sangujoseph
Senior Member
- Nov 30, 2015
- 164
- 184
By Sangu Joseph
.
Leo March 22 , 2020 nimemsikiliza kwa makini sana Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli, na nimeendelea kumsoma zaidi nakujua ni kiongozi ambaye anaujua uhalisia wa wananchi anaowaongoza, kama ambavyo Mimi niliwaza majuma kadhaa yaliyopita. ( Nilipita kituo cha Daladala, Sokoni, Mama Lishe, NK niliwauliza unaweza kumudu maisha bila kufanya kazi na utumie akiba yako tu, baadhi ya walinieleza uwezo wao ni wa siku 2 wengine waliniambia broh hata hiyo akiba hatuna, tunajua tutatuma nini nyumbani tukishafika kwenye mishe)
Licha ya kelele nyingi za muda mrefu juu ya kutangazwa kwa Lock Down, katik jiji la Dar es salaam, lakini yeye amekuja na maamuzi ambayo kwangu nimeyaita kama kuruka mtego wa pili ambao wapinzani wake wangetamani auingie na iwe ngumi yao ya kumpigia hapo baadaye (Soma mtego wa 1 aliouvuka Magufuli Hata mimi ningefanya kama Rais Magufuli - JamiiForums )
Ni kweli tunajua kwa sasa DSM ndiyo inaongoza kuwa na wagonjwa wengi wa Corona kuliko mikoa mingine (Hii ni kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watu Mil. 6 jumlisha na wale wanaoingia na kutoka) tuendelee kutumia nafasi zetu kuwahamasisha kuchukua tahadhari ya kujilinda.
Kwanini nasema Rais Magufuli amevuka mtego huu wa Kulock Down DSM, kwa asilimia kubwa sana ya Watanzania hawana uwezo kumudu maisha ya bila kufanya kazi kuanzia siku 5 wengi wao wakisogea sana siku 3 na wengine huwa wanajua watakula nini baada ya kwenda kutafuta asubuhi.
Sasa mtego ungekua hapa endapo Rais angeruhusu lock Down maana yake shughuli za kiuchumi na uzalishaji zisingefanyika ndani ya Dar es salaam na hata nje ya DSM (Imagine wewe ndiyo Rais unawafungia watu Mil 6 asilimia 80 hawana uwezo wa kusurvive kuanzia siku 3, ungeongozaje)
Hivyo uamuzi Kulock Down DSM, ungepelekea idadi kubwa sana ya Watanzania ambao hawana uwezo wa kumudu maisha kwa muda mrefu tungesikia taarifa nyingi mno juu ya athari za njaa, Vifo na pengine hata kuongezeka kwa matukio ya kiuhalifu kwa sababu watu wanasaka chakula na kujikimu.
Hivyo badala ya kuwaponya watu na Corona tungewaua watu kwa njaa, na matukio ya uhalifu hilo, kwa uamuzi huu wa Rais Magufuli kwangu ameruka mtego mwingine nampongeza sana.
.
Insta : FB ; Twit : Sangu Joseph
.
#KijanaMzalendo #IloveTZ
Sent using Jamii Forums mobile app
.
Leo March 22 , 2020 nimemsikiliza kwa makini sana Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli, na nimeendelea kumsoma zaidi nakujua ni kiongozi ambaye anaujua uhalisia wa wananchi anaowaongoza, kama ambavyo Mimi niliwaza majuma kadhaa yaliyopita. ( Nilipita kituo cha Daladala, Sokoni, Mama Lishe, NK niliwauliza unaweza kumudu maisha bila kufanya kazi na utumie akiba yako tu, baadhi ya walinieleza uwezo wao ni wa siku 2 wengine waliniambia broh hata hiyo akiba hatuna, tunajua tutatuma nini nyumbani tukishafika kwenye mishe)
Licha ya kelele nyingi za muda mrefu juu ya kutangazwa kwa Lock Down, katik jiji la Dar es salaam, lakini yeye amekuja na maamuzi ambayo kwangu nimeyaita kama kuruka mtego wa pili ambao wapinzani wake wangetamani auingie na iwe ngumi yao ya kumpigia hapo baadaye (Soma mtego wa 1 aliouvuka Magufuli Hata mimi ningefanya kama Rais Magufuli - JamiiForums )
Ni kweli tunajua kwa sasa DSM ndiyo inaongoza kuwa na wagonjwa wengi wa Corona kuliko mikoa mingine (Hii ni kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watu Mil. 6 jumlisha na wale wanaoingia na kutoka) tuendelee kutumia nafasi zetu kuwahamasisha kuchukua tahadhari ya kujilinda.
Kwanini nasema Rais Magufuli amevuka mtego huu wa Kulock Down DSM, kwa asilimia kubwa sana ya Watanzania hawana uwezo kumudu maisha ya bila kufanya kazi kuanzia siku 5 wengi wao wakisogea sana siku 3 na wengine huwa wanajua watakula nini baada ya kwenda kutafuta asubuhi.
Sasa mtego ungekua hapa endapo Rais angeruhusu lock Down maana yake shughuli za kiuchumi na uzalishaji zisingefanyika ndani ya Dar es salaam na hata nje ya DSM (Imagine wewe ndiyo Rais unawafungia watu Mil 6 asilimia 80 hawana uwezo wa kusurvive kuanzia siku 3, ungeongozaje)
Hivyo uamuzi Kulock Down DSM, ungepelekea idadi kubwa sana ya Watanzania ambao hawana uwezo wa kumudu maisha kwa muda mrefu tungesikia taarifa nyingi mno juu ya athari za njaa, Vifo na pengine hata kuongezeka kwa matukio ya kiuhalifu kwa sababu watu wanasaka chakula na kujikimu.
Hivyo badala ya kuwaponya watu na Corona tungewaua watu kwa njaa, na matukio ya uhalifu hilo, kwa uamuzi huu wa Rais Magufuli kwangu ameruka mtego mwingine nampongeza sana.
.
Insta : FB ; Twit : Sangu Joseph
.
#KijanaMzalendo #IloveTZ
Sent using Jamii Forums mobile app