Kinyengeli
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 452
- 143
mwambie hivi weekend hii tutakuja kula kwako so akae huko apike na mle huko kwake, ha watu hawa wanachosha sana, mi ilikuwa ni ndugu yangu kabisa mtoto wa cousin wangu, alikuja kwangu kutembea akakaa miezi miwili, kisha akapata kazi akiwa kwangu, akaendelea kukaa miezi minne ila ndo hivyo hela yake yake peke yake hanunui hata sabuni ya kufulia nguo zake, na siku nilichelewa kuacha pesa ya mahitaji ndani lol mwenyewe akaenda kula hotelini halafu bint yangu wa kazi akashinda njaa mpka saa kumi nilipoludi,nikaona isiwe tabu nikamtafutia nyumba mbali kabisa na ninakoishi ila karibu na kituo chake cha kazi, nikamwambia nimekutafutia nyumba na nimelipia miezi minne so utakawa uhamie huko hapa si unaona tunabanana, alikubli ki shingo upande tu, akahama, eh akanishangaza tena kila siku jioni anakuja kula home yaani kwake hapiki, nilivyoona kumbe hataki kunua vyombo, nikamwambia week end moja tutaenda kula kwake, basi akanunua vyombo na akapika, since then anajipikia mwenewe na ameshazoea kujitegemea.
Mimi ni mwanamke mwenye familia. Ndoa yetu ni changa bado. Hivi karibuni nilipata simu kutoka kwa mfanyakazi mwenzangu alieniomba nimsaidie kukaa na mdogo wake kwa siku tatu ili atafute chumba baada ya hapo angeondoka. Cha ajabu yule mtoto alikaa kwa wiki tatu akidai chumba hajapata ingawa haikua kweli vyumba vilikuepo ila yeye alitaka aendelee kukaa hapa kwangu. Nikamvumilia hadi alipoamua kuondoka na hajaenda kukaa mbali na hapa kwangu. Kilichonikera ni jinsi anavyokuja nyumbani kila mara hasa mida ya menu. Najua dada yake anampa hela ila yeye ananunulia viwalo kama mjuavyo wanachuo akitegemea kuangushia kwa mama Beata. Isitoshe mimi nina bajeti zangu nyumbani kwangu akishakuja yeye kila kitu kinaharibika. Mboga niliopanga iwe ya mchana na jioni itaishia mchana. Kingine akitaka kufua nguo, kuoga anakuja hapa kwangu kitu ambacho naona atanivunjia hata ndoa yangu maana huyu sio ndugu na hashindwi kufanya lolote na mume wangu. Hivi kweli kanikera. Naomba mnipe jibu zuri la kumwambia huyu mtoto asiizoee nyumba yangu mimi nilimkaribisha kwa heshima ya dada yake ila naona mazoea yamezidi wema wangu utaniponza. Mnisaidie wadau. Wasalaam, mama Beata
mmmh maman beata hata sijui nianzie wapi,
wengi tunakutana na hayo mambo, sio kwa watu baki tu lakini hata kwa ndugu,
ushauri wangu mimi muangalie na tabia yake kwanza kama ni nzuri, halafu mchukulie kama ndugu japo si ndugu
kama ana tabia nzuri sio mbaya akija mara moja moja, atakusaidia espcially kukupatia habari za wadad wa kazi ambao kwa kweli ni majanga
pia anaweza kukusaidia kazi mabali mabli za nyumbani...anapokula mpangi nza kazi kadhaa za kufanya, mfano akija kufua mpe na nguo zenu afue, aoshe vyombo, apike n.k ilimradi mshughulishe...akiona mwenyewe kazi zimemzonga atakata miguu kuja hapo..
siamini kama kweli chakula cha mtu mmoja ni bg issue sana, naaamini chakula cha watu 3 kinatosha wanne...n.k..
mimi kwangu chakula sio issue kama huyo mtu hana tabia mbaya...tatizo ni tabia, wengine utakuta anakukosanisha na wadada wa kazi au anakusema vibaya, au hasaidii kazi yoyote hapo nyumbani..hapo sawa unamuondoa..
nafikiri ungelichukulia in postive way kuliko negative..halafu huyo ni km mdogo wako unatakiwa umkalishe chini umfundishe hasa kama anachzea hela,
sio mbaya kumsaidia mwanafunzi, mdog wa rafiki yako esp kitu km chakula mi naona very minor issue..
kiukweli mi yaani uchoyo uchoyo wa ugali sinaga kabisaaa....tutakula hicho hicho kilichopo hata km ni dagaa...ila akiniboa kwa matabia yake hapo namuondoa ila chakula tu aleeeeee mpk ashibe
huyo mtu mmoja kila siku Sista? Tena anataka kulala tu asimsaidie msichana wangu wa kazi? Yani humu ndani tumekua wenye nyumba wawili. Kinachonikera hataki mapishi nayoagiza mimi. Mfano chai huwa napenda iweke tea masala anamwambia dada usiweke bwana mi sipendi. Wali tumezoea kuweka iliki ye anasema ya nn usiweke. Mi mtu wa kunipangia maisha yangu kwenye nyumba yangu simtaki hata ukisema mi mchoyo.
Jamani kwa nn wanawake wanaongoza kwa roho mbaya!?? Just ugali only unaleta JF!!? Mara ooo atanichukulia mume wangu hujiamini? Hayo umeamua kuongezea tu bt da major issue ni ugali (mavi), yaani ww ukikabidhiwa mtoto ambae huna undugu ndani ya mwezi waweza mlisha sumu ili asikuharibie budget Lol! Wa unga robo na nyanya chungu utawajua tu, NB: safisha ndani ya kikombe kabla ya kusafisha nje ya kikombe. Nalog off
Jamani kwa nn wanawake wanaongoza kwa roho mbaya!?? Just ugali only unaleta JF!!? Mara ooo atanichukulia mume wangu hujiamini? Hayo umeamua kuongezea tu bt da major issue ni ugali (mavi), yaani ww ukikabidhiwa mtoto ambae huna undugu ndani ya mwezi waweza mlisha sumu ili asikuharibie budget Lol! Wa unga robo na nyanya chungu utawajua tu, NB: safisha ndani ya kikombe kabla ya kusafisha nje ya kikombe. Nalog off
Ngoja nikupashe upashike mtoto wa kike, kwa taarifa yako wa unga robo na nyanya chungu ni wakarimu mno kwenye chakula kuliko hao wa mboga Saba. Uswazini wana maisha ya taabu na dhiki lakini wana upendo wa hali ya juu kuliko uzunguni...
Kama bi Dada mchoyo kwa mujibu wa maelezo yako si sababu ya umaskini alokuwa nao..
asante Gefu kweli hata wahenga walisema wema usizidi uwezo. Kiukweli nimemchoka naona anamuaibisha dada yake kwa hizi tabia zake yani vituko vyake vinachefua. Akifika anataka apikiwe hata dada wa kazi hataki kumsaidia kuosha vyombo anadai ye kwao hafanyagi kazi!