kinyamkela mahaba
JF-Expert Member
- May 4, 2022
- 1,181
- 1,574
Jamani za wikiendi, nilikuwa na utaratibu wa kuweka 1,000 kila siku kwenye kibubu chetu na mke, ni miezi mitatu sasa.
Ilitakiwa leo nikute 90k na kidogo, ila nimeikuta 2000 tu. Nimehamaki na kumuuliza mwenzangu ananiuliza zile nyama na ile mikate ya mayai aliyokuwa ananipikia hela alikuwa anatoa wapi?
Baada ya kumbana mno kwa maswali ndiyo akafunguka kuwa alikuwa anachukua yeye na ananunua mahitaji hayo tajwa, ambayo kimsingi hayakuwa na ulazima wowote. Usiku huu naona utakuwa mrefu mno kwangu, mwenzangu ndiyo anakaribia kupitiwa na usingizi muda huu.
Yaani kutoka 90k mpaka 2k kwa mikate ya mayai na nyama mara 3 au 4 kwa wiki? Hayupo serious kabisa huyu mke wangu.
Anathamini mno vyakula vizuri kuliko maendeleo. Ni kweli tulifululiza mno kula nyama na mikate ya mayai na sikujua kuwa anachukua akiba yetu.
Dah!
Ilitakiwa leo nikute 90k na kidogo, ila nimeikuta 2000 tu. Nimehamaki na kumuuliza mwenzangu ananiuliza zile nyama na ile mikate ya mayai aliyokuwa ananipikia hela alikuwa anatoa wapi?
Baada ya kumbana mno kwa maswali ndiyo akafunguka kuwa alikuwa anachukua yeye na ananunua mahitaji hayo tajwa, ambayo kimsingi hayakuwa na ulazima wowote. Usiku huu naona utakuwa mrefu mno kwangu, mwenzangu ndiyo anakaribia kupitiwa na usingizi muda huu.
Yaani kutoka 90k mpaka 2k kwa mikate ya mayai na nyama mara 3 au 4 kwa wiki? Hayupo serious kabisa huyu mke wangu.
Anathamini mno vyakula vizuri kuliko maendeleo. Ni kweli tulifululiza mno kula nyama na mikate ya mayai na sikujua kuwa anachukua akiba yetu.
Dah!