Nimetokea kuchukia ndoa

Mnatusema sana hatuolewi.
Sasa unanisema siolewi halafu anatokea boya mmoja anaingia line nakubali tu tuoane ila moyoni simpendi wala nini.

Nyie wanaume mkipunguza kuona ndoa ni basic need itawapunguzia presha wanawake kukimbilia ndoa za kuwaonyesheni.

Wanawake wengi sana wanacheat siku hizi, ndoa zimepoteza thamani. Zamani tulikua tumezoea wanaume ndio wachepukaji ila imekua kinyume sasa hivi na ndio maana divorce rate imekua juu kwa sababu wanawake hatuheshimu tena ndoa.

Fanya research ndogo utakuta 60% ya ndoa za kileo ni mimba/mtoto. Watu hawaoani kwa sababu wanapendana ila kunakua na kaconnection kanakowalazimu waoane.

Kwa style hii ya wanawake kuolewa kupunguza masimango na wanaume kuoa ili mtoto akue na baba na mama NASEMA kwamba wanaume mtaendelea kupata wanawake mtakaogongewa na ndoa zenu zitaendelea kuvunjika kila leo.
 
Kwanza usiseme umechukia ndoa, sema umechukia ndoa ya huyo rafiki yako

Lakini pia mbona kama stori yako inaonekana Kama chai mkuu?
 
Sielewi unachoshangaa ni nini hasa?
Wasema we ndo umeifanya ndoa hii
Ndoa iendelee kuwepo katika vitabu
La sivyo ingeshasambaratika kitambo

Bazazi
 
Utakuwa umeoa/lewa na jina wewe..
 
Mnatusema sana hatuolewi.
Sasa unanisema siolewi halafu anatokea boya mmoja anaingia line nakubali tu tuoane ila moyoni simpendi wala nini.
NASEMA kwamba wanaume mtaendelea kupata wanawake mtakaogongewa na ndoa zenu zitaendelea kuvunjika kila leo.
Kosa la mwanaume ni kukuoa siyo ndiyo? Kama haujaolewa halafu anatokea mwanaume anahitaji kukuoa na ukamkubalia unahitaji kumheshimu na kama haujampenda mwambie ukweli na haupo tayari kuolewa naye. Kwanini mtendee ubaya mwanaume aliyekupenda na kukuthamini na kukuweka ndani? Wengine wamekutumia mpaka umechakaa na hawajakuoa ila huyu ambaye hajakutumia unataka umtendee ubaya kisa haujampenda. Unaishi ili kuwafurahisha watu au unaishi ili kujifurahisha mwenyewe? Huyo anayekupenda mbona hajakuoa na kibaya zaidi anakutumia ukiwa ndoani na ndoa ikivunjika hana mpango na wewe tena. Unabaki ningelijua. Waheshimu sana wanaume wanaowapenda maana mkiwachukiza watazidi kutoweka na kubaki wanaume wasio na upendo sasa hapo wanawake mtakuwa kwenye hatari sana.
Una miaka 30 haujaolewa umefikisha miaka 33 anatokea jamaa anakuoa na ndoa yenu ina miaka 3 unaanza kumcheat ukiwa na umri wa miaka 36. Jamaa anagundua na kukupiga chini. Huoni kama hii ndiyo aibu sana kuliko hata hiyo ya kusemwa haujaolewa? Bora usiolewe jamii ijue kuliko kuolewa halafu uachwe kwasababu ulifanya umalaya huko nje na uzee wako unamaliza hauna mume. Bora ndoa ivunjike kwa masuala mengine ila siyo kwasababu ya umalaya maana ni aibu sana na fedheha.
 
Wakati mwingine unapenda hasa! Na pia mwanamke anajifunza kupenda hata akiwa ndani ya ndoa ndiyo maana wanawake wa zanani walikuwa wakichaguliwa wachumba.

Hili tatizo limesababishwa na wanaume wenyewe wengi ingawa wameoa lakini kama hawajaoa tu wana wanawake telee,mke akishajua upendo wote hupotea wanabakia kuishi tu kulea watoto..
Wanaume muelewe pesa haiwezi kununua upendo,pamoja na kuhudumia famila kila kitu kama unamvunja moyo mkeo hutaona raha ya hiyo pesa,utabakia kusema tu nampa kila kitu lakini wapi....
Ukiona mkeo amebadilika muulize shida iko wapi mama mbona umebadilika kwa upole tu utajibiwa!
 
Shetani karuhusiwa kumpepeta mwanadamu kama unavyo pepeta mchele kwenye ungo! sema hawa wachungaji wetu hawatuambii ukweli. Shetani anamtumia mwanamke ili kumuangusha mwanaume. No woman No 😭
 
Ni kweli unachosema...

Ila na wanaume pia usioe tusababu una historia na huyo mwanamke au sabubu ya ndugu,halafu unakuja kumtesa na kuchepuka kwako...hii ndiyo sababu ya ndoa nyingi kuwa zipo zipo tu kulipana visasi....
 
Asante sana mkuu kwa hii perfect reply yenye ujazo wa hali ya juu. Nilikuwa naandaa gazeti la kumjibu huyo mwanadada lakini baada ya kukutana na hii comment yako nikaona haina haja tena maana umemaliza kila kitu nilichotaka kukisema.

Unajua bwana kuna watu wengine ukisoma mawazo yao mpaka unajiuliza hivi huyu ni kwanini kwanza bado anaishi duniani? Ni kwanini hata anafikiria mapenzi/mahusiano kwa mindset aliyonayo?

Mzigua90 anajaribu kutwambia kwamba ni heri mwanamke aende akafanye umalaya ndoani kuliko kufanya umalaya akiwa single hili tu haepukane na social pressure ya kutokuolewa!!! What kind of toxic mentality is this?

Yaani alivyojaribu ku-glorify umalaya mpaka nimepatwa na bumbuwazii!

Halafu hapo hapo anatwambia kwamba eti msababishi wa haya yote ni wanaume maana wanaume ndio wamekuwa waki wapressurize wanawake waolewe hata na watu wasiowapenda.. Ni akili hiyo!?

Funga kazi ni hapo anasema kuwa "wanaume ndoa zenu zitazidi kuvunjika" huku akiwapa wanawake verdict yaani utafikiri labda ndoa ikivunjika mwanaume pekee ndio muathirika!!

Inasikitisha sana.
 


Ni kwanini wanawake mnapenda sana to play a victim card hata kwenye hamna?

Yaani kwamba uchepukaji wa wanawake uliokithiri leo hii umesababishwa na wanaume wenyewe how?

So hakuna wanawake wanaochepuka kwa msukumo wa tabia zao wenyewe za kimalaya?

Halafu pia mwanaume wako akichepuka sululisho na wewe ni kwenda kuchepuka.. serious?

Yaani mume wako akiwa na mahawala wengi nje ya ndoa basi na wewe ni kuwa na mabwana wengi nje ya ndoa? Na hili nalo ni sehemu ya usawa mliokuwa mna uhitaji au?

Aisee kama na wewe umeolewa pole zangu nyingi ziende kwa huyo mshikaji unaemuita mume.
 
still niko njia panda maana mmewe amenipigia simu mda huu tukapate chakula cha jioni pamoja kwake ndo nmezid kupata mawazo
 
Wanawake wanavisingizio vyingi sana.
Sisi tukichepuka ni kwasababu ya umalaya wetu
Wao wakichepuka sababu ni sisi wanaume
Tutafika mahala unapiga mimba mwanamke unabeba mtoto unalea, ukihitaji unafanya hivyo hivyo.
 
Usipende sana kufuatilia mambo ya watu...

Utawagombanisha, ila watapatana ubaya utakugeukia wewe... Ulikwakuta wanafanya mapenzi kibarazani, kwa maana yake hukupiga hodi kwenye nyumba ambayo siyo yako...



Cc: mahondaw
 
still niko njia panda maana mmewe amenipigia simu mda huu tukapate chakula cha jioni pamoja kwake ndo nmezid kupata mawazo
Usioneshe hofu yoyote. Nenda ukapate chakula na usiseme neno lolote ila hizo picha usizifute baki kama ushahidi maana huko mbeleni mwanamke atakulazimisha muizime hii issue na akikuona haueleweki atamwambia mumewe kuwa wewe unamtaka kimapenzi na hapo ugomvi lazima uibuke kati yako na jamaa.
 
Maana yangu ni kwamba,wengi wanaume ndiyo mnaoharibu ndoa! Wanawake wanachepuka kwa hasira na kulipa kisasi na wanahamisha mioyo yao kwa michepuko ndiyo hapo ndoa inakuwa ipo ipo tu...

Hao wanawake wachepukaji hao ni malaya ukikosea kuoa utajuta lakini ukipata mwanamke sahihi hata uchepuke anaweza asichepuke na yeye...

Kuhusu mimi,hata wewe ungenioa usingejutia....
 
umetukanwa wapi....we pumbafu sana...katafute kazi ya kufanya......mwanaume kamili hana tabia kama zako....eti na picha nimepiga..kapigie punyeto....iblisi wewe...wachana na ndoa za watu....
Niko na wewe. Usimchunguze na kumchunga mwanamke. Huyo jamaa ni marioo,analelewa mjini. Hapo anatengeneza njia ya kupata hela. Bibi yangu aliniasa nisimchunge mwanamke;nisirudi nyumbani kwa kuvizia,nitoe ishara kuwa mzee anakuja hata kwa kuhoa au kupiga mluzi. Mleta thread ni ovyo katika kujenga familia.
 
Wanawake wanavisingizio vyingi sana.
Sisi tukichepuka ni kwasababu ya umalaya wetu
Wao wakichepuka sababu ni sisi wanaume
Tutafika mahala unapiga mimba mwanamke unabeba mtoto unalea, ukihitaji unafanya hivyo hivyo.
Wanashangaza na wanaudhi..!!

Halafu hiyo ya kuchapa mimba na kusepa hata wao wenyewe wanaikaribisha kwa mikono miwili na hawajui kama ndio watakuwa kwenye losing side.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…