Nini hasa kinafanya siku ya tarehe 01/01/ kuwa special sana kuliko siku nyingine zote za mwaka?

I am Groot

JF-Expert Member
Jul 20, 2018
3,730
10,033
Binafsi sioni tofauti yoyote iliyopo siku hiyo ya tarehe 1 mwezi wa kwanza, ingawa nimezaliwa na kukuta utamaduni wa kuitukuza sana siku hiyo upo. Utaratibu huu wa kuikuza siku hiyo sijui umeanzia wapi.

Ukiangalia kwa umakini siku hiyo haina lolote jipya tofauti na siku nyingine za mwaka. Au shida ni namba ambayo mzungu aliipa siku hiyo?? Siku inakuzwa sana hii.

Imezoeleka kuonwa watu mbalimbali wakimsifu Mungu na wengine kulia kwa furaha, wengine wanalazimika hata kugharimika vitu ambavyo walikuwa hawafanyi siku zote yote hiyo ni ili kuonekana nao wapo katika msafara wa kufuata mkumbo ila yote hayo kisa tu wameweza kuiona siku inayofuata baada ya tarehe 31 disemba. Khaaaa! Huu ni upumbavu uliokubuhu. Hayo yanayofanyika tarehe hiyo yaendelezwe pia na siku zinazofuata italeta maana zaidi.
 
niutamaduni mkuu tulioukuta na ukatifanya tuamini hivyo tunavyoamini

yaani Kwa mfano unaamini Leo ni j3 hivyo nicku ya kazi, j2 cku yakupumzika
 
Ni mkumbo tu wa kumuabudu mungu wa kigiriki aitwae january bila wenyewe kutambua.

Sent from my DUB-LX1 using Tapatalk
 
Ni mkumbo tu wa kumuabudu mungu wa kigiriki aitwae january bila wenyewe kutambua.

Sent from my DUB-LX1 using Tapatalk
Tuacheni tuserebuke kwa kuvuka salama.
Kama siku zisingekuwa zinabadilika toka asubuhi kuwa mchana, mchana kuwa jioni, jioni kuwa usiku, usiku kuwa usiku wa manane na kisha alfajiri na kurejea asubuhi tena tusingejisumbua kushangilia mabadiliko maana yasingekuwepo. Sisi tunashangilia mabadiliko maana nilivyo mwaka huu sivyo nilivyokuwa mwaka jana na mwakani nitaendelea kubadilika kuelekea uzeeni zaidi.
Pia wengine wengi tumewaacha njiani ambao tumetoka nao Januari, huku niliko wako wengi lakini maarufu wapo kina Mengi, Mufuruki, Ruge nk. Hao wote wametangulia mbele za haki si kwamba walikuwa na dhambi kuliko mimi, la hasha. Yawezekana nawazidi katika maovu na wao wametenda mema kwa wengi kuliko Mimi. Lakini cha ajabu mbali ya uwezo wao kiuchumi unainizidi sana, magonjwa yao yameshindikana hadi nje ya nchi wakati Mimi kwa mwaka mzima sijatoka hata nje ya kijiji changu. Nikijisikia homa nanunua Panadol na ALU nakula maisha yanakwenda, nikivurugwa na tumbo nameza Flagyl au Erythromycine nadunda na njia. Kwa hayo majaliwa kwa nini nisimshangilie Mungu wangu hata hiyo Mara moja na kuifanya Siku hiyo moja kuwa tofauti na nyingine?
Siku kama siku haina tofauti na nyingine, lakini tumeifanya ya kipekee (Siyo ya tofauti) kwa sababu ya matendo makuu aliyotujalia Mungu kwa siku 365.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom