Ninashauri Mkutano wa CHADEMA Dar es Salaam usifanyike Jumatatu

Ninashauri Mkutano wa CHADEMA Dar es Salaam usifanyike Jumatatu

tufe

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2015
Posts
750
Reaction score
290
Habari wakuu,

Wakuu kama munavyofahamu kwamba chama makini,chama cha watanzania CHADEMA kimepanga kufanya mkutano mkubwa wa had hara katika jiji la Dar es salaam siku ya Jumatatu.

Ila mimi mpenda mabadiliko asieyumba ninapenda kuwashauri viongozi Wangu wakuu kwamba ni heri wangesitisha huu mkutano kwa sasa mpaka pale zoezi la uandikishaji kwa BVR litakapomalizika kwasababu kama tunavyojuwa mikutano ya CHADEMA inavuta watu wengi hususani vijana kwasababu ya hamasa na mapenzi yao kwa chama hiki.

Kitendo vijana kuhudhuria mkutanoni kitapelekea vijana wengi kukosa kujiandikisha kwa siku ya Jumatatu na pia kutoa nafasi kwa magamba(CCM) kuandikisha watu wao bila ya usumbufu na kwa faragha kabisa.

Tusije tukashangaa siku hiyo mashine tuliozoea kuandikisha watu 50 kwa siku ikaja kuandikisha watu 1000 kwa siku sababu wanajua wapo peke yao.

Hivyo basi ninaomba chadema kuendelea na mikutano yake katika mikoa ya MBEYA na ARUSHA pamoja na mikoa mengine ambayo uandikishaji umeshapita mwisho kuja kufanya Dar baada ya zoezi la uandikishaji kumalizika.

Naomba kuwasilisha.
 
Siku hiyo ni siku maalum kabisa kwa ajili ya kubadilisha uelekeo wa siasa za Tanzania.... Kuna jambo kubwa sana litatokea Jumapili, hivyo Jumatatu ni mapokezi ya karne....

Vile vile mkutano huo unaweza kuwa njia nzuri ya kuwahamasisha vijana kujiandikisha kwa kasi kuanzia jumanne mpaka tarehe 2
 
Ocampo four umenena vemaa Lakin pia mtoa mada yuko sawa..tukubali chochote ilimrado watu ASA vijana tujindikishe mpk Siku ya mwisho
 
Huu mkutano ni nani aliyewapa kibali atafutwe haraka sana?
 
Jambo gani muhimu litakalotokea siku ya j2?
 
tufe naunga mkono hoja 1000%!

Umeona mkuu eeee! Hata hizo BVR zinazogandaganda ni kwasababu ya hofu ya MAFURIKO(wapinzani) siku wakipata nafasi tu Mara unasikia wameandikishwa watu 50,000 kwa siku moja katika jimbo la UBUNGO.
 
Siku hiyo ni siku maalum kabisa kwa ajili ya kubadilisha uelekeo wa siasa za Tanzania.... Kuna jambo kubwa sana litatokea Jumapili, hivyo Jumatatu ni mapokezi ya karne....

Vile vile mkutano huo unaweza kuwa njia nzuri ya kuwahamasisha vijana kujiandikisha kwa kasi kuanzia jumanne mpaka tarehe 2


Nimekuja kugundua wewe pekee yako ndiye ulikuwa credible kwa EL humu JF..

Wengine wote walikuwa waganga njaa tu..
 
Nimekuja kugundua wewe pekee yako ndiye ulikuwa credible kwa EL humu JF..

Wengine wote walikuwa waganga njaa tu..

Huyo occampo four ni "HB" hivyo lazima aendelee kuwa credible kwa EL milele japo yeye anagombea kupitia ccm
 
Siku hiyo ni siku maalum kabisa kwa ajili ya kubadilisha uelekeo wa siasa za Tanzania.... Kuna jambo kubwa sana litatokea Jumapili, hivyo Jumatatu ni mapokezi ya karne....

Vile vile mkutano huo unaweza kuwa njia nzuri ya kuwahamasisha vijana kujiandikisha kwa kasi kuanzia jumanne mpaka tarehe 2
Lowassa anapokelewa!
 
Siku hiyo ni siku maalum kabisa kwa ajili ya kubadilisha uelekeo wa siasa za Tanzania.... Kuna jambo kubwa sana litatokea Jumapili, hivyo Jumatatu ni mapokezi ya karne....

Vile vile mkutano huo unaweza kuwa njia nzuri ya kuwahamasisha vijana kujiandikisha kwa kasi kuanzia jumanne mpaka tarehe 2

Ocampo four umenena vemaa Lakin pia mtoa mada yuko sawa..tukubali chochote ilimrado watu ASA vijana tujindikishe mpk Siku ya mwisho

Nilijua tu wahanga wa maamuzi sahihi ya kitengo lazima waje kwa pupa! Ila mtanyooka tu, si mnamuona nduguyenu Bashe?
 
Huyo occampo four ni "HB" hivyo lazima aendelee kuwa credible kwa EL milele japo yeye anagombea kupitia ccm

Una maana ni HB ya zile penseli,HB ya Head Boy au HB ya Hussein Bolt wa Nzega,wanaesema ana udugu na Omary Bashir??!!

cc ocampo four

Mkuu mwaga japo harufu basi ya pilau la j2!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom