planexboi
Member
- Aug 5, 2021
- 45
- 227
Natumaini mko poa
Nina miaka 24 sasa.nilitoka nyumbani nikiwa ni miaka 22 na kuamua kujitegemea ,niliondoka nyumbani nikiwa na elfu 50 mfukoni nikaenda geita kutafuta maisha.
Sikuwa na ndugu yeyote ,sikuwa na kazi maalum ya kufanya kwa hyo kiasi nilichokuwa napata kiliishia tu kwenye chakula,
Baada ya ugumu wa maisha kuzidi niliamua kuingia machimboni eneo la rwamgasa-KATORO,nimekaa huko pesa nilizokuwa napata ilikuw kidogo sana ,
Sasa mwezi uliopita nimebahatisha kupata millioni 1 na laki 2 baada ya kuuza dhahabu,nimelipa lipa madeni ya watu nimebakiwa na laki 9 nimeziweka MPESA, huku machimboni kugumu sana hasa kama hauna mtaji wa kutosha.
Nimeamua nitoke ili hata hiki nilichokipata kisitekee chote.naombeni ushauri nimefika leo nipo katoro mjini ,nifanye biashara gani ambayo ntakuwa napata elfu 15 kwa siku.
Nahitaji michango yenu ya mawazo wakuu.
Nina miaka 24 sasa.nilitoka nyumbani nikiwa ni miaka 22 na kuamua kujitegemea ,niliondoka nyumbani nikiwa na elfu 50 mfukoni nikaenda geita kutafuta maisha.
Sikuwa na ndugu yeyote ,sikuwa na kazi maalum ya kufanya kwa hyo kiasi nilichokuwa napata kiliishia tu kwenye chakula,
Baada ya ugumu wa maisha kuzidi niliamua kuingia machimboni eneo la rwamgasa-KATORO,nimekaa huko pesa nilizokuwa napata ilikuw kidogo sana ,
Sasa mwezi uliopita nimebahatisha kupata millioni 1 na laki 2 baada ya kuuza dhahabu,nimelipa lipa madeni ya watu nimebakiwa na laki 9 nimeziweka MPESA, huku machimboni kugumu sana hasa kama hauna mtaji wa kutosha.
Nimeamua nitoke ili hata hiki nilichokipata kisitekee chote.naombeni ushauri nimefika leo nipo katoro mjini ,nifanye biashara gani ambayo ntakuwa napata elfu 15 kwa siku.
Nahitaji michango yenu ya mawazo wakuu.