Nini husababisha baridi?

Plaimali=Primary
 
Mkuu !
Ktk physics pamoja na geography ya o level unaweza pata majibu ya swali lako japo kwa juu juu !

Pressure huongezela kadri unavyo kwenda katika usawa wa bahari na kadri uendavyo ktk centre of the earth ( earth crust )

Ktk Charles , Boyles and pressure laws , pressure huwa directly proportional to pressure ! Hivyo kadri pressure inaongezeka ndivyo na joto huongezeka !

Pengine swali lingine litakuwa kwa nn pressure iongezeke kadri uendavyo bondeni ! Labda jibu linaweza kuwa ni kwa kuwa gravitational force huongezeka pia kadiri uendavyo chini na hupungua kadri uendavyo nje ya usawa wa dunia na ukitoka ktk orbit kunakuwa hakuna kabisa !

Nimejaribu kufadavua kwa kashule kadogo ka o level ! Nadhani waliopiga geography a level watatupa majibu sahihi zaidi !

Mimi huwa najiuliza kwa nini kukianza pambazuka kunakuwa na kabaridi kakali sana ghafla !? Pls wenye shule zao mtusaidie hapa
 
Presur ikipungua joto hupungua.

Jinsi unavyoenda mbali na usawa wa bahari hewa huwa nyepesi na presure huwa ndogo thats why joto hupungua
 
 
Ndugu swali lako ni la msingi sana. Kama tujuavyo kipimo cha joto kwenye jua ni zaidi ya nyuzi ,6000cent.gredi . Ni kweli joto hupungua kadri unavyokwenda juu . Na hii hutokea kwenye tabaka la chini la anga linaloitwa kwa kiingereza Troposphere. Tabaka hili hupatikana kuanzia usawa wa ardhi hadi kilometa 9-10 kwenda juu kulingana na latitude ya mahali husika. Cha msingi hapa Ni kuwa molecule za hewa zipo nyingi usawa wa ardhi na hupungua kadri unavyopanda juu kutokana na nguvu ya uvutano ya dunia na tabaka la hewa lililo juu yake. Na hii nguvu ya uvutano pia hupungua kadri unavyoeleakea juu. Hoja ingine ni kuwa jua hutoa mionzi yenye mawimbi mafupi yaani short wave radiation ambayo inauwezo wa kupenya tabaka la hewa la troposphere bila kuliasha joto . Ndiyo maana ukisogea karibu na jua yaani juu unapata baridi kinyume cha matarajio. Hivyo mionzi inapofika ardhini ndipo hufyonzwa na ardhi nayo ardhi hupasha joto hewa iliyolala kwenye usawa wa ardhi kwa njia ya conduction na baada ya hiyo hewa kuchemshwa hupasia joto kwa molecules za hewa zilizo juu yake kwa njia ya convection ,( mvukisho). Sasa kwa vile hewa inapungua kadri unavyoenda juu uwezo wa kusafirisha joto kwa njia mvukisho nayo hupungua hivyo kufanya tabaka la juu la hewa linabaki na joto kidogo kuliko la chini. Je Nishati ya jua yaani ile short wave radiation ilifvyozwa (absorbed )na ardhi linakwenda wapi? Hii inabadilishwa kuwa mionzi ya mawimbi marefu yaani long wave radiation na hurudi tena angani na ndiyo inayofanya tuhisi joto nyakati za usiku na baridi kuzidi alfajiri wakati nishati hiyo inapokuwa imekwisha kutoroka yote kurudi kwenye outer space. Kumradhi kwa KISWA_NGLISH lengo ni kutaka kueleweka zaidi na wote.
 

Attachments

  • IMG-20160609-WA0001.jpg
    27.6 KB · Views: 35
mzeewamakavu asante sana ! Umesomeka vizuri sana ! Nitairudia mara kwa mara niielewe vizuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…