Ninaipenda Mno CCM Kuliko Nchi Yangu!

Ninaipenda Mno CCM Kuliko Nchi Yangu!

TEKNOLOJIA

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2014
Posts
4,305
Reaction score
2,563
Kuna wanaCCM ambao wapo radhi kuipigania CCM yao vyovyote vile wawezavyo,hata ikibidi kuyaweka maslahi ya nchi pembeni watafanya hivyo.Tumeona kashfa nyingi za ufisadi zilizoiandama serikali ya CCM na jinsi wanaCCM walivyosimama kidete kukitetea chama chao.Wamefikia hatua ya kuwanadi Kwenye mitandao ya kijamii baadhi ya wahusika wa ufisadi kugombea kuongoza ofisi kubwa kabisa hapa Tanzania ya urais.

Hizi ndizo aina ya siasa tunazozihitaji hapa Tanzania?
 
Sasa huju Jf unamwambia nani,siuende kwenye msiba ili wakupe kurithi nafasi ya mzee wa msituni
 
Mkuu CCM inazindika wafuasi wao kwa namna mbalimbali , ukitaka kujua ukweli kula vyakula vinavyoandaliwa kwenye mikutano ya CCM kama hujageuka kondoo bin zuzu. Kwa nini hujiulizi mbona ALBINO wanamalizwa wakati wa uchaguzi , nani kama si wana CCM ana uwezo wa kununua albino kwa gharama hiyo inayotajwa !!?
 
wasisahau hata Lowasa alikuwa mmoja wa wao lakini sasa ameona matokeo yake
 
Nchi kwanza vyama mwisho.Nchi itadumu lakini vyama vitaishia recycle bins
 
Kuna wanaCCM ambao wapo radhi kuipigania CCM yao vyovyote vile wawezavyo,hata ikibidi kuyaweka maslahi ya nchi pembeni watafanya hivyo.Tumeona kashfa nyingi za ufisadi zilizoiandama serikali ya CCM na jinsi wanaCCM walivyosimama kidete kukitetea chama chao.Wamefikia hatua ya kuwanadi Kwenye mitandao ya kijamii baadhi ya wahusika wa ufisadi kugombea kuongoza ofisi kubwa kabisa hapa Tanzania ya urais.

Hizi ndizo aina ya siasa tunazozihitaji hapa Tanzania?

Unachonena ni UKWELI unaouma,tuka tayari kumpa UONGOZI,mtu ambaye ni FISADI na Mlarushwa mkubwa sababu tu anawakilisha chama chetu cha kijani.

Sina uhakika kama ni yale MAPAMBIO ya risala za Mwalimu Nyerere ya kwamba bila CCM nchi itayumba huwa sielewi.Sina uhakika kama Mwalimu huyu alikuwa anamaana ya BILA RUSHWA NCHI ITAYUMBA au BILA MADAWA ya KULEVYA NCHI ITAYUMBA? pia sielewi na sipati jibu la kujiridhisha na kuwaambia kesho wajukuu zangu.

Na ndiyo maana wakiita mkutano au kampeni yoyote basi utasikia tumuenzi Mwalimu kwamba bila RAIS kutoka CCM nchi itayumba,sipati jibu maana hata walarushwa nao ni VIONGOZI wakuu ndani ya CCM.

Napata wasiwasi sana kujua huyu Mwalimu JK alikuwa anamaanisha nini?Maana aliiacha CCM ikiendelea kupalilia rushwa kubwa na kuamua hata kuuza raslimali zetu kwa bei ya kutupwa ilimradi VIONGOZI wapate sehemu ya asilimia kumi ya mauzo ya raslimali hizi.
 
Nchi kwanza vyama mwisho.Nchi itadumu lakini vyama vitaishia recycle bins

Kwako kaka lakini kwa siye wanaCCM ni CHAMA kwanza TAIFA baadaye.Tena usithubutu kuongea utatukanwa mpaka utamani ukuta ukubomokee..........:A S embarassed::A S embarassed:
 
wajingaaa wengi wamesema neno hilo la kupenda chama zaidi kuliko nchi ahahahah
 
Mkuu Tetty nadhani Mwalimu Alisema bila CCM madhubuti Nchi itayumba lkn pia akasikika akisema CCM si mama yake........akimaanisha kwa lolote litakalokwenda nje ya katiba yao Basi anaweza kuondoka...........kuna Taarifa nyingi kuwa walimuondoa yye kabla hajaamua kuondoka kwa hiari.......Mwalimu angalikuwa hai Leo asingalibaki Ndani ya CCM.
 
hoja yako ni hoja ya msingi sana lakini bila kujua tatizo huwezi kutatua tatizo bali unaweza kudhani unatatua kumbe unahamisha tatizo.

kuna msemo unasema wajinga ndio waliwao, kwa maana kama vyama vinafanya upuuzi ni wananchi wajinga tu ndio wanaweza kufanyiwa upuuzi.

vyama vya wasiasa ni makundi ya wananchi waliojiunga pamoja na kuwakeka malengo ya pamoja jinsi ya kuongoza nchi.

kwa nchi yenye wananchi werevu chama kukumbatia wajinga kupeperusha bendera yake ni sawa na kujinyonga kwa kujitia kitanzi.

lakini lipo tatizo pia la watu kuja wakipiga kelele kuonyesha makosa ya hawa lakini wananchi wakiwaangalia wanaona hata wanaopiga kelele ni wabaya zaidi.

uozo wa chama kinachoweza kuwa madarakani ni mtaji kwa vyama vingine kuweza kupewa nafasi lakini si mtaji kwa kupiga kelele tu bali kutengeneza mifumo na kanuni ambazo wananchi wakikiangalia chama wanaona ni mkombozi.

hivyo wapinzani wasidhani wananchi wanafurahi yale wanayoyalalamikia bali kama hawajapewa nafasi kushika hatamu watambue yawezekana wanapiga kelele lakini wananchi wakivitathmini vyama hivi wanaona kabisa kuwa may be nothing good can come out of them.

wajipange waweke mifumo mizuri na sera nzuri ndio waanze kupiga kelele kuwa mnaona hili lakini tatizo hili limetokana na haya na haya na sisi tutatatua hivi.

Kuna wanaCCM ambao wapo radhi kuipigania CCM yao vyovyote vile wawezavyo,hata ikibidi kuyaweka maslahi ya nchi pembeni watafanya hivyo.Tumeona kashfa nyingi za ufisadi zilizoiandama serikali ya CCM na jinsi wanaCCM walivyosimama kidete kukitetea chama chao.Wamefikia hatua ya kuwanadi Kwenye mitandao ya kijamii baadhi ya wahusika wa ufisadi kugombea kuongoza ofisi kubwa kabisa hapa Tanzania ya urais.

Hizi ndizo aina ya siasa tunazozihitaji hapa Tanzania?
 
Kuna wanaCCM ambao wapo radhi kuipigania CCM yao vyovyote vile wawezavyo,hata ikibidi kuyaweka maslahi ya nchi pembeni watafanya hivyo.Tumeona kashfa nyingi za ufisadi zilizoiandama serikali ya CCM na jinsi wanaCCM walivyosimama kidete kukitetea chama chao.Wamefikia hatua ya kuwanadi Kwenye mitandao ya kijamii baadhi ya wahusika wa ufisadi kugombea kuongoza ofisi kubwa kabisa hapa Tanzania ya urais.

Hizi ndizo aina ya siasa tunazozihitaji hapa Tanzania?

Naona siku hizi mpo kwa maslahi ya chama sio wananchi makabwela na sie tunasema hivi tuko na wale wenye maslahi na sisi wananchi na sio chama upo hapo?
 
HAPANAAA!!!!

KWA HILI LA KUPENDA CHAMA KULIKO NCHI UMEJIONDOA AKILI.

Haivumiliki huo ni ujuha na wendawazimu,kwetu sisi wenye AKILI TIMAMU,AKILI NZURI KIPAUMBELE NI KUPENDA NCHI YETU TANZANIA KWANZA VYAO BAADAYE.
 
Kuna wanaCCM ambao wapo radhi kuipigania CCM yao vyovyote vile wawezavyo,hata ikibidi kuyaweka maslahi ya nchi pembeni watafanya hivyo.Tumeona kashfa nyingi za ufisadi zilizoiandama serikali ya CCM na jinsi wanaCCM walivyosimama kidete kukitetea chama chao.Wamefikia hatua ya kuwanadi Kwenye mitandao ya kijamii baadhi ya wahusika wa ufisadi kugombea kuongoza ofisi kubwa kabisa hapa Tanzania ya urais.

Hizi ndizo aina ya siasa tunazozihitaji hapa Tanzania?
Ni hivi , ccm inalipa kuliko Tanzania , huyu hakwenda Tanzania lakini kaenda ccm , si unaona ?
 

Attachments

  • attachment-8.jpeg
    attachment-8.jpeg
    9.3 KB · Views: 429
Back
Top Bottom