Nimepata Tender za Nest na TRA wanakataa kunisajili VAT, je nifanyaje?

Nimepata Tender za Nest na TRA wanakataa kunisajili VAT, je nifanyaje?

Upepo wa Pesa

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2015
Posts
21,786
Reaction score
35,747
Kwa mujibu wa sheria, ili mfanyabiashara asajiliwe kama VAT unatakiwa either ufike makusanyo ua 200m kwa mwaka, au uwe mtoa ushauri wa kitaalamu au uwe na mikataba inayoonesha kazi uliyopata.

Sasa mimi naona nimeangukia hapo kundi la 3 maana japo ni kweli sijafika makusanyo ya 200m kwa mwaka ila nna mikataba ya Nest inayotaka ni supply vitu na mikataba ina VAT.

Nimejaribu kwenda ofisi ya TRA ili kuomba kusajiliwa lakini wamegoma! Je nafanyaje na nimeshalipwa natakiwa kutoa receipt?

Naombeni uzoefu wadau, je kama ulishapitia hii changamoto ulifanyaje kuvuka? Je nitoe recipt YA EFD isiyo na VAT?
 
Nachojua wakati unapata mashine unaulizwa VAT iwepo au isiwepo. Wakulungwa wanajibu isiwepo, haya madhara si ndo kama hayo?

Sidhani kama ni dhambi kisheria kutoa risiti bila VAT, we watolee. Unless mteja wako ndio akatae..
 
Baada ya kufika kwao wanasema mikataba lazima iwe ya 100m, kwa kweli kwa tunao anza kupata mkataba wa 100m at once si kazi rahisi na ndio maana tunajikongoja taratibu ili tufike huko juu! Sasa nimewapelekea mikata niliyo nayo wamegoma! Na nnatakiwa kutoa receipt! Je nitoe tu receipt ya efd isiyo na vat?
 
Nachojua wakati unapata mashine unaulizwa VAT iwepo au isiwepo. Wakulungwa wanajibu isiwepo, haya madhara si ndo kama hayo?

Sidhani kama ni dhambi kisheria kutoa risiti bila VAT, we watolee. Unless mteja wako ndio akatae..
Ukisema uwekewe vat watakuuliza VRN number na huna! So ngoma ina baki pale pale..
 
Baada ya kufika kwao wanasema mikataba lazima iwe ya 100m, kwa kweli kwa tunao anza kupata mkataba wa 100m at once si kazi rahisi na ndio maana tunajikongoja taratibu ili tufike huko juu! Sasa nimewapelekea mikata niliyo nayo wamegoma! Na nnatakiwa kutoa receipt! Je nitoe tu receipt ya efd isiyo na vat?
Toa.. mpe mteja.. kwani ni mara yako ya kwanza kutoa risiti? Kama sio, je kuna kibaya kilishatokea ulipotoa risiti ya mashine bila VAT?
 
Toa.. mpe mteja.. kwani ni mara yako ya kwanza kutoa risiti? Kama sio, je kuna kibaya kilishatokea ulipotoa risiti ya mashine bila VAT?
Nilivyoona mkataba unasema kuna 18% ya vat ndio nikapata shaka kidogo hasa ukizingatia niliyo lipwa ni kiasi chenye vat ndani. Ila nikiona ngoma ngumu itabidi nitoe risiti tu hamna namna!
 
Kwa mujibu wa sheria, ili mfanyabiashara asajiliwe kama VAT unatakiwa either ufike makusanyo ua 200m kwa mwaka, au uwe mtoa ushauri wa kitaalamu au uwe na mikataba inayoonesha kazi uliyopata.

Sasa mimi naona nimeangukia hapo kundi la 3 maana japo ni kweli sijafika makusanyo ya 200m kwa mwaka ila nna mikataba ya Nest inayotaka ni supply vitu na mikataba ina VAT.

Nimejaribu kwenda ofisi ya TRA ili kuomba kusajiliwa lakini wamegoma! Je nafanyaje na nimeshalipwa natakiwa kutoa receipt?

Naombeni uzoefu wadau, je kama ulishapitia hii changamoto ulifanyaje kuvuka? Je nitoe recipt YA EFD isiyo na VAT?
Mzee,hiyo taasisi waambie tu huna VAT,then watolee tu risiti..mbona normal tunafanya hivyo always.
 
Back
Top Bottom