baluhya M.
Member
- Apr 22, 2011
- 33
- 79
Ndg wananchi leo hotuba yangu ya mwisho wa mwezi tofauti na miezi mingne itakuwa fupi sana, itahusu mambo mawili tu yaliyotikisa taifa katika huu mwezi unaoisha, nayo ni Kifo cha Daudi Mwangosi na Dr Swakala na sign 200 za kuombea msamaha.. Ndg wananchi Sitaki kuongea mengi juu ya kifo cha Daudi Mwangosi maana mengi yamesemwa, mimi leo nataka nitangaze tu kuanzia leo waziri wa mambo ya ndani Dr. Nchimbi, IGP- Mwema, RPC-kamuhanda, MSAJILI wa vyama vya Siasa- TENDWA nimewafukuza kazi na watatakiwa kukamatwa mara moja, nataka hili liwe fundisho kwa wateule wangu wanaojipendekeza kwangu kwa gharama yoyote ikiwemo kuua raia ambao nimeapa kuwalinda kwa mujibu wa katiba. Kuhusu nafasi zao, nitatangaza wiki ijayo watakao jaza nafasi hizo. Kuhusu Dr SWAKALA na kikundi chake cha watu 200 nimeagiza vyombo vinavyohusika kuwa kamata mara moja na hukumu yao nimeelekeza iwe kati ya kifungo cha maisha na kunyongwa, hili litakuwa fundisho kwa watanzania wote wanaoshiriki migomo halafu wanaishia kusingizia watu kwamba waliwashawishi. Kimsingi ndg wananchi haingii akilini mtu ugome karibu mara 4 ktk kipindi cha miezi 7 halafu uje uende habari maelezo kusema kuwa ulipotoshwa na MAT. Mwisho kabisa natangaza kuwasamehe madaktari wote waliosimamia Ukweli hadi mwisho wakiongozwa na Dr. ULIMBOKA, DR. Chitage, Dr. Godbles na Dr. Namala, hvyo madaktari wote ambao wako na Jumuiya madaktari ya Dr. Ulimboka, wanapaswa kuanza kuripoti katika vituo vyao vya kazi mapema iwezekanavyo. Leseni zao na malipo yao ya usumbufu yatawakuta hukohuko kazini. Nawaahidi kuwa serikali yangu imebaini madai yao yalikuwa ya msingi na yenye lengo la kuleta mapinduzi ya sekta ya afya,hvyo nitawapa ushirikiano wangu binafsi na wa serikali yangu katika kuhakikisha tunaleta mapinduzi ya kweli katika sekta ya Afya. Asanteni kwa kunisikiliza.