Nimeibiwa laptop, msaada wa kui-trace

Nimeibiwa laptop, msaada wa kui-trace

Maega

Senior Member
Joined
Jul 10, 2010
Posts
156
Reaction score
31
Habari wadau

Wiki iliyopita niliibiwa laptop yangu lakini nilisikia kuna namna au wataalamu wanaoweza kui-trace mara tu ikiunganishwa online, je nitawapata wapi hao wataalam hapa Dar?
 
Ilibidi kutafuta kinga ya kuibiwa laptop yako kabla ya kuibiwa kwani sio laisi kutrace hiyo laptop hivihivi kama hukuisajiri kabla,unachouliza ni sawa na kuokota nazi kwenye mti wa mfenesi.
 
MKUU pole sana hao jamaa nilisikiaga wanapatikana pale bamaga maeneo ya shel hata mm nilisha wahi waona kipindi cha nyuma pale ambapo sasa hivi wanauza vyombo na bidhaa mbali mbali.

ila nilivyosikia mm ni kuwa kabla hujaibiwa unawaona nazani ww umechelewa sana mkuu.
kama upo dar fanya mpango wa kuwatafuta janja wa maeneo uliyo ibiwa watangazie dau utaipata tuu
 
Mkuu umekumbuka shuka kumekucha tayari, kwa sasa sidhan kama unaweza kufanikiwa kuipata. Sijui labda kama watatrace ip adress yake. Mimi ndomana device zangu kama simu etc. Hua naweka software ya kutrace mapema sana!
 
Habari wadau

Wiki iliyopita niliibiwa laptop yangu lakini nilisikia kuna namna au wataalamu wanaoweza kui-trace mara tu ikiunganishwa online, je nitawapata wapi hao wataalam hapa Dar?

Hapo unaulizia kununua nyingine au maana umechelewa sana
 
Habari wadau

Wiki iliyopita niliibiwa laptop yangu lakini nilisikia kuna namna au wataalamu wanaoweza kui-trace mara tu ikiunganishwa online, je nitawapata wapi hao wataalam hapa Dar?

Nenda kwa mheshimiwa maji marefu atakusaidia
 
Kama unajua IP adress yake unaweza kuitrace wakiingia online
Swali je unaijua ip address??? Na je wataalamu wa kutrace kwa kutumia ip wapo?? Polisi wetu wanaweza??? Unaijua imei yake pia??
Nje ya hapo ilibidi uweke software ya kuitrace na kuiregister kwa hao jamaa ....
 
Ingebidi uweke software ya tracking KABLA ya kuibiwa.

Hauwezi kutrace kwa IP kama baadhi wanavyodai, IP inatokana na network uliyokuwa connected na si na kompyuta hivyo akikonect kwengine anapata IP nyingine kutokana na hiyo network, hakuna uwezekano wa trace kwa IP.
 
Ingebidi uweke software ya tracking KABLA ya kuibiwa.

Hauwezi kutrace kwa IP kama baadhi wanavyodai, IP inatokana na network uliyokuwa connected na si na kompyuta hivyo akikonect kwengine anapata IP nyingine kutokana na hiyo network, hakuna uwezekano wa trace kwa IP.

NIC network interface card kila computer ya kisasa inayo hii kitu na ina address yake may be wanakosea kusema IP ila ku track NIC no. Ya comptuter ni very easy kama uliiweka kwenye tracking software...kuna tofauti ya IP ya internet na computer...
 
NIC network interface card kila computer ya kisasa inayo hii kitu na ina address yake may be wanakosea kusema IP ila ku track NIC no. Ya comptuter ni very easy kama uliiweka kwenye tracking software...kuna tofauti ya IP ya internet na computer...

Angeweka tracking software of course ni tofauti, kwa sababu software inatuma info kwenye server computer inapoconnect kwenye mtandao, hivyo itakwambia IP inayotumia hiyo laptop kwa wakati huo, ila hili nalo halisaidii bila msaada wa ISP aliyegawa hiyo IP ndo anaweza kujua ni mteja gani alikuwa ana hiyo IP kwa wakati huo, na kwa vile tunashare IPs kuna complications zaidi.

IP inategemea na network both IP ya internal network(useless kwa tracking kwa kuwa sio unique duniani) na external IP inayoonekana mtandaoni, kama unaongelea MAC address hii haiwezi kutumika kutrace computer kwa kuwa MAC haiwi transmitted kwenye internet, packet inapogonga router ya kwanza MAC address inatupwa na router.
 
Back
Top Bottom