Nimekutana nae.........

bodachogo

Member
Apr 14, 2011
89
8
ni muda mrefu toka tumeonana mara ya mwisho,
Leo nimeonana nae lkn hanikumbuki kabisa.,me namkumbuka cz nili-fall kwake but I failed to tell her ,how I felt. Tumeongea kwa kirefu ,trying to remind her , hapa na pale. At last najikuta nataka use this opportunity kumwambia ukweli, sitaki kukumbana na rejection tena ,coz i have been rejected several times mpaka nahisi nimerogwa. Ni siku 3 zimepita toka tumekutana ,nifanye nini ili this time nisikumbane na rejection cz nimechoka hizi rejection. Jaribu kuwa na hisia za kukataliwa na almost every woman you have come accros ndo utajua namaanisha nini. Ahsante kwa msaada.....
Since nimemuona najisiki furaha lkn huzuni huanza pale ninapoona kama atanitendea kama wengine,hakuna hisia mbaya kama kujihisi "insecure"
Ningekuwa mdogo kiumri isingekuwa shida but i m 27yrs old,
No jokes,if you think you can't help just pass....
 
Dah... by the time you finish reading, ushauri wote unakuwa umepaa....
 
Achana na tamaa za kufatafata mabinti, tafuta wa kuoa kama bado na kama tayari umeoa, acha kufukuzia mabinti wa barabarani.
The unseen is illustrated by the seen.
 
Watu hutafuta furaha nawe umefurahi kukutana nae lakini kumweleza ndio mwanzo wa kutokuwa na furaha! Ushauri wangu ni kuwa endelea tu kufurahi kwa kukumbuka ulivyokutana nae usije ukaiharibu furaha kwa kumwambia kilicho moyoni mwako!
 
Mkuu kitu cha kwanza unachopaswa kujua, je anakuchangamkia mkiongea naye? ukimtumia ujumbe wa simu or ukimpigia simu hakawii kukujibu? Je anaenjoy maongezi yenu? Haoneshi kuboreka mfano kuonge, or kukaa na wewe kwa muda kidogo?
Kama majibu yote yatakuwa ni positive basi una nafasi kubwa ya kumchukua. Kama ni Negative then kutakuwa na ugumu.
Nipe majibu then nitakuPM ni jinsi gani unaweza mpata.
NB: Hawa ni urithi wetu, so usiogope kijana:first:
 
sijawahi kataliwa n msichana coz nawasoma kabla yakuwaingia,dalili zinaonekana mapema mkuu..
la muhimu angalia ka mnalingana,wahanga walisema kila shetani na mbuyu wake mkuu,,,
 
Dah... by the time you finish reading, ushauri wote unakuwa umepaa....

Ha ha ha ha sijafika hata mstari wa tatu nikaona labda nikisoma comment ntaelewa kilichokua kimeandikwa......holaaa
 
Jichunguze ze way unavyomwaga sera mara kikwete mjomba wangu, leo nimepanda daladala gari langu bovu, wakati hata bajaji huna,mara mimi sijakulia uswahilini,au ukinikubali matatizo na shida zako zoote nitazimaliza. kwa sera hizo kaka utahuzunika milele
 
Mkuu kitu cha kwanza unachopaswa kujua, je anakuchangamkia mkiongea naye? ukimtumia ujumbe wa simu or ukimpigia simu hakawii kukujibu? Je anaenjoy maongezi yenu? Haoneshi kuboreka mfano kuonge, or kukaa na wewe kwa muda kidogo?
Kama majibu yote yatakuwa ni positive basi una nafasi kubwa ya kumchukua. Kama ni Negative then kutakuwa na ugumu.
Nipe majibu then nitakuPM ni jinsi gani unaweza mpata.
NB: Hawa ni urithi wetu, so usiogope kijana:first:
Mbimbinho yaelekea wewe ni mtaalamu wa kutupa ndoana, unatumia skills gani mwenzetu?
 
Last edited by a moderator:
Anza taratibu kwa kujenga mazoea si ya dada na kaka, bali mazoea ya kawaida kama kujaribu kumjulia hali anagalau mara mbili kwa siku lakini epuka kumghasi.
Fanya mtoko mara chache kwa mwezi lakini hii isiwe siku za karibuni.
Mwisho jaribu kumuuliza kama ana mtu au lah, hii itakusaidia kujua kama ana mtu wameshibana kiasi gani na kama hana ndio huenda ikawa nafasi yako kuonesha hisia zako kwake.

Note: Ukichelewa sana atakuchukulia kama kaka au ndugu wa karibu na hapo ndipo itakua ngumu kuanzisha mahusiano.
 
mazoea yakizidi atakufanya mtu wake wa karibu kama kaka au rafiki jaribu kumueleza shida yako mapema
 
Mbimbinho yaelekea wewe ni mtaalamu wa kutupa ndoana, unatumia skills gani mwenzetu?

Mkuu gfsonwin hakuna skills zozote hapa, ni kumjua na mkumsoma. Wahenga walisema mbwa ukimjua jina wala hakupi shida...:glasses-nerdy:. Mkuu trust me hakuna mwanamke mgumu duniani and they are all the same mkuu.
NB: Najua wanaweza kuja hapa na kuanza kuponda, but that's the truth.
 
Last edited by a moderator:
Chomekea vizuri shati safi, then panga mabunda ya noti za tzs 10,000 zungusha kiuno kizima nakuambia hachomoki hapo
 
Mkuu gfsonwin hakuna skills zozote hapa, ni kumjua na mkumsoma. Wahenga walisema mbwa ukimjua jina wala hakupi shida...:glasses-nerdy:. Mkuu trust me hakuna mwanamke mgumu duniani and they are all the same mkuu.
NB: Najua wanaweza kuja hapa na kuanza kuponda, but that's the truth.

sina haja ya kuponda mkuu Mbimbinho ishu tu ni jins ulivyomwambia akupm lololol hasa siku akinyimwa unyumba si utampa tena desa? na je si waweza mtongoza wewe ukampiku?
 
Last edited by a moderator:
sina haja ya kuponda mkuu Mbimbinho ishu tu ni jins ulivyomwambia akupm lololol hasa siku akinyimwa unyumba si utampa tena desa? na je si waweza mtongoza wewe ukampiku?

Hahahahaa., mkuu gfsonwin sio kiivo asee, tunasaidiana si unajua kila mtu na sector yake. So, hapa tunapeana ushauri tu, na wala hata sihitaji kumjua yeye wala mwanamke wake.:glasses-nerdy:
 
Last edited by a moderator:
Mi kwangu naanza kwa kukuuliza, is she your type?, sio unaenda tu kwa mtu ambaye yaani types zenu haziendani kabisa, for example we decent person na yeye ni kicheche kupitiliza, we unakesha kanisani, hujui hata club moja, na yeye club ndio kama nyumbani kwao usiku, wewe ni mlevi, yeye hanywi kabisa, kazoea mapedezyee, mwenzangu na Mimi una gari moja, tena starlet, chunguza ujue ni types gani za Wanaume anapenda, pia kimo, age, body size, elimu, kabila, na hata dini na rangi zao, though hivi, hasa dini, sometimes kama watu wamependana kweli havina uzito, pia angalie anavyoreact anapokuona, je anakufurahia, anakufurahia vipi, as a friend, kibuzi au kama mtu anayekufeel kinoma, yaani kimapenzimapenzi fulani, I mean kuwe na chemistry kati yenu, yaani kama wote mnavutika, mnaonyesha kuvutiwa, mnatamani kuwa karibu kila mara, sio unamwomba umtoe out, anakuambia that day or hiyo day atakuwa yuko busy na hakupi option ya siku nyingine, hakuelezi ni lini mnaweza kutoka, ujue haoni umuhimu, hajisikii kuwa karibu na wewe, je ana mtu au hana, mnatofautiana vipi na that person, kama una sifa anazozitaka na huyo jamaa yake ana mapungufu fulani kwenye huo uhusiano, maybe hamtreat well, hamtoi out, hamthamini, anampiga na kumtukana, huo ni mwanya mzuri wa wewe kumpata, mfanye ajisikie wa thamani, mfanye ajione mtu wa thamani, na wa maana sana kwako, mwonyeshe unavyomjali, na yeye kama ameuona na kuuappriciate upendo wako kwake, atakupa nafasi ya kuwa wake, iwe kama namna ilivyokuwa kwenye ile video ya Ben Pol ya "Nikikupata", BUT kama unaona kabisa hakufagilii, type zenu haziendani hata kidogo, hawezi kubadilika au wewe huwezi kubadilika ili angalau muendane, haonyeshi kuwa interested kumeet na wewe, haonyeshi kukufurahia hasa mnapokutana, Mheshimiwa hapo itabidi uchukue time yako, cause atakuwa kiukweli hana mpango na wewe , na ukijifanya king'ang'anizi atakupeleka puta na atakufanya ATM hata kwa kidogo ulichonacho then akishakufilisi akumwage, kuwa makini!
 
Mkuu kitu cha kwanza unachopaswa kujua, je anakuchangamkia mkiongea naye? ukimtumia ujumbe wa simu or ukimpigia simu hakawii kukujibu? Je anaenjoy maongezi yenu? Haoneshi kuboreka mfano kuonge, or kukaa na wewe kwa muda kidogo?
Kama majibu yote yatakuwa ni positive basi una nafasi kubwa ya kumchukua. Kama ni Negative then kutakuwa na ugumu.
Nipe majibu then nitakuPM ni jinsi gani unaweza mpata.
NB: Hawa ni urithi wetu, so usiogope kijana:first:

Thanx for your concern, sijaenda mbali sana toka tubadilishane namba na siku hiyo alikuwa normal tu, napanga jinsi ya kumleta karibu.
Nisije nikaumia ka zamani,huwezi amini kwangu mapenzi nayaona kama almasi, sijawahi kuwa katika uhusiano wenye furaha, nimedanganywa ,nimependwa nisipopenda na nikashindwa kabisa kulazimisha hisia, sijua kwa nini inatokea kwangu tu,bora hata nitendwe ili nikose kabisa hamu ya kupenda ......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom