Ninashangaa sana wananchi wakiwemo wasomi kwa jinsi wanavyomlaani CAG

kibaravumba

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
6,635
7,005
Niliwahi kushangaa wakati fulani kuona mama mmoja anajiita "mfalme zumaridi" anawafuasi wengi kiasi kwamba unaweza kujiuliza jinsi akili za binadamu zilivyo dhaifu na kuna watu wanaweza kuzifanya vyovyote wanavyotaka.

Hata hivyo nikakumbuka mtu mmoja aliitwa Kibwetere jinsi alivyowarubuni watu kule Uganda hadi akauunguza moto katika hekalu lake wao wakiwa wanasubiri kuja kwa Yesu.

Kama haitoshi nikakumbuka yale makundi ya kigaidi yanayofanganya watu wa mrengo wa dini fulani kuwa yanampigania Mungu wao kwa njia ya kuchinja binadamu waliowatambua kama makafiri.

Sijui kwanini leo ninawashangaa wasomi wengi (kama kweli ni wasomi au wahitimu sijui) wanahoji tena kwa hasira na chuki eti ni kwa nini CAG anayasema haya wakati mwenda zake hayupo! Wanafikia mahali pa kusema mwenda zake amesalitiwa kisa ukweli wa kuwa ATCL inajiendesha kwa hasara.

Hivi kumbe inawezekana kuwafanya hata waliohitimu digrii kuwafanya wasiweze kufikiri vizuri?

Kweli ubinadamu ni kazi sana, ndio maana hata Mungu aliwanyooshea mikono binadamu.
 
Hao wasomi wanashangaa kwa sababu CAG amejikita kwenye kazi moja tu ya UKAGUZI na kusahau kazi nyingine ya UDHIBITI, Kama angelikagua na kudhihiti tusingelifikia hatua ya kila sehemu pesa kuonekana zimepigwa.

Pia wasomi wanashangaa kwanini enzi za Hayati Magufuli hakuwa mkweli bali alijawa uongo na unafiki, mshangao wao ni woga wake wa kushindwa kutimiza majukumu yake ipasavyo kama mtangulizi wako Prf Assad bali alinyamaza kimya, hivyo hali hii imeimua mshangao mkubwa wa CAG kujimwambafai baada ya mzee kuondoka anaanza kutema nyongo zake.

Viongozi ambao mnakabidhiwa nafasi mbali mbali kama mnataka watanzania na wasomi wasiendelee kuwashangaa punguzeni unafiki na woga, ni heri ukasema ukweli angali mhusika akiwa hai kwa manufaa ya umma kwani nafasi hizo ni dhamana, leo kwako kesho kwangu,timiza wajibu wako utakumbukwa licha ya changamoto utakazokumbana nazo.
 
Hata kama walihisi kuna siku yatajulikana ila sio gafla hivi manake hawakudhani kuna siku wangeachwa gafla na mambo yao yote kuwa hadharani.

Wananchi tuko gado tu.
 
Kama na wewe ni msomi au muhitimu, na una mshangaa CAG, nina kila sababu ya kusema tunamuhitaji mkoloni atutawale tena,maana licha ya watu kuwa na elimu kubwa, bado tuna ujinga wa mtu aliyerogwa.

Wasomi wanajua kwa mamlaka aliyonayo Rais kwa mujibu wa katiba, anaweza kujigeuza kuwa mungu. Ni nani anaweza kupingana na mungu kama mlivyotaka iwe?

Kuna mtu angeweza kumkosoa mwendazake hata hata kwa siri halafu akabaki salama?

Kama kweli mmesoma, jitafakarini sana
Hao wasomi wanashangaa kwa sababu CAG amejikita kwenye kazi moja tu ya UKAGUZI na kusahau kazi nyingine ya UDHIBITI, Kama angelikagua na kudhihiti tusingelifikia hatua ya kila sehemu pesa kuonekana zimepigwa.

Pia wasomi wanashangaa kwanini enzi za Hayati Magufuli hakuwa mkweli bali alijawa uongo na unafiki, mshangao wao ni woga wake wa kushindwa kutimiza majukumu yake ipasavyo kama mtangulizi wako Prf Assad bali alinyamaza kimya, hivyo hali hii imeimua mshangao mkubwa wa CAG kujimwambafai baada ya mzee kuondoka anaanza kutema nyongo zake.

Viongozi ambao mnakabidhiwa nafasi mbali mbali kama mnataka watanzania na wasomi wasiendelee kuwashangaa punguzeni unafiki na woga, ni heri ukasema ukweli angali mhusika akiwa hai kwa manufaa ya umma kwani nafasi hizo ni dhamana, leo kwako kesho kwangu,timiza wajibu wako utakumbukwa licha ya changamoto utakazokumbana nazo.
 
Yanasemwa sasa kwa sababu Bwana Mkubwa hakutaka yasemwe. Hakuna kitu kibaya kama kuficha ukweli ila nasi tuliaminishwa vile vya uongo kuwa ndo ukweli na ndio maana watu wanashangaa.

Lakini wangepata japo wasaa wa kuyasikia ya Prof Assad na wabunge wa vyama mbadala nina uhakika wasengekua wanashangaa haya.
 
Hao wasomi wanashangaa kwa sababu CAG amejikita kwenye kazi moja tu ya UKAGUZI na kusahau kazi nyingine ya UDHIBITI, Kama angelikagua na kudhihiti tusingelifikia hatua ya kila sehemu pesa kuonekana zimepigwa.

Pia wasomi wanashangaa kwanini enzi za Hayati Magufuli hakuwa mkweli bali alijawa uongo na unafiki, mshangao wao ni woga wake wa kushindwa kutimiza majukumu yake ipasavyo kama mtangulizi wako Prf Assad bali alinyamaza kimya, hivyo hali hii imeimua mshangao mkubwa wa CAG kujimwambafai baada ya mzee kuondoka anaanza kutema nyongo zake.

Viongozi ambao mnakabidhiwa nafasi mbali mbali kama mnataka watanzania na wasomi wasiendelee kuwashangaa punguzeni unafiki na woga, ni heri ukasema ukweli angali mhusika akiwa hai kwa manufaa ya umma kwani nafasi hizo ni dhamana, leo kwako kesho kwangu,timiza wajibu wako utakumbukwa licha ya changamoto utakazokumbana nazo.
CAG angeanikaje uozo wa aliyemteua? Hivi kibinadamu tu, unanzaje kuukata mkono unaokulisha?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom