Ninajihisi aibu sana kwa kumtaka kimapenzi huyu binti wa mama akaamua kunikataa na matusi juu

Melki the Storyteller

JF-Expert Member
May 3, 2022
5,700
9,778
Nahisi mu buheri wa afya wapendwa,

Ni binti wa kazi wa ndani wa ma mdogo wa kufikia ambaye yeye na huyu mama wana historia ya kutoka kijiji kimoja tena majirani huko nyumbani kwao kijijini

Tukianza tu na sifa za binti huyu. Si msiri na hakuna kitu kawahi kuficha

Mwaka mmoja na miezi kama minne hivi iliyopita, niliingia rasmi kwenye jiji hili kutoka mkoa X kwa lengo la kibiashara zaidi. Hivyo nilifikia kwa huyu bi mkubwa, baada ya kama wiki mbili nikapata chumba cha kupanga jirani na nyumba ya bi mkubwa. Hivyo kuwaona kila siku jioni nilipokuwa natoka kwenye mihangaiko yangu ikawa kawaida yangu.

Siku moja niliwahi kutana na tifutifu pale kwake, kuna kijana mmoja ambaye ni msaidizi wa bi mkubwa katika mambo ya kiofisi alikuwa akitukanwa matusi mazito huku akitupiwa mabegi yake nje mithili ya mbwa koko anayeelekea kupoteza makazi.

Baada ya kufika kwenye tukio nilijaribu kuzungumza na huyo kijana akawa kaniambia kuwa yeye na binti huwa wana mazoea, tena kwa jinsi yeye alivyodhania ni kuwa ni mazoea ya kimapenzi. Lakini mida ya saa kumi na moja wakati akirejea kutoka kazini, alimkuta binti yuko mwenyewe nyumbani, katika harakati za kujaribu bahati yake, binti akagoma kabisa kumtunuku jamaa.

Baada ya bi mkubwa kuwasili nyumbani jioni ile, taarifa iliyokuwepo ni kuwa binti eti alitaka kubakwa. Na hicho kikawa chanzo cha kijana kupoteza 350k kwa mwezi. Kuna kijana mmoja aliwahi kabidhiwa bodaboda na bi mkubwa ya mkataba, kwa kuwa aliona kuwa nina mazoea na huyo binti aliamua kuniuliza kama ni ndugu yangu au lah!

Nikamweleza kuwa huyo ni ndugu tu na baada ya hapo nikamfanyia mpango wa namba ili amalize yeye. Kweli bhana, kijana alikuwa si haba, akam-sound-isha binti, binti akaingia kwenye line, mahusiano yao yakaanza, akawa ni mtu wa kumletea vijizawadi kama viatu, nguo, simu n.k, lakini mwisho wa siku kijana ali give up kutokana na kuwa ule utelezi aliokuwa akiutegemea hakuweza kuupata.

Baada ya siku kadhaa mbeleni yule kijana alinyang'anywa pikipiki, kwa maelezo yake alisema kuwa yule binti yuko nyuma ya pazia. Baada ya miezi kadhaa, niliuza nyumba yangu iliyoko mkoani nikapata pesa za kuamsha jumba la uongo na ukweli hapa DSM, nikabeba msalaba wangu, Mwa Jay mke wangu na wanangu wawili tukahamia rasmi huku, hapo ndipo nikapunguza mawasiliano na bi mkubwa, japo namba ya huyu binti nilikuwa nayo.

Huyu binti akawa ni mtu wa kunijulia hali kila muda, ikabidi hata simu yangu niiwekee 'app' ya kuficha simu na ujumbe za mtu husika. Nilivyoona kama anaelekea elekea nikasema si vyema nionje kinyama hicho. Miadi tuliyopanga alikubali, japokuwa nilipomtengenezea mazingira ya gesti alikwepa.

Siku ya jana nikapata wasaa wa kumtembelea bi Mkubwa kwake nyakati za jioni mida ya saa 11. Baada ya kufika pale nikamkuta akiwa peke yake na khanga tu. Nikaona niitumie hii nafasi vyema kufaidi tunda la mti wa katikati, tunda la ujuzi wa mema na mabaya.

Si unajua tena wanawake wetu wa Kitanzania wanavyoanza na zile za sitaki nataka! Nikajua ndio ameanza na intro ya staki kwanza, kumbe mtu anamaanisha bhana! Katika kujaribu kufosi fosi hapa na pale nilijikuta nimechakazwa vibaya sana, nimechapika sio poa hadi sikuamini.

Nilijikuta na alama za kucha na michirizi shingoni, mashimo mashimo ambayo sielewi hata alitumia nini kuyatengeneza, korodani moja inauma, leo asubuhi nakuta jicho la kushoto limeumuka, kidole cha mwisho cha mkono wa kushoto kinauma, kichwani nahisi kuna minyoo tegu ina tembea mwilini, yaani hata sielewi.

Baada ya hiyo vita kuisha, nilimsikia akitamka kwa sauti kama ya mzee aliyelewa hivi, "Naomba tuheshimiane". Nilijikuta natetema kama Mayele pasipo kumtazama machoni, kiaibu fulani hivi cha uchungu kikinizonga. Muda huo najiuliza nikifika nyumbani nimueleze vipi Mwa J, shati linanukia 'deodorant', dah!

Leo asubuhi wakati nafufuka nimekutana na 'missed calls 4' kutoka kwa bi mkubwa na ka ujumbe kamoja kanakosomeka "Wewe"!

Najutia sana wakulungwa, yule wa bodaboda aliwahi sema kuwa huyu binti bado ana bikra yake (miaka 21), ila sidhani kama hicho ni kigezo cha usumbufu wote huu.

Sijui cha kufanya kwa sasa, naombeni tu mnitie moyo!

images%20(2).jpg
 
Hapana mkuu, kuhusu namna gani naweza kuondokana na aibu hii, yaani kwanza najiona mnyonge kwa kuonesha udhaifu wangu mbele ya hicho kibinti
Nyege mshindo mbaya sana.

Pole mkuu.
Binafsi kama mwanamke yupo karibu na mimi na najua kua sio msiri aisee huyo namwogopa kam ukoma hachelewei kukuchomesha huyo.

Hata ukifanikiwa kufanya yako, atakutangazia mbofu tu.

Pole na usirudie
 
Back
Top Bottom