uzito wa ktoka moyoni mwako

nimepapenda hapa!
 
Salaam wana JF!

Kama wasafiri hapa duniani, binadamu tumekuwa tukipigana na kujitahidi kwamba tunapata mafanikio ili siku pale parapanda litakapolia, basi mtu aweze kuondoka na kuacha alama, kwamba jamaa alikuwa amefanikiwa au hajafanikiwa kimaisha n.k.

Je, mafanikio katika maisha ya binadamu ni nini?
Yanakuwa defined vipi?
Ni yapi yanayotufanye tuseme fulani kafanikiwa kimaisha?


Je, kuwa na mali nyingi - magari, nyumba, pesa n.k. ni mafanikio katika maisha?
Je, kusafiri na kutembelea nchi na sehemu mbalimbali duniani (hata nje ya dunia, mwezini, angani n.k.), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na kazi nzuri (yenye mshahara mnono au kazi unayoipenda), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na watoto wengi, ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na marafiki wengi (kuishi vizuri na binadamu wenzako), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na machapisho mengi (vitabu, articles n.k.), ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na wake/waume au wapenzi wengi ni mafanikio katika maisha?
Je, kuwa na mume au mke, ni mafanikio katika maisha?
Je, kushika neno la Mungu na kumwamini Yeye, ni mafanikio katika maisha?


Je, kuna universal meaning ya mafanikio ya maisha?

Hakika ninapata ugumu katika kudefine mafanikio katika maisha!

NB: Mtanisamehe sana kama mada kama hii imeshawahi kujadiliwa; kama ndiyo, basi ifutwe.

mafanikio =success??
kama ndivyo ...maana yake kuna kitu ulikuwa unapigania au kustruggle ndio umefanikisha...

kitu hicho ni kipi??

kila mmoja ana priorities zake

wakati maskini anatafuta mali.....tajiri anatafuta amani!!

personally nadhani mafanikio ni kuwa na FURAHA NA AMANI IDUMUYO!

You may be hungry but peacefull, you may not have money but joyfully

watoto wa maskini wanaochezea mpira wa kufunga funga na kamba fuaha yao ni sawa kabisa na watoto wa matajiri wanaochezea mpira wa dukani!!

Amani ya kweli inapatikana kwa kumjua Mungu
 
hili swali halina jibu kamili. its is relative to what you are refering to. muda mwingine mtu huwa anasema amefanikiwa pale anapotaka jambo fulani na akalipata. kwahiyo unapopata unachokitaka kwa wakati huo basi hayo ni mafanikio.
 
Mafanikio ni kuwa na taaluma/kipaji, Afya njema,fedha au kipato cha uhakika na Familia bora kama huna baadhi au vyote kati ya hivyo hapo juu haujafanikiwa.Kwa hiyo endelea kuvisaka.

afya njema sio mafanikio bana, itoe kwenye kundi hili.
 
hili swali halina jibu kamili. its is relative to what you are refering to. muda mwingine mtu huwa anasema amefanikiwa pale anapotaka jambo fulani na akalipata. kwahiyo unapopata unachokitaka kwa wakati huo basi hayo ni mafanikio.

kama nimemuelewa mleta mada, ni kwamba anazungumzia mafanikio yakiwa judged na watu wengine, sio self satisfaction.
 
Angalau umenipa mwanga kidogo. Lakini:
Kwa hiyo hakuna universal meaning?
Kwa hiyo unataka kumainisha hakuna binadamu aliye na mafanikio katika maisha kwa sababu maana ya mafanikio inatofautiana baina ya wanadamu au?

mafanikio gani unaulizia, jinsi anavyojisikia mtu binafsi au anavyoonekana kwa watu wengine?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom