PreGE2025 Nimesikitishwa kuna watanzania wamekamatwa baada ya kuzuia watu ambao hawana sifa za kuandikishwa kupiga kura

PreGE2025 Nimesikitishwa kuna watanzania wamekamatwa baada ya kuzuia watu ambao hawana sifa za kuandikishwa kupiga kura

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Genius Man

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2024
Posts
3,560
Reaction score
7,914
Nimesikitishwa kuona watu wamekamatwa baada ya kuzuia watu wasio na sifa kuandikishwa kupiga kura kwasababu hawana sifa, baadhi yao nimesikia katika vyombo vya habari ikiwemo JamiiForums kuwa walizuiwa kwasababu wananchi wa eneo hilo waliwatambua kuwa sio wakazi wa eneo hilo.

Hii inaweza kupelekea hawa watu wasio wakazi wa eneo hilo kujiandikisha zaidi ya mara moja na ukizingatia uandikishaji wetu hauna utaratibu wa kuhakiki mtu utambulisho wake.

Nilishauri kuwe na utaratibu huu wa kukagua utambulisho wa mtu hata kwenye kitambulisho chake kutaonesha mtaa anao tokea ili kuthibitisha kwamba ni mkazi wa eneo flani na kama yupo kwenye mkoa mwengine na anahitaji kuandikishwa lazima awe na barau hata ya mjumbe ili kumthibitisha utambulisho wake.

Sikuizi hata ukitaka kufungua account JamiiForums unatakiwa uthibitishe email yako lakini sisi kwenye mambo ya msingi na muhimu zaidi tumeshindwa kuweka utaratibu mzuri wa kuhakiki wapiga kura hali inayo pelekea hata zile sheria zetu za uchaguzi kuwa kama mapambo tu haziwezi kufanya kazi ipasavyo.

Kumbuka kuto kuhakiki wapiga kura kunaweza kupitisha watu wasio na sifa kujiandikisha kupiga kura hali inayoweza kupelekea kuvurugika kwa uchaguzi mzima.

watanzania waliokamatwa hawakutakiwa kukamatwa bali tulipaswa turekebishe sheria zetu za uchaguzi kuwe na uhakiki wa taarifa mambo kama haya yasingetokea hivyo watanzania waliokamatwa hawana hatia waachiliwe.
 
Wameshajua jinsi ya kujipigia kura. Vijana wanaandikishwa halafu tume inapiga kura.

Kuna mama kauliza, hwa chadema wamesema 'No Reform no election" sasa kwanini wanahangaika na INEC hata ikiandikisha marehemu? Kwa sababu hakuna reform yoyote itafanyika.
 
Fafanua unazungumzia uchaguzi upi? Uandikisha wa wapiga kura kwaajili ya Uchaguzi Mkuu wa 2025 bado unaendelea.Kwasasa Undikishaji unaingiza namba ya NIDA, na fingerprints za mwananchi anaeandikishwa.

Mwananchi mmoja hataweza kuandikishwa zaidi ya mara moja, mfumo utamkataa.
 
Fafanua unazungumzia uchaguzi upi? Uandikisha wa wapiga kura kwaajili ya Uchaguzi Mkuu wa 2025 bado unaendelea.Kwasasa Undikishaji unaingiza namba ya NIDA, na fingerprints za mwananchi anaeandikishwa.

Mwananchi mmoja hataweza kuandikishwa zaidi ya mara moja, mfumo utamkataa.
watu wamejiandikisha zaidi ya mara moja mfumo wala haujui
 
Back
Top Bottom