Nimejifunza kitu kuhusu Sadaka

Nimejifunza kitu kuhusu Sadaka

CHIBA One

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2018
Posts
558
Reaction score
2,100
Jumapili iliyoisha Nilienda mwenye ibada kama kawaida, nikaketi Mistari kadhaa kutoka mbele, kwa kuwa nilikuwa nimewahi,

Ibada iliendelea kwa Kwaya za kanisani kwetu kutoa ujumbe kwa njia ya uimbaji na baadae Matangazo,

Katikati Ya ibada, Nilipata simu ya dharula Nikatoka nje kwa muda kidogo (Niliweka Vibration) Na ilikuwa ni simu muhimu kwa hyo ilibidi nipokee kisha Kurudi kuendelea Na Ibada.

Wakati narudi, Nilikuta sehem Niliyokaa Tayari kuna waumini wengine wamekaa na Kanisa lilishaanza kufurika, Mbele yangu kulikuwa na benchi 2 Za mwanzo ambazo bado zilikuwa bado na Ma gap, kwa hyo nikakaa benchi Moja wapo.

Mbele Yangu alikaa Mzee mmoja Ambaye nilipomwangalia, Ilikuwa tu Ni kama kapewa shati hilo sehemu, au hana option nyingine, lilikuwa ni shati Chafu, halijanyooshwa Na suruali vile vile, Pembeni alikuwa na mfuko aliobeba vitu ambavyo Sikuvijua.

Lakini pia alikuwa na kofia ambayo kwa Heshima na Madhabahu Alikuwa ameivua na kuiweka juu Ya Mfuko wake.

Mahubiri Yalianza, akawa na karatasi na kalamu anaandika na anafatilia kwa umakini,

Nilimwangalia miguuni Nikaona hana viatu na pembeni Yake kulikuwa na ndala zilizochakaa,

Muda wa sadaka ulifika, Hakusimama kwenda kutoa Sadaka. Kwanza kabla Ya sadaka nilianza kuwaza sana kuhusu Huyu mzee na passion aliyokuwa nayo licha ya kuonekana na Maisha magumu,

Alifatilia ibada, aliandika, alisikiliza kwa umakini, lakini nilimuona zaidi akiwa mnyonge wakati tunaenda kutoa sadaka na yeye hana.

Kabla hata ya kunyanyuka tayari linishawaza sana, Huyu baba huenda ana watoto tena wakubwa, Hana mavazi ya kuvutia kama wengine, Nikawa najiuliza anakula wapi? Amekujaje? Akitoka hapa anarudije? Anajisikiaje?

Nilipotoka kutoa sadaka Moyo wangu uliniambia "LEO SADAKA YANGU KUBWA NI KUMPA HUYU MZEE CHOCHOTE"
Nilimfata nikamshika mkono kama naongea nae kisha nikiwa nimekunja pesa mkononi nikampa, Akashtuka sana, kwa sababu nadhani hakutegemea, Alipoangalia mkononi, Niliona tabasamu kubwa sana kutoka kwake, Nikakunja mikono kumshukuru bila kuongea kisha nikaondoka..Alitamani aseme kitu lakini tayari Nikawa nimeshaondoka.

Jumapili ile, imenikumbusha KUTOA SADAKA sio tu kanisani au msikitini, Kuna aina Nyingi ya watu kama huyu mzee mtaani kwetu, kina mama wajane, n.k TUWAPE CHOCHOTE, tutenge siku hata moja tu unazunguka kidogo unamkuta mama anachoma mahindi nunua mhindi wako muachie hata elf 5 akawalishe wajukuu..Nadhani hizi ndio sadaka za kweli.

Poleni kwa kuwachosha na story Ndefu.
 
Cornelius ilikuaje
Matendo Ya Mitume 10

Neno: Bibilia Takatifu

Mungu Ajibu Sala Ya Kornelio

10 Katika mji wa Kaisaria aliishi afisa mmoja wa jeshi ambaye alikuwa kamanda wa kikosi cha Italia, jina lake Kornelio. 2 Yeye alikuwa mcha Mungu pamoja na jamii yake yote. Alitoa msaada kwa ukarimu kwa watu na kumwomba Mungu mara kwa mara.
3 Alasiri moja, mnamo saa tisa, malaika wa Mungu alimjia katika ndoto na kumwita, “Kornelio!” 4 Kornelio akamtazama yule malaika kwa hofu akasema, “Ni nini Bwana?” Malaika akasema, “Sala zako na sadaka ulizotoa kwa maskini zimefika mbinguni, na Mungu amezikumbuka. 5 Sasa tuma watu Jopa wakamlete Simoni ait waye Petro. 6 Yeye hivi sasa anaishi na Simoni mtengenezaji ngozi kando ya bahari.” 7 Yule malaika aliyekuwa akizungumza naye ali poondoka, Kornelio aliwaita watumishi wake wawili na mlinzi wake mmoja aliyekuwa mcha Mungu, 8 na baada ya kuwasimulia mambo yote yaliyotokea, akawatuma waende Jopa.
9 Kesho yake, walipokuwa wanaukaribia mji, Petro alipanda juu ghorofani kuomba mnamo saa sita. 10 Alipokuwa akisali aliona njaa akatamani kupata chakula. Lakini wakati kilipokuwa kinaan daliwa, alisinzia akaota ndoto. 11 Akaona katika ndoto mbingu zimefunguka na kitu kama shuka kubwa ikishushwa kwa ncha zake nne. 12 Ndani ya ile shuka walikuwemo aina zote za wanyama na nyoka na ndege. 13 Kisha sauti ikamwambia Petro, “Inuka, uchinje na ule mnyama ye yote umpendaye kati ya hawa.” 14 Petro akajibu, “La Bwana! Sijawahi kula cho chote ambacho kimetajwa na sheria zetu za Kiyahudi kuwa ni kichafu.” 15 Ile sauti ikarudia kusema naye mara ya pili, “Usiite cho chote alichokitakasa Bwana kuwa ni kichafu.” 16 Hii ilitokea mara tatu, ndipo ile shuka ikarudishwa mbinguni.
17 Petro alikuwa bado akijiuliza maana ya mambo haya aliyoy aona, wakati wale watu waliokuwa wametumwa na Kornelio walipofika kwenye nyumba ya Simoni mtengenezaji ngozi. 18 Wakabisha hodi na kuuliza kama Simoni aliyeitwa Petro alikuwa anaishi hapo.
19 Wakati huo Petro alikuwa akifikiria juu ya ile ndoto, Roho Mtakatifu akamwambia, “Wako watu watatu wamekuja kukuta futa. 20 Shuka chini ukaonane nao na usione shaka kwenda nao kwa kuwa nimewatuma kwako.” 21 Petro akashuka, akawaendea wale watu akawaambia, “Mimi ndiye mnayemtafuta. Mnataka nini?” 22 Wao wakamjibu, “Tumetumwa na Kamanda Kornelio ambaye ni mtu mwema anayemcha Mungu na kusifiwa na Wayahudi wote. Yeye ameagi zwa na malaika wa Mungu akukaribishe nyumbani kwake, ili asiki lize maneno utakayomwambia.” 23 Petro aliwakaribisha walale kwake. Kulipokucha akaandamana nao pamoja na baadhi ya ndugu waamini wa pale Jopa.

Petro Nyumbani Kwa Kornelio

24 Kesho yake wakawasili Kaisaria. Kornelio alikuwa akiwan goja pamoja na ndugu zake na marafiki wa karibu ambao alikuwa amewaalika. 25 Petro alipokuwa akiingia ndani, Kornelio alikuja kumlaki, akapiga magoti. 26 Lakini Petro akamwinua akamwambia, “Simama! Mimi ni mwanadamu tu.” 27 Petro alipokuwa akizungumza naye aliingia ndani ambapo alikuta watu wengi wamekusanyika. 28 Petro akawaambia, “Mnajua kwamba sheria ya Wayahudi hairu husu Myahudi kuwatembelea au kuchangamana na watu wa mataifa men gine kama hivi nifanyavyo. Lakini Mungu amenionyesha kwamba nisimwone mtu ye yote kuwa mchafu au asiyefaa. 29 Ndiyo sababu ulipotuma nije sikusita. Kwa hiyo naomba unieleze kwa nini ume niita.” 30 Kornelio akajibu, “Siku nne zilizopita, nilikuwa nyumbani nikisali saa kama hii, saa tisa mchana. Mara akatokea mtu aliyevaa nguo za kung’ara akasimama mbele yangu. 31 Akasema, ‘Kornelio, maombi yako yamesikiwa na Mungu, naye amekumbuka msaada wako kwa maskini. 32 Basi tuma watu waende Jopa wakamwite Simoni aitwaye Petro. Yeye ni mgeni katika nyumba ya Simoni mtengenezaji ngozi ambaye nyumba yake iko sehemu za pwani.’ 33 Ndio sababu nilituma watu kwako mara moja, nawe umefanya vizuri kuja. Basi sasa tuko hapa wote mbele ya Mungu kuyasikiliza yote ambayo Mungu amekuamuru kutuambia.”

Hotuba Ya Petro

34 “Ndipo Petro alianza kwa kusema, “Sasa naamini ya kuwa Mungu hana upendeleo. 35 Yeye huwakubali watu wa kila taifa wam chao na kutenda haki. 36 Huu ndio ujumbe ambao Mungu aliwapele kea watu wa Israeli, kuhusu Habari Njema za amani kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye ni Bwana wa wote. 37 Ninyi bila shaka mnafa hamu mambo yaliyotokea sehemu zote za Yudea, kuanzia Galilaya tangu wakati wa mahubiri ya Yohana Mbatizaji. 38 Mnafahamu jinsi Mungu alivyompa Yesu wa Nazareti Roho Mtakatifu na uwezo, na jinsi alivyozunguka kila mahali akifanya mema na kuponya wote waliokuwa wakiteswa na nguvu za shetani, kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye. 39 Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyofanya katika nchi ya Wayahudi na Yerusalemu. Walimwua kwa kumtundika msalabani. 40 Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu siku ya tatu na akamwezesha kuonekana na watu. 41 Hakuonekana kwa watu wote, lakini alionekana kwa mashahidi ambao Mungu aliwachagua, yaani sisi ambao tulikula na kunywa naye baada ya kufufuka kwake. 42 Naye alituamuru kuhubiri kwa watu wote, na kushuhudia kwamba yeye ndiye aliyechaguliwa na Mungu kuwahukumu walio hai na wafu. 43 Manabii wote walishuhudia juu yake, kwamba kila mtu amwami niye atasamehewa dhambi katika jina lake.”
 
Wachoma mahindi wana hela weweeee
We wazarau tu
Ila Mungu aikumbuke sadaka yako kama alivyoikumbuka ya cornelius
Hahaha ni kweli kabisa mkuu, Acha wale ambao unakuta kabisa yuko vizuri, lakini unakutana na Mama unaona kabisa anafanya hicho sababu ya kujaribu kujikimu tu...hali yake utaiona tu...ni vyema sana kuwasapoti na nadhani watoto au wajukuu wake wakienda kufurahia alichokipata kutoka kwako, unakuwa umerudisha tabasamu kwenye familia kwa siku hyo
 
Hahaha ni kweli kabisa mkuu, Acha wale ambao unakuta kabisa yuko vizuri, lakini unakutana na Mama unaona kabisa anafanya hicho sababu ya kujaribu kujikimu tu...hali yake utaiona tu...ni vyema sana kuwasapoti na nadhani watoto au wajukuu wake wakienda kufurahia alichokipata kutoka kwako, unakuwa umerudisha tabasamu kwenye familia kwa siku hyo
Yeah sadaka ni muhimu kwa wahitaji
 
Jumapili iliyoisha Nilienda mwenye ibada kama kawaida, nikaketi Mistari kadhaa kutoka mbele, kwa kuwa nilikuwa nimewahi,

Ibada iliendelea kwa Kwaya za kanisani kwetu kutoa ujumbe kwa njia ya uimbaji na baadae Matangazo,

Katikati Ya ibada, Nilipata simu ya dharula Nikatoka nje kwa muda kidogo (Niliweka Vibration) Na ilikuwa ni simu muhimu kwa hyo ilibidi nipokee kisha Kurudi kuendelea Na Ibada.

Wakati narudi, Nilikuta sehem Niliyokaa Tayari kuna waumini wengine wamekaa na Kanisa lilishaanza kufurika, Mbele yangu kulikuwa na benchi 2 Za mwanzo ambazo bado zilikuwa bado na Ma gap, kwa hyo nikakaa benchi Moja wapo.

Mbele Yangu alikaa Mzee mmoja Ambaye nilipomwangalia, Ilikuwa tu Ni kama kapewa shati hilo sehemu, au hana option nyingine, lilikuwa ni shati Chafu, halijanyooshwa Na suruali vile vile, Pembeni alikuwa na mfuko aliobeba vitu ambavyo Sikuvijua.

Lakini pia alikuwa na kofia ambayo kwa Heshima na Madhabahu Alikuwa ameivua na kuiweka juu Ya Mfuko wake.

Mahubiri Yalianza, akawa na karatasi na kalamu anaandika na anafatilia kwa umakini,

Nilimwangalia miguuni Nikaona hana viatu na pembeni Yake kulikuwa na ndala zilizochakaa,

Muda wa sadaka ulifika, Hakusimama kwenda kutoa Sadaka. Kwanza kabla Ya sadaka nilianza kuwaza sana kuhusu Huyu mzee na passion aliyokuwa nayo licha ya kuonekana na Maisha magumu,

Alifatilia ibada, aliandika, alisikiliza kwa umakini, lakini nilimuona zaidi akiwa mnyonge wakati tunaenda kutoa sadaka na yeye hana.

Kabla hata ya kunyanyuka tayari linishawaza sana, Huyu baba huenda ana watoto tena wakubwa, Hana mavazi ya kuvutia kama wengine, Nikawa najiuliza anakula wapi? Amekujaje? Akitoka hapa anarudije? Anajisikiaje?

Nilipotoka kutoa sadaka Moyo wangu uliniambia "LEO SADAKA YANGU KUBWA NI KUMPA HUYU MZEE CHOCHOTE"
Nilimfata nikamshika mkono kama naongea nae kisha nikiwa nimekunja pesa mkononi nikampa, Akashtuka sana, kwa sababu nadhani hakutegemea, Alipoangalia mkononi, Niliona tabasamu kubwa sana kutoka kwake, Nikakunja mikono kumshukuru bila kuongea kisha nikaondoka..Alitamani aseme kitu lakini tayari Nikawa nimeshaondoka.

Jumapili ile, imenikumbusha KUTOA SADAKA sio tu kanisani au msikitini, Kuna aina Nyingi ya watu kama huyu mzee mtaani kwetu, kina mama wajane, n.k TUWAPE CHOCHOTE, tutenge siku hata moja tu unazunguka kidogo unamkuta mama anachoma mahindi nunua mhindi wako muachie hata elf 5 akawalishe wajukuu..Nadhani hizi ndio sadaka za kweli.

Poleni kwa kuwachosha na story Ndefu.
Well done!
 
Umenikumbusha wiki iliyopita jumapili mida ya saa 1 usiku natoka soko la Kisutu pale naelekea mwendokasi pale DIT...ile napita City mall nawaona watoto wadogo tuliozoea kuwaita wa mtaani age around 7-10 wako maeneo ya parking pale wanategeshea watu wanaoshuka kwenye gari zao au wanaotoka mule ndani ya Mall walau waombe chochote.

Nikiwa naendelea kutembea nikamuona mmojawapo wa wale watoto ameketi pembeni ya barabara na hajajichanganya na wenzake kwenda kuomba...

Nikaguswa sana na wale watoto kwa umri wao kuwa pale huku wakiwa hawana uhakika wa kula, sehemu nzuri ya kulala na mahitaji mengine ya msingi.

Nilipomfikia yule dogo nikatoa kiasi cha fedha na kumwambia aende akale...akaipokea ile pesa kwa furaha na kunishukuru sana. Nikaona anawakimbilia wenzake kuwaonesha kuwa amepata fedha.

Ile feeling ya furaha ya kuweka walau tumaini kwa mtoto yule is priceless. Ijapokuwa hakikuwa kiasi kingi cha fedha..lakini atleast usiku ule alipata namna ya kupata mlo na wenzake.

Hawa watoto wanaozagaa mitaani na wahitaji wengine ukipata nafasi wasaidie....Mungu atakubariki.
 
Umefanya vizuri...
Mimi kuna program yangu ya sadaka naifanya kila week,Nataka kuacha alama kama yule Dorcas...
Kuna baraka sana katika kutoa haswa kwa wenye Uhitaji wa kweli
Hakika mkuu, tukiwa na utamaduni wa kufanya hilo ulilopanga kwanza tunatengeneza jamii moja yenye mshikamano sana, Huwa najskia raha sana kutoa kwa mtu ambaye unaona kabisa alikuwa amekosa matumaini
 
Umenikumbusha wiki iliyopita jumapili mida ya saa 1 usiku natoka soko la Kisutu pale naelekea mwendokasi pale DIT...ile napita City mall nawaona watoto wadogo tuliozoea kuwaita wa mtaani age around 7-10 wako maeneo ya parking pale wanategeshea watu wanaoshuka kwenye gari zao au wanaotoka mule ndani ya Mall walau waombe chochote.

Nikiwa naendelea kutembea nikamuona mmojawapo wa wale watoto ameketi pembeni ya barabara na hajajichanganya na wenzake kwenda kuomba...

Nikaguswa sana na wale watoto kwa umri wao kuwa pale huku wakiwa hawana uhakika wa kula, sehemu nzuri ya kulala na mahitaji mengine ya msingi.

Nilipomfikia yule dogo nikatoa kiasi cha fedha na kumwambia aende akale...akaipokea ile pesa kwa furaha na kunishukuru sana. Nikaona anawakimbilia wenzake kuwaonesha kuwa amepata fedha.

Ile feeling ya furaha ya kuweka walau tumaini kwa mtoto yule is priceless. Ijapokuwa hakikuwa kiasi kingi cha fedha..lakini atleast usiku ule alipata namna ya kupata mlo na wenzake.

Hawa watoto wanaozagaa mitaani na wahitaji wengine ukipata nafasi wasaidie....Mungu atakubariki.
Mkuu Mimi Mungu akinijalia ntakuja kusomesha mmoja wa watoto wa mitaani, Najua sitopungukiwa kitu kwa kufanya hivo, maana sijui wanangu watakuja kusaidiwa na nani nikiwa sipo
 
Back
Top Bottom