Nimempoteza Gongolamboto...!

Mkwaruzo

JF-Expert Member
Feb 21, 2011
563
98
Sidiriki kuyapima machofu ya kazi yako, inayokupa usumbufu kutoka kwa mgambo wa jiji. Inayokupigisha virungu mkiwa mnkimbizana kama vile watoto wapo mchezoni. Au ile ya nyongeza ya kukesha na zege usiku mzima. Huku ukiwa umeniacha mpweke kitandani. Yote hayo uliyafanya kwa ajili yangu mimi na watoto. Nilikuhurumia na kukupenda sana, kufikia kiasi cha kukosa hata ladha ya chakula bila ya kula nawe. Tukiwa tunaishi kwa utaratibu huo, siwezi kuisahau siku hii, baada ya chakula kuwa tayari na kuwakogesha watoto, nilianza na simulizi nzuri ili kuufanya mlo kuwa wa furaha kwao. Mara Baba Chanja ukapiaga hodi, nami kwa heshima nilikuja kukufungulia na kukupokea huku nikikukaribisha ndani bila ya kuacha utani wa hapa na pale kukufanya uwe na furaha. Nilipaswa kuwa na kila sababu ya utiifu kwako kwani nawe ulinipenda na pia kunijali.
Basi nikakuandalia maji ya kukoga na kubaki nakusubiria kwa ajili ya kula. Haikupita muda, vishindo vya ajabu na moto mwingi uliweza kuonekana katika kila pembe ya mitaa yetu ya Gongolamboto. Wakati nikiwa sijuwi hata wapi pakuelekea, sikuamini macho yangu kukuona upo hoi umeshajeruhiwa na bomo. Nguvu ziliniishia,nikamua kumruhusu Farjala akimbie na wadogo zake watatu na waende wanapoweza. Bali mimi nilibaki nawe huku nikiwa na kichanga changu mgongoni ambacho kilikwisha kaukwa na sauti kwa kilio. Sauti ya simanzi iliyoambatana na maumivu, uliitoa kuleta ujumbe wa maagano kati yetu. Uchungu wa hayo maneno yako ya mwisho yananifanya nashindwa kufanya lolote pale yanapojireje akilini mwangu. Kwa sasa nimebaki nakukumbuka tu Baba Chanja na kukuombea makazi mema huko uliko. Ila sijuwi wapi naweza kumpata mwengine kama wewe wa kuwa farijiko la moyo wangu.
 
pole mama chanja, usijali kazi ya Mungu haina makosa kama bado age inaruhusu utapata mwingne wakukufariji hadi nawe utakapomfuata baba chanja
 
Jamani Mama Chanja ,Chozi limenitoka pamoja nawe mungu akupe faraja katika maisha yako yote ,ni ngumu sana kumpoteza mpendwa wa moyo wako ,wewe ulimpenda lakini mungu kampenda zaidi ,Jipe moyo mkuu
 
kwa huzuni uliyonayo ,hakika maneno yangu hayawezi kukufuta simanzi ,na machozi yakutokayo siwezi kausha kwa ujumbe ,zaidi niliwezalo ni kukuambia mama chanja piga moyo konde ,ingiza ujasiri moyoni mwako ujipe nguvu kuwapigania chanja na wadogo zake wapate maisha mema na mwenyezi mungu atakujalia farijiko la moyo wako.
 
Sidiriki kuyapima machofu ya kazi yako, inayokupa usumbufu kutoka kwa mgambo wa jiji. Inayokupigisha virungu mkiwa mnkimbizana kama vile watoto wapo mchezoni. Au ile ya nyongeza ya kukesha na zege usiku mzima. Huku ukiwa umeniacha mpweke kitandani. Yote hayo uliyafanya kwa ajili yangu mimi na watoto. Nilikuhurumia na kukupenda sana, kufikia kiasi cha kukosa hata ladha ya chakula bila ya kula nawe. Tukiwa tunaishi kwa utaratibu huo, siwezi kuisahau siku hii, baada ya chakula kuwa tayari na kuwakogesha watoto, nilianza na simulizi nzuri ili kuufanya mlo kuwa wa furaha kwao. Mara Baba Chanja ukapiaga hodi, nami kwa heshima nilikuja kukufungulia na kukupokea huku nikikukaribisha ndani bila ya kuacha utani wa hapa na pale kukufanya uwe na furaha. Nilipaswa kuwa na kila sababu ya utiifu kwako kwani nawe ulinipenda na pia kunijali.
Basi nikakuandalia maji ya kukoga na kubaki nakusubiria kwa ajili ya kula. Haikupita muda, vishindo vya ajabu na moto mwingi uliweza kuonekana katika kila pembe ya mitaa yetu ya Gongolamboto. Wakati nikiwa sijuwi hata wapi pakuelekea, sikuamini macho yangu kukuona upo hoi umeshajeruhiwa na bomo. Nguvu ziliniishia,nikamua kumruhusu Farjala akimbie na wadogo zake watatu na waende wanapoweza. Bali mimi nilibaki nawe huku nikiwa na kichanga changu mgongoni ambacho kilikwisha kaukwa na sauti kwa kilio. Sauti ya simanzi iliyoambatana na maumivu, uliitoa kuleta ujumbe wa maagano kati yetu. Uchungu wa hayo maneno yako ya mwisho yananifanya nashindwa kufanya lolote pale yanapojireje akilini mwangu. Kwa sasa nimebaki nakukumbuka tu Baba Chanja na kukuombea makazi mema huko uliko. Ila sijuwi wapi naweza kumpata mwengine kama wewe wa kuwa farijiko la moyo wangu.

Nimejikaza lakini machozi nimeshindwa kuyazuia!pole sana mama Chanja,Mungu akupe faraja siku zote,mwachie Mungu tu,inauma sana uwe na amani mpendwa wangu
 
Alitakalo muumba cku zote huwa,jina lake lihimidiwe,hakuna kifo kinachokusa sababu kwa hiyo gongolamboto ni sababu tu,hata kama icngekuwa gongolamboto ingekuwa kwa ki2 kingine chochote,hivyo piga moyo konde, utayashinda.
 
Simanzi na masikitiko ya kuondokewa na mpendwa wa moyo wako daima huwa ni makubwa. Lakini msaada wa vitendo na maneno humpa moyo muathirika wa janga lolote lile. In reallity nilichokiwasilisha hapa kinamuwakilisha mama wa Mbagala na Gongolamboto kwa yaliyo watokea. Nami kwa heshima nazipokea pole zote zilizotolewa kwa mioyo mikunjufu zinazoonyesha wingi wa imani na machungu kwa yale yaliyotokea.
 
hii novel inaitwaje?

Baada ya kuitayarisha hiyo kazi, sikuchukua muda mrefu kufikiria title ya kuweka coz nilikuwa na kazi, hivyo niliiweka hiyo ya NIMEMPOTEZA GONGOLAMBOTO lkn nimeiona kuwa haiko poa that why nimejaribu kuibadilisha na kutaka kuiweka ya MABOMU YAMEMCHUKUWA BABA CHANJA lkn imenishinda. Ipi iko poa?
 
Pole mama Chanja hakika mkono wa Bwana hautapungua kwako na kazi yake haina makosa, mipango yake daima iko sahihi na faraja pekee ipo kwake. Tumshukuru yeye kwa kila jambo!
 
pole mama chanja. Mungu akurehemu na kukuzingira pande zote hata usipungukiwe na kitu. amen

Glory to God
 
Sidiriki kuyapima machofu ya kazi yako, inayokupa usumbufu kutoka kwa mgambo wa jiji. Inayokupigisha virungu mkiwa mnkimbizana kama vile watoto wapo mchezoni. Au ile ya nyongeza ya kukesha na zege usiku mzima. Huku ukiwa umeniacha mpweke kitandani. Yote hayo uliyafanya kwa ajili yangu mimi na watoto. Nilikuhurumia na kukupenda sana, kufikia kiasi cha kukosa hata ladha ya chakula bila ya kula nawe. Tukiwa tunaishi kwa utaratibu huo, siwezi kuisahau siku hii, baada ya chakula kuwa tayari na kuwakogesha watoto, nilianza na simulizi nzuri ili kuufanya mlo kuwa wa furaha kwao. Mara Baba Chanja ukapiaga hodi, nami kwa heshima nilikuja kukufungulia na kukupokea huku nikikukaribisha ndani bila ya kuacha utani wa hapa na pale kukufanya uwe na furaha. Nilipaswa kuwa na kila sababu ya utiifu kwako kwani nawe ulinipenda na pia kunijali.
Basi nikakuandalia maji ya kukoga na kubaki nakusubiria kwa ajili ya kula. Haikupita muda, vishindo vya ajabu na moto mwingi uliweza kuonekana katika kila pembe ya mitaa yetu ya Gongolamboto. Wakati nikiwa sijuwi hata wapi pakuelekea, sikuamini macho yangu kukuona upo hoi umeshajeruhiwa na bomo. Nguvu ziliniishia,nikamua kumruhusu Farjala akimbie na wadogo zake watatu na waende wanapoweza. Bali mimi nilibaki nawe huku nikiwa na kichanga changu mgongoni ambacho kilikwisha kaukwa na sauti kwa kilio. Sauti ya simanzi iliyoambatana na maumivu, uliitoa kuleta ujumbe wa maagano kati yetu. Uchungu wa hayo maneno yako ya mwisho yananifanya nashindwa kufanya lolote pale yanapojireje akilini mwangu. Kwa sasa nimebaki nakukumbuka tu Baba Chanja na kukuombea makazi mema huko uliko. Ila sijuwi wapi naweza kumpata mwengine kama wewe wa kuwa farijiko la moyo wangu.


Dah! Very touching mpaka machozi yamenilengalenga, pole sana. Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi~AMEN.
 
Aaaaah! Watu wengine bana. Bado tuna kumbukumbu ya maafa pamoja na vifo kutokana na ajali ya gongolamboto. Uchungu na kumbukumbu bado zipo fresh kuhusiana na ajali ile. Uandishi wako ungalitaja majina na mazingira tofauti lakini ujumbe ulokusudia ukafika. Mimi nimeguswa na stori hadi nashindwa kumalizia.....kumbe ni urongo!
 
Back
Top Bottom