Nimeshangaa sana! Eti kuna Chama kinaitwa CHAUSTA?

Nimeshangaa sana! Eti kuna Chama kinaitwa CHAUSTA?

KAMP2015

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2013
Posts
281
Reaction score
69
Ndugu zangu kiukweli nimeshangaa kuona kuna chama cha siasa kinaitwa CHAUSTA na kimempitisha Richard Minja kugombea ubunge jimbo la Kalenga-Iringa.

Basi kama ndo hivi hadi 2020 tutakuwa na utitiri wa vyama zaidi ya 30.

Naomba wanaojua kirefu chake watuambie maana nimekuta katika gazeti la Mwananchi likiwa hivo hivo.
 
Chausta- chama cha haki na ustawi cha James Mapalala.

Hiyo ndio demokrasia yenyewe hata Marekani usidhani vyama ni viwili tu.
 
Weka picha ya huyo mgombea manake kama tushakutana ktk kiti moto ARUSHA.
 
Mbona kipo muda tu? Nakumbuka mwaka 2005 ilibaki kidogo tu kichukue kata ya Kiwalani
 
Mbona kipo muda tu? Nakumbuka mwaka 2005 ilibaki kidogo tu kichukue kata ya Kiwalani

Wacha uongo wewe, chama kinachokaribia kuchukuwa kata kinaweza kushika nafasi ya 3?

Mafanikio ya Chausta kiwalani ni kwa bwana Magid kupewa uenyekiti wa mtaa baada ya ccm kuamuwa kukomoana kutokana na bifu zao za kura za maoni.
 
utakuwa mwana wa bavicha hujui tz ina vyama vingapi then enakwenda kutoa et elimu ya uraia
 
Vyama vyenye usajili wa kudumu, ni CCM, CUF, Chadema, UMD, NCCR-Mageuzi, NLD, UPDP, NRA, Tadea, TLP, UDP, Demokrasia Makini, Chausta, DP, APPT-Maendeleo, Jahazi Asilia na Sau. vilivyo futwa ni People's Democratic Movement (PDM) na Democratic National Congress (DNC).
 
Mbona mimi ni mwanachama??

Sent from my Nokia Lumia using Tapatalk
 
Hivi vyama vingine yaani hata havijulikani vipo kwa ajili ya kumtetea nani zaidi ya matumbo yao tu, Tuwaepuke kama UKOMA...
 
Vyama vyenye usajili wa kudumu, ni CCM, CUF, Chadema, UMD, NCCR-Mageuzi, NLD, UPDP, NRA, Tadea, TLP, UDP, Demokrasia Makini, Chausta, DP, APPT-Maendeleo, Jahazi Asilia na Sau. vilivyo futwa ni People’s Democratic Movement (PDM) na Democratic National Congress (DNC).

Mkuu inamaana vyama vyote hivi vinapokea ruzuku?
 
Ndio Demokrasia yenyewe hiyo, ili mradi utimize masharti ya Katiba ya Nchi.
Vingi vinajifia vyenyewe kwa kukosa Pesa za kuviendesha.


Ndugu zangu kiukweli nimeshangaa kuona kuna chama cha siasa kinaitwa CHAUSTA na kimempitisha Richard Minja kugombea ubunge jimbo la Kalenga-Iringa.

Basi kama ndo hivi hadi 2020 tutakuwa na utitiri wa vyama zaidi ya 30.

Naomba wanaojua kirefu chake watuambie maana nimekuta katika gazeti la Mwananchi likiwa hivo hivo.
 
Back
Top Bottom