Kwanza kabisa nina sura baya kwa kweli hilo nalijua. Na baada ya kujua hilo, nikasema sitaki watoto wangu wawe na sura baya kama mimi.
Kwahiyo moja ya mkakati wangu ukawa kutafuta mwanamke mwenye sura nzuuri kabisa ili angalau ni dilute kidogo hili sura wasije nilaumu baadae.
Nikatafuta kwa nguvu zote mwanamke mzuri, yani nilitumia uongo grade ya juu hadi nikampa mimba huku nikijua hatuna future yoyote ila nikamdanganya ntamuoa nakadhalika ili tu ata ni dilute hii gene, maana kwetu wote reception ni majanga.
Mimmba ikalelewa hadi akagombana na ndugu zake wasionipenda, akakataa kuitoa kwasababu track niliyompa kwakweli alijua kampata mwanaume bora kuliko wote duniani, na pia alikuwa mgeni kwenye mapenzi hivyo akajua mimi ndiyo kila kitu.
Basi yoote yakaenda juzi usiku akazaliwa njemba. Mimi sikuwepo hospitali ila nilikuwa na safari ya kikazi nje, simu niliyopigiwa na besti yangu ni kwamba njemba inafanana na mimi kopirait pia wakaniwhatsapp. Pumzi zikaniishia kwenye simu. Nikajiuliza sasa hiki ni kitu gani tena? Yani pamoja na kuinvest muda waoote jamaa kafata tena ile reception yetu ya kule nyumbani? Imenidepress vibaya mno maana nimerudi leo nimemuona, du nimechoka. Ila namshukuru Muumba. Naombeni ushauri