Nimeitwa Kwenye Network Marketing

Nimeitwa Kwenye Network Marketing

Kingsmann

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2018
Posts
5,184
Reaction score
19,384
Jana kuna rafiki yangu alinambia ana project fulani anayofanya na wa-Malaysia kwa hiyo mimi kama rafiki yake kipenzi angependa tu-shee hii fursa.

Nlipojaribu kumdodosa ni aina gani hiyo ya project akakataa katakata kunambia kwa madai ya kwamba hayo yote ntayajua nikishafika ofisini.

Inshort mimi nina uelewa mpana wa hizi network marketing, na najua anaenda kupigwa, lkn ngoja niingie tuu niwasikilize.

Salamu kuu hapa ni GOODMORNING muda wote, yani ni kama kale ka salamu ka HI! ambako hakanaga muda wala saa.

Ntazidi kuwapa updates.

=====================================
 
Mkuu hawa jamaa usiwape nafasi ya kuwasikiliza..yaani wana maneno matamu na nguvu ya ushawishi.
Baada ya kupigwa ndipo utakapokuja kujilaumu.

Ndio maana jamaa yako anajua kua na wewe unajua kwamba ni utapeli lakini still anakwambia uende sababu anajua wakikuweka mtu kati utakubali tu..

Kwa usalama wako.mpige chini tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waliopiga pesa na hz mambo ni wale wa mwanzo siku hz watu wajanja sana
 
Hivi kwa nn serikali isiingilie kufungia hii so called Qnet watu wanatapeliwa jmn unaambiwa pesa itarudi lkn ukweli hata anaekuambia pesa inarudi hali yake ni mbaya anamadenii kama yotee jmn mimi ni muhangaaa 🙆‍♀️🙆‍♀️🙆‍♀️..Vijana wanaingia mikopo ya riba kubwaaa wanarudi to zerooo daah
Note : mtu anapokuambia anakuitia kwenye fursa kama ni network marketing jua wewe ndio fursa hapo
 
Wapuuzi sana hao jamaa. Mtu anakuita unafikiri anakuitia kitu cha maana unafika pale unaambiwa mambo ya Goodmorning....Aghrrrr inakera sana.
Dawa yao hao ni kuwaambia ukweli vijana waache tamaa ya hela za kusadikika
 
Ao Jamaa kila mtu anakwambia kaacha kazi bank kwa ajili ya iyo project,nilipoteza rafiki pia kwa ajili ya kuniambia habari izo baada ya kuingia makumbusho kwenye jengo lao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom