NIMR: Asilimia 45 ya watoto wachanga wakutwa na Virusi vya homa ya ZIKA Tanzania, asema Mwale Malecela

savo

JF-Expert Member
Sep 14, 2015
279
204
,
Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu, NIMR imethibitisha kugunduliwa kwa virusi vya Zika nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Dkt Mwele Malecela,virusi hivyo vimepatikana mkoani Morogoro, Mashariki mwa Tanzania na Mkoani Geita, kaskazini magharibi mwa Tanzania.

Utafiti huo ulifanyika kutokana na uhalisia kuwa kuna mazingira yanayowezesha kuzaliana kwa mbu wanaoeneza virusi hivyo.

Dkt Mwele Malecela alizungumza na BBC na anafafanua kugundulika kwa virusi hivyo.


Chanzo: BBC


Rais Magufuli: Aliyetangaza ugonjwa wa ZIKA nchini alikuwa anatumika na ndiyo maana nilipomfukuza, waliomtuma wakamteua kuwa Mkurugenzi
 
Nafikiri hili ni 'chezo' kuhamisha mawazo ya wananchi, la kama ni kweli Mungu atuepushe na janga hilo
 
hakuna kitu kama hicho,hizi homa za kutengeneza ili watu wapige dili,tutashuhudia mengi katika hii dunia.
 
Umeona eeh ila ila poa mwenye mkono mwache ajidai namsubiri trump awanyooshe nxt month
 
Embu fikiri unajifanya sista duu au bachela mpka tm hii gafla ukaja gundulika na ugonjwa huu unazani utapata mtoto wa aina gani kama sio type ya zombies@nakujatena
 
Wataalam wa Afya hapa Tanzania wanajua sana kutumia fursa. Mara Dengue imeingia, mara Mafua ya Ndege yameingia, Mara tezi Dume imeshamiri, Mara Homa ya Ini karbia sote tunayo nk nk. Vyooote hivyo ni Kutafuta International Attention ili kupata fedha za Miradi. Wapi MEWATA na Kansa ya Ziwa.....hhahahaaaa nafikiri hawa wakifanyiwa Audit na CAG watakimbia Nchi. Kwa suala la Zika acheni wadau wapige zumari wafadhili waje. Safi sana wataalam wa afya.
 
Kisingizio cha kutokuajiri na kuongeza mishaharà kwani pesa zote zimeelekezwa kwenye mapambano ya kirusi cha Zika. Maana January
kabla hamjaanza kuyadai hayo ngoja tuanze kuwatengeneza kwanza. Nawaza tu kimyakimya
 
Kwa wale ambao hawataki kutumia condom .
Zika inaambukizwa kwa njia ya sex pia.

Vaeni condom mjikinge na mengi.
 
acha tuzaliane bhana hata gufuli kasema fyatueni so mtoto akiwa nakichwa kidogo,kikubwa ndo imetokea tu..
 
Zika ya kuzikana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…