kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,252
- 16,171
Sina uhakikika kama viongozi wangu wakuu wa nchi wameitumia vema fursa hii ya kutembelewa na wageni mashuhuri kama Obama, Bush, Michelle Obama, Laura Bush, na Rais wa China. Nilichosikia mimi cha maana kutoka kwa Obama ni Umeme wa vijijini. Hivi ni wanavijiji wangapi wana nyumba na hela za kuvutia umeme majumbani mwao? Nijuavyo mimi asilimia 80 ya wanavijiji wanaishi kwenye nyumba za matembe, manyasi na makuti na wanahitaji chakula cha msaada kila mwaka, hivi huo umeme wataweza kuulipia kila mwezi kwa matumizi yao hata kama wakiunganishiwa bure?
Utahitaji nguzo na nyaya ndefu kiasi gani ili uwasambazie wanavijiji waliotawanyika huku na kule mashambani mwao? Nadhani mimi gharama za kuufikisha umeme vijijinj haitalingana na manufaa watakayopata wanavijiji walio wengi. Angekuwa mimi Rais wa Tanzania badala ya umeme, ningemwambia Rais Obama atusaidie au atukopeshe:
1. Meli kubwa za kisasa za uvuvi kama ile meli ya Magufuli angalau 5 tu ili tukavue wenyewe samaki baharini,
2. Watalaam wa sheria za mikataba angalau 5 tu ili watusaidie katika kutoa mafunzo kwa wanasheria na viongozi wetu namna yaku-negotiate katika kuingia mikataba na wawekezaji,
3. Ningemuomba msaada/mkopo wa technologia ya kupambana na wakwepa kodi nchini ili kuwafanya watu wote wanaostahili kulipa kodi walipe,
4. Ningemuomba msaada/mkopo wa kuweza kuvitangaza vivutio vyetu vya utalii kupitia vyombo vya habari vya Marekani (CNN, ABC, VOA, n.k), Ulaya (BBC, skynews, n.k) na China ili kuongeza watalii nchini.
5. Ningemuomba msaada wa kusomesha vijana wetu kwenye maeneo muhimu ya kimkakati kama madini, uvuvi mkubwa, utalii, kilimo na ufugaji.
Faida itakayopatikana kutoka maeneo haya tuliyoombea msaada/mkopo ndio ingetumika katika kusambaza umeme kwa wananchi, na kujenga barabara na kuzihudumia. Vinginevyo tumeliwa tu ..
Utahitaji nguzo na nyaya ndefu kiasi gani ili uwasambazie wanavijiji waliotawanyika huku na kule mashambani mwao? Nadhani mimi gharama za kuufikisha umeme vijijinj haitalingana na manufaa watakayopata wanavijiji walio wengi. Angekuwa mimi Rais wa Tanzania badala ya umeme, ningemwambia Rais Obama atusaidie au atukopeshe:
1. Meli kubwa za kisasa za uvuvi kama ile meli ya Magufuli angalau 5 tu ili tukavue wenyewe samaki baharini,
2. Watalaam wa sheria za mikataba angalau 5 tu ili watusaidie katika kutoa mafunzo kwa wanasheria na viongozi wetu namna yaku-negotiate katika kuingia mikataba na wawekezaji,
3. Ningemuomba msaada/mkopo wa technologia ya kupambana na wakwepa kodi nchini ili kuwafanya watu wote wanaostahili kulipa kodi walipe,
4. Ningemuomba msaada/mkopo wa kuweza kuvitangaza vivutio vyetu vya utalii kupitia vyombo vya habari vya Marekani (CNN, ABC, VOA, n.k), Ulaya (BBC, skynews, n.k) na China ili kuongeza watalii nchini.
5. Ningemuomba msaada wa kusomesha vijana wetu kwenye maeneo muhimu ya kimkakati kama madini, uvuvi mkubwa, utalii, kilimo na ufugaji.
Faida itakayopatikana kutoka maeneo haya tuliyoombea msaada/mkopo ndio ingetumika katika kusambaza umeme kwa wananchi, na kujenga barabara na kuzihudumia. Vinginevyo tumeliwa tu ..