Nimepata kazi South Africa, baba kanikataza kwenda

xaidjr

JF-Expert Member
May 29, 2016
392
467
Habari zenu humu ndani,

Nawasilisha kama kichwa cha habari hapo juu mimi ni diploma graduate based on accounts. Majuzi hivi nili-apply kazi moja kutoka South Africa ambayo ilihitaji watu kutoka Tanzania, ilitangazwa Zoom Tanzania.

Kwa kuwa walihitaji CV, nikawatumia kesho yake ambapo ni Jana. Mida ya saa tano nilipata email kutoka kwao wakisema wamepitia CV na wameipenda so wakanipa questionnaire. Bhasi sikuchelewa nikaijaza Nika send back to them.

Leo asubuhi wakanitumia message I got accepted and if we can communicate through WhatsApp bhasi nikawatext, wakanambia kama nina passport nikawaambia hapana, wakasema kama naweza ipata kabla ya March nikasema nitafanya hivoo, then wakanambia as soon as possible nikiipata niwaambie.

Bhasi mi kwa muda wa miezi 7 nipo nyumban nikabidi nimshirikishe mzee kuhusu passport kwa sababu yeye ndio anayejua. Alichoniambia ni kwamba tafuta kazi sehemu nyingine, South Africa sio nchi ya kwenda..

Duh! Nimefadhaika sana ukizingatia nimetuma application zaidi ya 100 hapa Tanzania I only got respond once, tena nikiambiwa tuma 20000 nikupe maswali ya interview na ukipata kazi utanipa 200,000 mshahara 900,000, nikaipotezea.

Wadau naombeni ushauri katika hili. Ni sawa kuchukua opportunity hii na kumkonvice mshua kwamba SA ni pahali pazuri ukiwa una kazi? Please msaada wanajamviii wenzangu
 
Nenda kafanye kazi mkuu.
Cha msingi jaribu kufuatilia taarifa ya hiyo taasisi.
Mzee ana wasiwasi ni kawaida kwa sababu anafikiria kukaa mbali na wewe na vipi utaweza kujimudu (pengine amekulea kama mayai) na bado haamini kwamba unaweza kujitegemea.Ni hofu tu ya mzazi kwa mwanawe.
 
Nenda kafanye kazi mkuu.
Cha msingi jaribu kufuatilia taarifa ya hiyo taasisi.
Mzee ana wasiwasi ni kawaida kwa sababu anafikiria kukaa mbali na wewe na vipi utaweza kujimudu (pengine amekulea kama mayai) na bado haamini kwamba unaweza kujitegemea.Ni hofu tu ya mzazi kwa mwanawe.
Mkuu sijalelewa kimayai na sio Mara ya kwanza kuka mbali name by the way nashukuru kwa ushaur mkuu pamoja
 
Sizan kama kuna kazi za kirahisi kutoka nje ya nchi kama ulivojielezea. Usifurahi sana kuwa umepata kazi waweza kua matapeli tu na wameplan kukutapeli itakapofikia wakati wa kutafuta
working permit
Visa
Psychometric Test na
Air ticketing.

Nina uzoefu kwenye hizo mambo nimewah pata kazi Somalia, na Belgium.

Sisemi haiwezekani bali nakuasa kua makini vinginevo waweza kupata hasara na ukajutia maneno yako na kukumbuka mzazi wako
 
Sizan kama kuna kazi za kirahisi kutoka nje ya nchi kama ulivojielezea. Usifurahi sana kuwa umepata kazi waweza kua matapeli tu na wameplan kukutapeli itakapofikia wakati wa kutafuta
working permit
Visa
Psychometric Test na
Air ticketing.

Nina uzoefu kwenye hizo mambo nimewah pata kazi Somalia, na Belgium.

Sisemi haiwezekani bali nakuasa kua makini vinginevo waweza kupata hasara na ukajutia maneno yako na kukumbuka mzazi wako
Nimekusoma mkuu ebu wangalie wanajiita the be investment corporation ni group of company ilikuwa founded 1992 na employees ni 11-50 so ndo mna nkaleta hapa ushauri wako ndo unanipa njia mkuu asajteh sana
 
Sizan kama kuna kazi za kirahisi kutoka nje ya nchi kama ulivojielezea. Usifurahi sana kuwa umepata kazi waweza kua matapeli tu na wameplan kukutapeli itakapofikia wakati wa kutafuta
working permit
Visa
Psychometric Test na
Air ticketing.

Nina uzoefu kwenye hizo mambo nimewah pata kazi Somalia, na Belgium.

Sisemi haiwezekani bali nakuasa kua makini vinginevo waweza kupata hasara na ukajutia maneno yako na kukumbuka mzazi wako
Well said,, akikuta ndivo sivo atapambana tu kiume kuliko kubaki hii nchi ambayo ata ajira zake hazijulikan zitatokaga lini
 
Nimekusoma mkuu ebu wangalie wanajiita the be investment corporation ni group of company ilikuwa founded 1992 na employees ni 11-50 so ndo mna nkaleta hapa ushauri wako ndo unanipa njia mkuu asajteh sana
only 11-50 employees for the whole company or what ar' you trying to say Dude!!
Nimekusoma mkuu ebu wangalie wanajiita the be investment corporation ni group of company ilikuwa founded 1992 na employees ni 11-50 so ndo mna nkaleta hapa ushauri wako ndo unanipa njia mkuu asajteh sana
only 11-50 employees for the whole company or what ar' you trying to say Dude!!
 
hakuna kazi unaipata kirahisi hivyo South Africa tena accountant .... work permit ya south Africa ni ngumu sana kuipata na unatakiwa uwe na rare profession za south Africa pia unaanza kuiapply nchini kwako

Be ware .... hao watakuwa ni wanageria aka wapopo wa 416

siku njema
 
Nimekusoma mkuu ebu wangalie wanajiita the be investment corporation ni group of company ilikuwa founded 1992 na employees ni 11-50 so ndo mna nkaleta hapa ushauri wako ndo unanipa njia mkuu asajteh sana
Inawezekana kweli ipo hiyo kampuni yenye hizo details ulizoweka, je una uhakika gani kama ni wahusika wenyewe ndo unaowasiliana nao ? Na sio wataalam kutoka Lagos ? Fanya double check kupata real email yao kupitia search engines kama Google uwasiliane nao kama wanayo taarifa yako...
 
ushauri wangu ni kwamba jaribu kumshawishi baba ako akuruhusu kwenda SA, kama akikataa usinyanyue mguu wako, endelea kutafuta kazi hapa hapa TZ and by Grace of God utapata ajira. but NEVER go against your father in this.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom