1979Magufuli
JF-Expert Member
- Feb 20, 2023
- 439
- 1,754
Mimi sio shabiki hoya hoya, nilikuwa nikienda uwanjani bila kujalj kama mm ni Simba lia lia, kiukweli katika maisha yangu moja ya mawinga hatari niliowahi kuwaona kwa macho yangu ni huyu marehemu Celestine Sikinde Mbunga na huyu Abubakary Salum Sure Boy.
Sikinde alitokea Maji Maji ya Songea alikuwa mtu hatari sana, kuna wakati Yanga waliwahi kucheza na timu moja ya Morocco Sikinde na Sure Boy waliwasumbua sana hadi wakapigwa na waarabu hao, Sure Boy alipasuliwa mdomo.Sikinde alikuwa zaidi ya Edibily Lunyamila maana wengi wamemuona Lunyamila lkn sio marehemu Sikinde.
Sikinde akiwa na kijezi chake cha Vimto alikuwa hakabiki, huku kulia akiwa Sure Boy, moja ya mawinga ambao mimi nasema hadi Leo Sure Boy sijapata mfanowe.Sure Boy alikuwa akiniumiza sana moyo wangu alipokuwa akicheza na Simba maana alikuwa ana chenga za maudhi na uwezo wa kumfanya lolote beki wa kushoto.
Kwa maoni yangu, wametokea mawinga wengi akina marehemu Justin's Mtekere , John Alex, Sammy Bitumba Iyela, Akida Makunda nk lakini kwangu sitokuja kuwasahau hawa jamaa. REST IN PEACE SELESTINE SIKINDE MBUNGA
Sikinde alitokea Maji Maji ya Songea alikuwa mtu hatari sana, kuna wakati Yanga waliwahi kucheza na timu moja ya Morocco Sikinde na Sure Boy waliwasumbua sana hadi wakapigwa na waarabu hao, Sure Boy alipasuliwa mdomo.Sikinde alikuwa zaidi ya Edibily Lunyamila maana wengi wamemuona Lunyamila lkn sio marehemu Sikinde.
Sikinde akiwa na kijezi chake cha Vimto alikuwa hakabiki, huku kulia akiwa Sure Boy, moja ya mawinga ambao mimi nasema hadi Leo Sure Boy sijapata mfanowe.Sure Boy alikuwa akiniumiza sana moyo wangu alipokuwa akicheza na Simba maana alikuwa ana chenga za maudhi na uwezo wa kumfanya lolote beki wa kushoto.
Kwa maoni yangu, wametokea mawinga wengi akina marehemu Justin's Mtekere , John Alex, Sammy Bitumba Iyela, Akida Makunda nk lakini kwangu sitokuja kuwasahau hawa jamaa. REST IN PEACE SELESTINE SIKINDE MBUNGA